Dr Matola PhD
JF-Expert Member
- Oct 18, 2010
- 60,050
- 104,466
Kama una matizo ya kuwa na kumbukumbu fupi, jikumbushe hapa:
Uliandika hivi:
Nikakujibu hivi:
Vipi, bado hujielewi tu?
Kwa misukule tu. Ngoja siku Jerry Slaa akishika Urais uone kama kutakuwa na upuuzi huo.
Siwezi kukataa moja kwa moja kwamba Raisi wangu kikwete amefanya mambo mazuri, wakati huo huo si kweli kwamba Nyerere ni chanzo cha uduni wa kiwango cha elimu uliopo sasa hivi, wakati huohuo naheshimu mchango na mawazo yako.
Lakini sitakubaliana na wewe kwamba serikali ya sasa imefanya juhudi za kutosha na kwa ufanisi kutatua suala la elimu.
Jitihada zaidi inahitajika na huenda kwa kushirikisha wataalam ilikuleta mabadiliko yenye tija kwa taifa. Thanks
Lakini dada yangu shule si kompyuta. Kwanza nimefanya kazi serikalini kiasi cha kujua uhalisia wa picha kama hizi. Mara nyingi kwenye mkusanyiko wa watu na matumizi ya kompyuta, nyingi huharibika.. Maofisini hii ipo sana, na ukarabati wake husubiri fungu toka serikalini au wafadhili. Sembuse kwa hizi shule? Hata kwenye vyuo vya kufundishia kompyuta utakuta ni mbovu haina mfano. Hizi picha zisituhadae hivyo. Na tujiulize wanajifunza nini hasa toka huko kwenye kompyuta? Kama hujui promo, ndio hizi. Pia kama kweli una data za hii Katanini tupe matokeo ya mwaka jana ya kidato cha nne tujue kweli shule hii ya serikali imejipambanua
Naona bado una matatizo makubwa sana ya ufahamu, si hasha leo hii Tanzania bado tupo hapa tulipo, sabau kubwa ni watu kama wewe, una mcho lakini hauna muono.
Hivi, elimu ya leo Tanzania unataka kufananisha na kipindi kipi? ni lini Tanzania iliweza kuwa na Vyuo vikuu zaidi ya 45 kwa miaka 7? Ni lini Tanzania imetoa madaktari wengi zaidi kwenye vyuo vya ndani zaidi ya kipindi hiki cha Kikwete? Ni lini Tanzania watoto wengi zaidi (asilimia 500 zaidi ya awamu iliyopita) wenye fursa ya kusoma sekondari?
Ni lini Tanzania ina vyuo vya kufundisha waalimu kwa wingi zaidi ya wakati huu wa Kikwete?
Narudia, una macho lakini hauna muono.
CC: FaizaFoxyFaiza anasema walimu wanaoandaliwa sasa watakuwa moto kweli miaka ijayo kisa wako kwenye utawala wa jk. Sasa atajitetea kuwa walimu wa walimu hao ni wa enzi za Mwalimu. Ila hii ya leo kiboko!
Na zile division zero 60% wanarudia mitihani au kuna utaratibu upi umetumika? am out sina muda wa kudebate na mtu aliyefungia akili zake kabatini na kujivika akili za maiti. Good bye.Hapo ndio ujuwe hakuna kubebwa kwa sasa. Kama hujafaulu kasome tena urudie mtihani. Unachokishangaa nini? na hao Waalimu Wao ni zao la Waalimu waleeeee wa St. Kayumba, au huelewi hilo?
haaaaha haaaha haaahaMimi ni msikilizaji mzuri wa Skonga kwani kila nikiangalia kipindi hiki siachi kucheka kwa jinsi wanetu wanavyotoa majibu ya utumbo,hii niliisikia live laini haikuwa hivyo.Binti mmoja wa kidato cha nne aliyedai kuwa anaweza sana somo la historia aliulizwawewe unatoka mkoa gani?,akajibu mkoa wa tabora,akaulizwa tena ni mtemi gani mashuhuri kutoka mkoa wa Tabora?akajibu mimi nina siku nyingi sana sijaenda Tabora hivyo watemi wa sasa hivi siwafahamu,kwa mshangao mtangazaji akamuuliza kwani wewe neno mtemi unalielewaje?binti akajibu mtemi ni mtu mbabe anayefanya fujo kwenye madisco!
Na zile division zero 60% wanarudia mitihani au kuna utaratibu upi umetumika? am out sina muda wa kudebate na mtu aliyefungia akili zake kabatini na kujivika akili za maiti. Good bye.
