soda hii ni hatari kwa maisha yetu


We ndo wale wa kupenda kufunika kombe mwanaharamu apite ulitaka niipeleke cocacola ili tuyamalize kienyeji hapa JF ndo mtambo wa kurekebisha tabia za uzembe siendekezi njaa kama unahitaji tafuta soda iliyo na makondomu uipeleke kiwandani watakupa japo kreti na vijisenti vya kununulia bamia hapa JF ujumbe umewafikia na jamii nzima inapaswa kujihadhari wakati wa kunywa soda.JF idumu na kudumu vizabinazabina ndo mnaiwekea usiku,,,,n2twork search,.....
 
Pole sanaaaaaaaa mkuu ]mimi december nilinunu sprite pale kimara mwisho nikiwa nahis i nimeshiba na soda bado ipo nikaona heri niichezeshe gesi itoke nilipoimwaga kinywani nikasikia kitu kigumu kama kina miguu nikawahi kukirudisha katikati kutema hivi inzi wa choooni wa kijani kabisaaaaaaaa kwa sababu ya garama ya ile soda nikamrudisha kinywaniiii nikamkamua nikammtupa na maneno ya nenda kaanze maisha yako mapya ..so sioni cha kushangaza ingawa vizuri kuwajulisha watengenezaji ukikutana na nzi ama mende usimwache aende hivihivi mkamue alafu mteme mwambie akaanze maisha mapya
 
Soda hii naitunza kama ukumbusho wangu baada ya kuacha kunywa soda rasmi.maisha yetu ya kibongo kuhifadhi vitu kwenye chupa then hazioshwi tunanyweshwa masumu kila siku no wonder kuna magonjwa ya ajabu ajabu tunapata cku hz!!

Pole kwa mkasa uliokupata; lakini tujiulize wa kulaumiwa ni nani?. Jamii yetu inapaswa kulaumiwa kwa kutokujali maisha ya mwingine, inakuwaje chupa ya soda ambayo unajua itatumika na mwingine halafu unaweka vitu visivyostahili ndani yake. Kumbuka hizi chupa zinaoshwa kwa mashine, hivyo basi inategemea mashine imeundwa kwa kutoa taka za namna gani. Ni wajibu wa kila mmoja wetu kujali maisha ya mwingine, leo wewe unalalamika kwasababu limetokea kwako, lakini na wewe jiulize ni kwa kiwango gani unajali maisha ya wengine, ulishawahi kuona jiwe barabara na ukaamua kuliondoa ili mwingine asijikwae, ulishawahi kuona mwiba barabarani ukaamua kuondoa ili mwingine asichomwe na mambo mengineyo; hivyi ndivyo vipimo vya kujali wengine.
 
vinywaji vingi sana hapa nchini tunakunywa uchafu
nilishanunua pepsi zaidi ya mbili na kukuta uchafu wa ajabu humo ndani,kibaya zaidi nilikuwa nimeshakunywa kama robo soda
 

mungu wanguuuuuuuu eeeeeeeeehhhhhhhhhhhhhh unarudi kwenye wanzuki tenaaaaaaaaaaa aiseeeeeeeee
tulijua soda zitakusahaulisha kule sasa ukiacha uko yewoooooooooooooomiiiiiiiiiiiiiiii apawasauyooooooooooooooooooooooooooo noshaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Ndugu ni kumshukur mungu tu umeona basi maisha yanaenda mbele
nikianza tu na huu uchafu wa mafuta ya kula...tumekuwa tukikimbia sana mafuta ya korie weeeeee lakini nikwambia kuna nyumba mbili pale sinza makaburini na moja pale afrika sana kazi yao ni kuchanganya mafita ya sundrop na korie then inafungwa kwenye dumu la sundrop we unajua haya ni sundrop kumbe mix ya korie

anyway turudi wale wenyeji wa value...unajua pale nyuma ya bar ya hongera nahisi ni nyumba ya tau ama tano kuna nyumba inakazi ya kutengeneza valueee na konyagi pori..ndio maana nenda kachukue value ya afrika sana nuonje kidogo uone mdundulizo wake then ukaonje na za supermarket ni hatari ndugu..hizi konyagi zenyewe unaambiwa moja ya mixer ni mtu kunywa maji alafu anakojoa kwenye ndoo zikijaa zile..zinaanza kuchanganywa na mambo mengine ukionja nakwambia utaipenda nenda kwenye lebo zina hadi nenmbo ya tra kwa juu tbs imeikumbatia usiniulize zinatoka wapi

ukija kwenye mafuta ya magari huko sisemi maana serikali wameshaidhinisha naamni sio mpya kwako kama ushawai kujaza mafuta ukajua unaweka mafuta ya petrol ujue ya taa yako pembeni yake lakin gari linasonga mbele ..nasema kazi ipo kubwaaaaaaaa
 

punguza jazba nadhani nia ya mleta mada ilikuwa kupata usahuri au mwongozo afanye nini koz uelewa unatofautiana toka kwa mtanzania mmoja hadi mwingine.. nadhani ushauri wako ameuchukua, ujuha wako wa hasira amekuachia. lakini pia coca cola watapata taarifa kwa njia moja au nyingine kwa mada kuletwa hapa siyo lazima kwenda,,, mbaya ingekuwa kukaa kimya kabisa juu ya hiyo soda.
 
