Soko la Bwawani Kinondoni lililogharimu Sh Bilioni 1 linaelekea kuwa makumbusho, lipo hoi hakuna Wafanyabiashara

Soko la Bwawani Kinondoni lililogharimu Sh Bilioni 1 linaelekea kuwa makumbusho, lipo hoi hakuna Wafanyabiashara

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Licha ya Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam kubainisha wazi tija ambazo zinatokana na uwepo wa Soko la Bwawani, lakini katika hali ya kusikitisha soko hilo limeanza kuwa makumbusho hata kabla ya miaka 5.

Kwenye soko hilo maeneo ya biashara ni matupu hakuna wafanyabiashara, vizimba vipo wazi hakuna shughuli za kibiashara zilizokusudiwa ambazo zinaendelea kwenye soko hilo.

Taarifa iliyochapishwa kwenye ukurasa rasmi wa tovuti ya Manispaa ya Kinondoni awali ilieleza tija mbalimbali zinapatikana kwenye soko hilo, ambazo ni pamoja fursa za urasimishaji kwa wafanyabiashara,
Ajira na kujiajiri, Fursa za usafirishaji mizigo na abiria,Fursa za elimu ya biashara.
fremu bwawani.jpg

photo_2024-10-15_12-27-40 (2).jpg

photo_2024-10-15_12-27-18.jpg
Katika hayo yote ambayo walibainisha wazi hakuna kinachoendelea eneo hilo, soko lipo hoi hata dhamira zao nyingine kwamba soko hilo litawezesha mazingira bora ya biashara hasa kwa makundi ya wanawake na vijana kwa pamoja ili wajikwamue kiuchumi, kujiongeza kipato na kupunguza tatizo la ajira hasa kwa vijana na kina mama kwa kuwarasimisha wajasiriamali hao wadogo, hali iliyopo ni mbingu na aridhi baina ya dhamira hizo na uhalisia uliopo sasa.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka kwenye tovuti ya Manispaa ya Kinondoni Soko la Bwawani ni mradi ambao umetekelezwa katika Manispaa ya Kinondoni kupitia mradi wa uboreshaji miundombinu katika Jiji la Dar es Salaam (DMDP) kwa (Package 6) kwa gharama ya fedha za kitanzania shilingi bilioni 1.
photo_2024-10-15_12-26-37 (3).jpg
Soko hilo kutotumika ipasavyo kuingiza mapato ni uzembe wa wasimamizi kukosa uwajibikaji stahiki. Kuna wakati unajiuliza hivi mamlaka huwa zinafikiri nini kujenga masoko ya gharama kubwa kwenye maeneo ambayo hayana mwingiliano mkubwa wa watu (maeneo rafiki ya kimkakati).

Basi kama mamlaka zimeshindwa kusimamia soko hilo la Bwawani ufanyike mchakato wa wazi ili miundombinu iliyopo itumike kwenye shughuli nyingine za kiuchumi ambazo zinaweza kuingiza mapato kuliko kinachoendelea kwa sasa, tutakuja kulipishwa mikopo ambayo haijaleta tija kutokana na uzembe wa Watu wachache ambao wamepewa dhamana kwa kushindwa kuwajibika na kuwa wabunifu.

photo_2024-10-15_13-03-16.jpg

photo_2024-10-15_13-03-17.jpg
 
Aliyetoa maelekezo ya kujengwa hilo soko anatakiwa kushtakiwa kwa matumizi mabaya ya uongozi
 
Licha ya Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam kubainisha wazi tija ambazo zinatokana na uwepo wa Soko la Bwawani, lakini katika hali ya kusikitisha soko hilo limeanza kuwa makumbusho hata kabla ya miaka 5.

Kwenye soko hilo maeneo ya biashara ni matupu hakuna wafanyabiashara, vizimba vipo wazi hakuna shughuli za kibiashara zilizokusudiwa ambazo zinaendelea kwenye soko hilo.

