Social media politics; Heri au shari? Kipi ni kipi, kwa nini, nani afanye nini na ili iwe nini

Social media politics; Heri au shari? Kipi ni kipi, kwa nini, nani afanye nini na ili iwe nini

Azizi Mussa

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2012
Posts
9,186
Reaction score
7,492
1621073339368.png
Hivi karibuni, mijadala juu ya siasa za mitandaoni zinavyoathiri siasa rasmi nchini na kuathiri maamuzi ya kitaifa imeshika kasi. Limejitokeza kundi linalofurahi kuwa maoni yao wanayoyatoa mitandaoni yanafanyiwa kazi huku kundi lingine likilalamika kuwa si sahihi kwa maoni ya watu wa mitandaoni kufanyiwa kazi wakati kwa upande mwingine kukiwa na uhakika kuwa watunga sera na wafanya maamuzi mbalimbali wanafuatilia kwa karibu mijadala ya mitandaoni na hivyo kuwaathiri kwa kiwango fulani kwenye maamuzi wanayofanya au kutofanya.

Lengo la mjadala huu ni kupanua uelewa juu ya nafasi ya mitandao ya kijamii kwenye siasa za Tanzania na duniani kwa ujumla kwenye zama hizi katika kujenga au kubomoa.

Aidha, mijadala unalenga kuchambua ni kundi gani linafanya nini huku mitandaoni, kwa nini linafanya linavyofanya, nini kinachotegemewa kutokea katika mazingira fulani fulani na nani anapaswa kufanya au kutofanya nini kwenye mazingira yetu ya Tanzania na ili iwe nini.

Katika mada hii, tutajadili kwa kina maeneo yafuatayo

1. Wanaofanya siasa mtandaoni ni kina nani hasa?

2. Malengo ya wanaofanya siasa za mitandaoni ni yapi?

3. Tafiti zinasemaje kuhusu siasa za mitandaoni na muelekeo wa siasa za dunia (Social media politics Vs actual field politics)

4. Nguvu ya mitandao ya kijamii kwenye siasa ni kubwa kwa kiasi gani? na hiyo maana yake ni nini?

5. Huko duniani wanafanya nini na ili iwe nini?

6. Hapa kwetu tanafanya nini na kwa nini na hatma yake ni nini?

7. Uzandiki mitandaoni na kwa nini?

8. Nani anapaswa kufanya nini na ili iwe nini?

9. Vikwazo ni nini kwenye kuchukuwa hatua sahihi na ni vipi tunaweza kuvivuka.

10. Ni nini kitatokea kama ikiachwa ‘nature’ iamue.
 
Back
Top Bottom