Hivi bado kuna watu wanakunywaga soda??? Mimi niliacha siku nyingiii. Sioni faida yake! Niige ukipenda!
 

Mkuu umenena vema; mhusika kuonyesha kwamba anajali maisha ya wengine alipaswa kuripoti kiwandani au ofisi husika ili hatua ziweze kuchukulia, kwani hapa inaonekana anataka kutushawishi kwamba tuache kunywa soda; jambo ambalo siyo sahihi. Mimi nilishawahi kununua chapati za bakhersa na ndani (katikati ya chapati) nilikuta glooves, nilichukua ile package na kupeleka kwenye duka la bakhresa na nilimuomba muuzaji afikishe ujumbe kunako husika, hata hivyo muuzaji alinishukuru sana na kuniahidi kuchukua hatua.
 

Mkuu kwa style yako ambayo unashawishi watu kwa kuona uzembe mkubwa hivyo kukaa kimya na kukimbilia kiwandani kuripoti mie naona haitoshi,alivyofanya huyu kuitangaza na kuipiga picha ni sawa kabisa.

Nyie kila siku mnatangaza product zenu kwenye tv mabango etc kuwa zina ubora kumbe mnakuwa wazembe mnaachia kondom na matakataka mengine ndani halafu mnafunga watanzania midomo wasitangaze,hiyo ni sawasawa na mgomo pale muhimbili watu wanakufa ovyo halafu unafunga mdomo watu,wanaharakati na waandishi kupigia kelele,huo ni uzembe wa hali ya juu kama zingekua nchi za wenzetu ni issue kubwa sana hiyo sio nyepesinyepesi kama ulivyoichukulia.

Suala lingine ambaloo umeliongelea hapo mie kwangu naona ni la kipumbavu,uzembe wa management yenu ya kusimamia wafanyakazi kwa makini kwa kufuata procedure zilizopo ndio utufumbe mdomo eti ni kutetea ajira ya watz wenzetu kwa hiyo tuendelee kunywa uchafu?Naomba sana usichukulie umasikini wetu sisi watanzania kama mtaji wa kutulisha uchafu eti tuogope kufukuzwa kazi.

Kwanza wewe utakua sio mtanzania kama ni mtz basi utakua ni kibaraka wa hao makaburu manake unaonekana unawalamba miguu sana mara oo tigo mzungu kilichobaki kwako ni kuwaabudu.

Jamani watanzania wenzangu nasema tunaweza tusijizaraulishe wala tusikubali kuzarauliwa na vibaraka wa wazungu.

Mie ni mpenzi mkubwa sana wa soda ya cocacola,Napenda kuchukua nafasi hii kuiomba serikali kupitia mashirika yake ya viwango kufanya suprise visit katika kiwanda hicho cha soda angalao twice a monthy ili kuweza kuthibitisha ubora wa vinywaji wanavyotengeneza.
 
Error zipop tu mama, hata kwenye noti ya Dollor huwa zinatokea! Sijui uoshaji wao uko vp, na uhakiki kabla ya kuruhusu chupa itumike ukoje; vyote kwa vyote error huwa zinatokea. Vp una mpango wa kuwawajibisha?
ingekuwa ni majuu weeeeeeeee ushapata mshiko wa nguvu na kampuni fungaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa hapana chezea ulaya
 
Soda hii naitunza kama ukumbusho wangu baada ya kuacha kunywa soda rasmi.maisha yetu ya kibongo kuhifadhi vitu kwenye chupa then hazioshwi tunanyweshwa masumu kila siku no wonder kuna magonjwa ya ajabu ajabu tunapata cku hz!!

Imefunguliwa????
 
Mimi tena miezi takribani nane iliyopita,niliagiza chakula,nikala nikashiba... Nikaagizia Fanta baridi... Alipofungua tu,na chupa ilitingishika,nikaona nyuzi nyembamba ndefu, nyingi kama nywele za kihindi.. Kumwonesha muuzaji, akanibadishia na kunipa
 
Mimi siku hizi nakunywa Pepsi... Sijapata nazo taabu yoyote..
 
Mkuu mopaozi tafadhari rudisha soda kwenye deport tena udai dameges!!! Otherwise usiifungue weka lawyer claim damages ili liwe fundisho wawe makini kwenye production!!! Pole!!!

 
Wacha woga hiyo si kazi yako kuna watu kazi yao nihiyo ya Law, wape Lawyers kesi wapambane na hicho kiwanda siku nyingine watakuwa na adabu!!!Wanaweza kuamua msolve hii issue out of court kwa maana itawaaribia biashara!!!!

 

mkuu ungejitapisha bana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…