Elections 2010 Slaa kama huwajui WATANZANIA ndio hawa

Hii mitangazaji ya BBC Swahili hovyo tu - angalia Tido Mhando halafu na lile lililoratibutu mjadala wa Baregu - Kinana. Kujipendekeza tu ili wazawadiwe posts na Kikwete.
 

Niliyasilia jana, katika watu watatu waliohojiwa wawili walisema watampigia Dr. Slaa, mmoja anapenda kwenda kumsikiliza Dr. Slaa ila atampigia Kikwete.

That's what i heard last nite
 
nanyi hamuachi kulia

polls ovyo tbc, itv ovyo radio zote ovyo

tume ya uchaguzi ovyo

obama kusema tanzania inasogea vizuri ovyo

mna kazi nyie wakukosa

sasa dunia nzima si ovyo ni chadema
 

Na hii je
 
Huo utafiti aliufanya upande mmoja tu? Hakuenda kwenye mkutano wa JK kuuliza kama watu wamehudhuria kumsikiliza au kumuona Juma Nature?
 
Yale yaliyomkuta Mrema mwaka 1995 ndio yanaelekea kumkuta Slaa,

Naam,,,

Hilo neno la pink linaonesha tu kuwa uko kidini zaidi.

Acha kutokwa jasho la kwapa.

Slaa ni namba nyingine. Mwaka 1995 hata mimi nilimpigia Mzee Mkapa.

2000 sikupiga kura kabisa baada ya kuona CCM (siyo Mkapa) imeingiliwa na Wahindi.

2005 SIKUMPIGIA KIKWETE.

2010 HATA BABA YANGU NA MAMA YANGU AMBAO NI CCM DAMU HAWAMPIGII KURA KIKWETE. FISADI!!
 
nanyi hamuachi kulia

polls ovyo tbc, itv ovyo radio zote ovyo

tume ya uchaguzi ovyo

obama kusema tanzania inasogea vizuri ovyo

mna kazi nyie wakukosa

sasa dunia nzima si ovyo ni chadema

Zuri la kusifia chama fulani unachokishabikia ila ukisema la hovyo unakuwa hovyoooooooo I love zis pipo haki ya Mungu
 
Kuna tofauti gani kati ya TBC1, REDET, SYNOVATE, KIKWETE, RIDHWANI, HALFAN, SALMA, MAKAMBA TIDO? si wote ni waajiliwa wa KIKWETE? Hayo unayoleta hapa hayana hadhi.
 

Nilikuwa Babati wiki iliyopita nikakutana na dada mmoja ninayemfahamu na nikatambua kuwa ni mwanutamaduni katika vikundi vya propaganda vya ccm. NIkamdodosa kuhusu kazi yake akaniambia kuwa pale wanafuata pesa tu, na wanachama wote wa kile kikundi kura zao ni kwa Slaa. Hii ndiyo Tanzania ya leo ndugu yangu, sio wakati wa Mrema. Ukombozi umefika, na safari hii ni zamu ya ccm kushangaa
 
Those who cast the votes decide nothing. Those who
count the votes decide everything.

- Josef Stalin



I think this time chadema will vote and count




 
E Bwanaaaaaae Watanzania (Barabara!!!!!!!???????) Nyie ,Mna uwezo wa kupanga na kutekeleza............Na nyie wagombea,hapendwi mtu hapa....Utakura kwa CV Yako......
Usitupigie manyanga mengi,ukidhani hatukukuona ulivyokuwa ukitegea Shambani !!!
 
Nawajua watu kumi wanaosoma na kuishi Kenya ambao walijiandikisha kupiga kura ili wapate vitambulisho vile kwa kuwa kumiliki kitambulisho ukiwa huko ni kitu muhimu sana. Kwa maana hiyo wamepania kuja kupiga kura kwa mara ya kwanza ili kuleta mabadiliko. Nahisi hawa wanakuja kuongeza kura za DK.Slaa.
Miaka ile watu walikuwa hawajiandikishi halafu walikuwa wanakuja kushtuka wakati kampeni zimepamba moto na mwisho wa siku hawapigi kura.

Muuaji wa SISIEM mwaka huu ni kampuni za simu na TCRA waliopiga debe kubwa wakati wa kusajili namba za simu, kuwa kitambulisho cha kupigia kura kilikuwa ni zana mojawapo muhimu kwenda kusajili. wale waliozoelewa kuitwa vibaka na wamachinga (watu waliopigika kutokana na mfumo mbaya wa utawala) wakajiandikisha na ndio hao watakaoleta mabadiliko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…