Bravo Mike
JF-Expert Member
- Apr 14, 2014
- 548
- 631
Naomba mnielekeze na aina ya vioo ambavyo havivunjiki kirahisi hasa simu ikidondoka, maana uzembe wangu upo kwenye kupasua vioo.
Thanks C/Mkwawa for useful info, nauliza, nikitaka kumnunulia mtu zawadi Samsung S 5 ya clone mpya ambaye sio mtaalam wa mambo ya sim, je ataweza kujua kama hio sio original ? Yaani kuna namna awezagundua kirahisi ?
Mkuu nakubaliana na wewe hasa kwenye kwenye gorilla glass,maana nimewai kutumia kwenye HTC desire S.1.saphire
2.gorrila glass 2
3. rugged smartphone
1.saphire screen
hivi ni vioo vigumu kushinda hata gorila glass lakini so far sijaona simu ya chini ya milioni moja yenye hivi vioo
2.gorilla glass 2
hivi ndio vipo kwenye flagship nyingi sana havipo strong sana ila vinasaidia navyo
3.rugged smartphone
hizi ni simu ambazo zimetengenezwa kuvumilia mazingira magumu na huwa si rahisi kuharibika zikidondoka mfano simu za caterpillar
Naomba utaje na simu nzuri ambazo ni bora sana za kuanzia 500k hadi milion moja kama hutojali ambazo hazifi haraka chember ya sim Card
actual lumia 520 haina c-r-a-p specs sababu even gs3 haina krait ina cortex a9, na lumia 525 inahandle game lolote la kwenye windows phone hadi magame makubwa kama gta san andrea na halo. pia si kila mtu ana uwezo wa kununua simu ya dola 300 ambayo huku itauzwa laki 6 kupanda juu.
ni wapi inapatikana kwa hyo bei ya 80000microsoft anairuzuku sana ili iuzwe bei rahisi kuna maeneo inauzwa dola 49 (80,000) ndio maana imeuza sana
Mkuu nakubaliana na wewe hasa kwenye kwenye gorilla glass,maana nimewai kutumia kwenye HTC desire S.
ila hivi vioo vya TFT naona kama chenga hivi yaani ubora wake wa kutilia shaka.
Hivyo vya saphire ni vyema ungefafanua vinatoka na simu gani Bila kujali bei.
ni wapi inapatikana kwa hyo bei ya 80000
microsoft anairuzuku sana ili iuzwe bei rahisi kuna maeneo inauzwa dola 49 (80,000) ndio maana imeuza sana
hawa Motorola wana simu nzuri kwa gharama nafu lakini upatkanaji wake ndio shida
Mi nna Lumia 710, yaani ni choo cha kike, nifanyeje ili niweze kudownload na kutumia huduma za pesa pesa?
Wana JF jaribuni kuipata TECNO PHANTOM A PLUS, hapa wameweza kwa kweli
tecno zinatumia chip ya mediatek na chip ya simu inajumuisha vitu kama hivi.
-processor
-gpu(kwa ajili ya games na app kubwa)
-fm radio
-network radio mambo ya 3g na 2g
hivyo tunaweza kusema chip zinazoekwa kwenye simu ndio kila kitu sababu mambo yote muhimu yapo kwenye hio chip, chip ikiwa mbaya na simu pia itakua mbaya. mediatek ina matatizo mengi kama.
1.inacorupt imei number na ikicorupt basi huwez piga simu wala kupokea wala kufanya karibia shughuli zote za kisimu hadi uifix.
2. huwezi kuiupdate simu ya mediatek kama inakuja na android 4.1 ili iende 4.2 inabidi ununue simu nyengine
3. simu zote za mediatek zinatumia cortex a7 ila wanatoka processor ya cortexa15 soon. hii processor ya a7 haina nguvu sana.
4. sometime vitu kama gps wifi au bluetooth pia huzingua
ina matatizo mengi meadiatek na pia simu zake ni bei rahisi sana.
incase ndio huna budi inabidi ununue simu ya mediatek zipo simu kali za around dola 130 kama xiaomi hongmi aka red rice na huawei honor 3c unaweza ukazigoogle uone zilivyokua na specs kubwa kwa bei ndogo
actual lumia 520 haina c-r-a-p specs sababu even gs3 haina krait ina cortex a9, na lumia 525 inahandle game lolote la kwenye windows phone hadi magame makubwa kama gta san andrea na halo. pia si kila mtu ana uwezo wa kununua simu ya dola 300 ambayo huku itauzwa laki 6 kupanda juu.
mkuu hio sh ngapi!?
Mkuu samahani kidogo naomba ufafanuzi hasa unaposema MTK maana yake nini?hapo kwenye kupoteza imei nadhani ni kwa wale tu wanaopenda kufanya rooting na kuweka custom roms tatizo ambalo lipo sana hata kwenye samsung. updates za kitkat za mtk mbona zipo sema ni kwa makampuni machache sana ila wenye tecno wasitegemee updates.
alafu mbona mtk6582 zina perfomance nzuri tu japo ni A7 antutu score ya 17000 plus is good enough kwa matumizi ya kawaida.
downside kubwa ni kwamba mediatek devices zinazopatikana bongo ni zile zenye quality mbovu at higher price sanasana tecno.
Mkuu samahani kidogo naomba ufafanuzi hasa unaposema MTK maana yake nini?
mediatek