Hivi Dr. Slaa na CHADEMA mmecheck usahihi wa mifano mnayotumia?
Argument ya ukubwa wa serikali ni nzuri sana lakini mifano inayotumika haiko sahihi. Mara mbili nimesoma Dr. Slaa akitoa mfano wa UK kuwa na baraza la mawaziri dogo na kutaja namba ya 14 lakini ukweli unapingana na hayo madai yake.
Uingereza ina mawaziri wapatao 100 kama unajumlisha na mawaziri wadogo na sio 14 kama anavyodai Dr. Slaa. Pia Uingereza ina watu karibu 60M na sio 300M anavyodai Dr. Slaa. Hata ukichukulia mawaziri kamili basi wako karibu 30, sijui hiyo namba ya 14 kaitoa wapi?
Mbali na serikali ya UK yenye hao mawaziri karibu 100 pia kuna serikali ya Scotland, Wales na Northern Ireland na kwa ujumla kufanya nchi iwe na baraza kubwa sana la mawaziri.
Baraza la mawaziri la UK linaweza kupatikana hapa:
BBC News - Cameron's government: A guide to who's who