Elections 2010 Slaa aunguruma Mwembeyanga, LIVE TBC1

Elections 2010 Slaa aunguruma Mwembeyanga, LIVE TBC1

Mkutano wa DR W P SLAA LIVE TOKA MwembeYanga

Nawakaribisha katika mkutano wa Mgombea uraisi kwa tiketi ya chadema DR W P SLAA unaofanyika hapa Kwenye uwanja wa Mwembe yanga watu wamejaa kweli kweli , kumefurika na kutia fora – Kuna watu wa aina mbalimbali hapa kuanzia wazee , vijana na wale watu wakati , kuanzia wamachinga mpaka wauza mitumba walioacha biashara zao kwa muda kwa ajili ya kuja kumwona dr slaa akinadi sera zake uwanjani hapa

Kwa wale walio mbali na maeneo haya wanafuatilia mkutano huu wanaweza kutazama TC1 Kuanzia saa 9 Kamili , wengine wanaweza kufuatilia kwa njia ya mtandao kama hii .

Kwa wale wanaopenda kuchangia Kampeni hizi wanaweza kutembelea blogu yetu kwa anuani www.marafikiwaslaa.blogspot.com kama una habari zaidi unaweza kututumia kupitia friendsofslaa@gmail.com

Wale wanaopenda kuchangia mkakati wa kutengeneza vipindi vya TV vinavyoendelea kurushwa kwenye vituo mbalimbali vya TV na radio wanaweza kuchangia kupitia namba

+255766334049 MPESA
+255786806028 ZAP

Kama unataka Fulana za DR SLaa na Kofia zenye sahihi yake wasiliana na 0714 667026

Kazi nzuri. Kwa vile wengine tuko kibaruani, endelea kutuletea habari zaidi. Leo ameonglea nini?

Simu ya tigo kwa ajili ta flana na kofia haipatikani. iweke on muda wote tuzipate kabla ya Jumapili. Bei?
 
Anasema uwanja wa Mwembeyanga yeye unamkumbusha mengi
 
Dah, kambamiza Lau Masha. Kasema CCM ni Chama cha Kigaidi, kinatengeneza jeshi la vijana (Green Guard?).
 
jamani anarusha bomu anasema wamekamata nyaraka za kuprove ccm wanatumia vijana, wanapelekwa kambini na kufundishwa ukakamavu, it means wanatengeneza jeshi lao la ccm
 
Its terrible my god, hawa ccm hawa, ee Mungu turehemu na utuepushe nao
 
Anasema anajua na hata kiravu anajua kwamba ccm wana uzoefu wa kuiba kura, anatoa onyo kwa tido mhando kwamba aache kukatakata matangazo (amepata taarifa) na kwamba TBC ni taasisi ya umma inayolipiwa kodi na wananchi na siyo ccm, so tido atumie busara na akishindwa adha ya wananchi itakapomshukia asimlaumu yeye, anaanza kuelezea ilani, oh Gosh i love him
 
Anasema ndo maana kikwete haoni umaskini wa watanzania kwa kuwa bagamoyo ambako ni kwake wananchi wana nyumba za mbavu za mmbwa, ukiona raisi ambaye kwake kuna hali hiyo ujue hana uona wa kitaifa, hana upendo kwa kuwa upendo huanza nyumbani.

Shaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaame, shame on you Kikwete
 
Eti taarifa iliyosomwa kwa jk na shukuru kawambwa, naye akashangilia na kumshika mkono kwambwa, vyoo vya shule kadhaa kama nne hivi kazitaja:

Kila shule kujenga vyoo vya matundu manne (choo cha shimo ofcourse) jumla wametumia sh million mia saba, kila shule, imagine kila matundu manne million mia saba, what a shame. kweli nchi imeliwa hii
 
Wakuu,

Napenda kuwafahamisha kuwa kesho Dr. Slaa atakuwa viwanja vya Mwembeyanga jijini Dar es Salaam ambapo atakuwa LIVE ndani ya TBC1 pia kuanzia saa 10 jioni kwa muda wa masaa 3.

Aidha, baadae atakuwa LIVE katika televisheni ya Agape kuanzia saa 1 jioni.

Mkutano wake leo umejaza watu wengi sana huko Zanzibar tofauti na wengi mnavyoweza kudhani, nitawaletea picha za Zanzibar hali ilivyokuwa.

Asante mkulu maana nilikuwa nimesahau kuingia tu JF, Niko naangalia live ingawa niko mererani mwanzo iliukuwa inakatakata ila sasa iko swari docta anazungumzia ujenzi wa vyoo matundu ya choo kwa docta manyaunyau milioni 700
 
Naona kaamua kumjibu Kamala, si mchezo. Anasema hahitaji PhD ya uchumi kujua hali halisi ya wananchi wake.
 
Kamchambua Kamala ile mbaya...!!!! Anasema hafai kuongoza bcoz hajui matatizo ya umasikini wa Watz.
 
Back
Top Bottom