Kila nikipata muda huwa natazama hiki kipindi kinachorushwa katika EATV na host wake akiwa ni Allan Laki. Sina shaka na upeo wa huyu kijana maana maswali yake ya papo kwa hapo kwa wanafunzi yanatoa changamoto ya kutosha. Hofu yangu ni uelewa finyu mno wa wanafunzi ambao huwa wanakutana na maswali ya huyu kijana.
Ni vijana walio kati ya umri wa miaka 14 hadi 22 hivi. Ukiwaona kabla ya maswali ni vijana waliochangamka sana na wenye kujiamini. Confidence zao huanza kupotea pale wanapotupiwa swali la kwanza tu, mathalan tofauti kati ya trekta na katapila. Mwanafunzi anaweweseka. Glacier erosion ni nini. Mwanafunzi anaweweseka wakati amesoma hayo.
Wanafunzi hao ni werevu sana kwenye burudani lakini taaluma zao wako hoi mno. Nini kifanyike? Hili ni suala letu kujadili wote hapa.
ukitizama kile kipindi unaweza zaba mtoto wa mtu kituo cha daladala hata hajakukosea.
Unahisi na yeye ni kilaza.
sasa hapo ndipo ujue waalimu wake wanachoka kiasi gani.
Kuna siku niliwah kujiuliza mbona enzi zetu sisi akili tulikuwa nazo?? Mbona wakati ule kipindi cha mama na mwana kilikuwa na maswali lkn tulimudu kuyajibu?? Ama kipindi cha watoto wetu cha rtd??
Yumkini maisha halisi yamebadili wanetu, yumkini wazazi tumejisahau kabisa. Leo hii usishangae kwenye familia utakutana na magazeti ya udaku mwanzo mwisho kila siku lkn hukuti magazeti ya siasa, uchumi, habari na michezo.
Zile quiz kwenye magazeti zamani tulishindana kuzifaya iwe ni hesabu ama kiingereza ama sayansi ama somo lolote lile. Atlas tulitumis kujifunza dunia na mabara yake. Watoto tulijua mito mikubwa si tu tanzania bali ulimwenguni mwote. Nakumbuka mfereji mkubwa kuliko yote duniani nilijifunzia kwenye atlas (suez canal) lkn leo hii hata maziwa yaiyopo nchini mwanafunzi hajui.
Kongosho kumbuka kila mkoa tulijua ni maarufu kw akilimo cha zao gani la biahsara kwa la chakula. Tulijifunza makao makuu ya kila mkoa, pamoja na miji maarufu kila mkoa na makabila yake leo hii mwambaie mwanafunzi akutajie makabila yaliyopo kwenye mkoa wake uone kama atataja.
Lkn waulize mwanamziki gani anatoka na nani utamsikia weee bwana acha kabisa
UNASEMA MWANAFUNZI AJE AKUULIZE SWALI??Tusifike mbali sana,shule nying za goverment mjini kuna waalimu wawili wa somo moja,lakn wanafunzi hata hawamfati mwalimu kutaka kujua kitu.inashangaza mwanafunzi hata nini maana ya citizenship hajui alafu yupo form 3.inamaana form one hakusoma?la hasha bali ni wazazi kosa kubwa wanafanya kutofuatilia maendeleo ya mwanafunzi.mi nafundisha wanafunzi hata kukufata kukuuliza swali hakuna ,wakat kakosa swali na haji.nkijaribu kufatilia maendeleo yao wanasema mwalimu mnoko na anakihelehele.tatizo lipo kwa 1.mwanafunzi,2.mwalimu3.selikali.mwanafunz anatakiwa kuwa wa kwanza kujiwajibisha pia mwalimu atawa anawajibika maana anajua wanafunz watamuwajibisha
Baba V unafikiri sikuhizi mie huwa naendaga marking?? Nilishajichokea kwakeli siwez kufa kwa presha. Manake ukiona wanavyokosa unaweza kurudi ukiwa mgonjwa wa akili.ndugu yangu wee, kizazi hiki cha ipad, google na bba ni balaa tupu, mie ngachoka kabisa, nilikuwa nasahihisha mitihani ya mock last week nilitamani kulia, kazi ipo nchi hii.
Vipindi vya burudani na miziki kwenye TV za Taifa ziwe baada ya saa tatu usiku. Masaa yaliyobaki viwe vipindi vya shule na dokyumentari zinazofundisha.
Baba V unafikiri sikuhizi mie huwa naendaga marking?? Nilishajichokea kwakeli siwez kufa kwa presha. Manake ukiona wanavyokosa unaweza kurudi ukiwa mgonjwa wa akili.