Taarifa iliyochapishwa kwenye ukurasa rasmi wa tovuti ya Manispaa ya Kinondoni awali ilieleza tija mbalimbali zinapatikana kwenye soko hilo, ambazo ni pamoja fursa za urasimishaji kwa wafanyabiashara,
Ajira na kujiajiri, Fursa za usafirishaji mizigo na abiria,Fursa za elimu ya biashara.
Katika hayo yote ambayo walibainisha wazi hakuna kinachoendelea eneo hilo, soko lipo hoi hata dhamira zao nyingine kwamba soko hilo litawezesha mazingira bora ya biashara hasa kwa makundi ya wanawake na vijana kwa pamoja ili wajikwamue kiuchumi, kujiongeza kipato na kupunguza tatizo la ajira hasa kwa vijana na kina mama kwa kuwarasimisha wajasiriamali hao wadogo, hali iliyopo ni mbingu na aridhi baina ya dhamira hizo na uhalisia uliopo sasa.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka kwenye tovuti ya Manispaa ya Kinondoni Soko la Bwawani ni mradi ambao umetekelezwa katika Manispaa ya Kinondoni kupitia mradi wa uboreshaji miundombinu katika Jiji la Dar es Salaam (DMDP) kwa (Package 6) kwa gharama ya fedha za kitanzania shilingi bilioni 1.
Soko hilo kutotumika ipasavyo kuingiza mapato ni uzembe wa wasimamizi kukosa uwajibikaji stahiki. Kuna wakati unajiuliza hivi mamlaka huwa zinafikiri nini kujenga masoko ya gharama kubwa kwenye maeneo ambayo hayana mwingiliano mkubwa wa watu (maeneo rafiki ya kimkakati).

Basi kama mamlaka zimeshindwa kusimamia soko hilo la Bwawani ufanyike mchakato wa wazi ili miundombinu iliyopo itumike kwenye shughuli nyingine za kiuchumi ambazo zinaweza kuingiza mapato kuliko kinachoendelea kwa sasa, tutakuja kulipishwa mikopo ambayo haijaleta tija kutokana na uzembe wa Watu wachache ambao wamepewa dhamana kwa kushindwa kuwajibika na kuwa wabunifu.

Hivi u meya hakunaga kikomo? Maana huyo Songoro mnyonge Yuko muda mrefu sana hapo kinondoni
 
Licha ya Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam kubainisha wazi tija ambazo zinatokana na uwepo wa Soko la Bwawani, lakini katika hali ya kusikitisha soko hilo limeanza kuwa makumbusho hata kabla ya miaka 5.

Kwenye soko hilo maeneo ya biashara ni matupu hakuna wafanyabiashara, vizimba vipo wazi hakuna shughuli za kibiashara zilizokusudiwa ambazo zinaendelea kwenye soko hilo.

Taarifa iliyochapishwa kwenye ukurasa rasmi wa tovuti ya Manispaa ya Kinondoni awali ilieleza tija mbalimbali zinapatikana kwenye soko hilo, ambazo ni pamoja fursa za urasimishaji kwa wafanyabiashara,
Ajira na kujiajiri, Fursa za usafirishaji mizigo na abiria,Fursa za elimu ya biashara.
Katika hayo yote ambayo walibainisha wazi hakuna kinachoendelea eneo hilo, soko lipo hoi hata dhamira zao nyingine kwamba soko hilo litawezesha mazingira bora ya biashara hasa kwa makundi ya wanawake na vijana kwa pamoja ili wajikwamue kiuchumi, kujiongeza kipato na kupunguza tatizo la ajira hasa kwa vijana na kina mama kwa kuwarasimisha wajasiriamali hao wadogo, hali iliyopo ni mbingu na aridhi baina ya dhamira hizo na uhalisia uliopo sasa.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka kwenye tovuti ya Manispaa ya Kinondoni Soko la Bwawani ni mradi ambao umetekelezwa katika Manispaa ya Kinondoni kupitia mradi wa uboreshaji miundombinu katika Jiji la Dar es Salaam (DMDP) kwa (Package 6) kwa gharama ya fedha za kitanzania shilingi bilioni 1.
Soko hilo kutotumika ipasavyo kuingiza mapato ni uzembe wa wasimamizi kukosa uwajibikaji stahiki. Kuna wakati unajiuliza hivi mamlaka huwa zinafikiri nini kujenga masoko ya gharama kubwa kwenye maeneo ambayo hayana mwingiliano mkubwa wa watu (maeneo rafiki ya kimkakati).

Basi kama mamlaka zimeshindwa kusimamia soko hilo la Bwawani ufanyike mchakato wa wazi ili miundombinu iliyopo itumike kwenye shughuli nyingine za kiuchumi ambazo zinaweza kuingiza mapato kuliko kinachoendelea kwa sasa, tutakuja kulipishwa mikopo ambayo haijaleta tija kutokana na uzembe wa Watu wachache ambao wamepewa dhamana kwa kushindwa kuwajibika na kuwa wabunifu.

Hawakufanya utafiti wa kutosha. Wachuuzi hawahitaji hayo majengo.
 
Hivo vizimba waongeze ukuta viwe vyumba kwa wanaolala nje
 
Back
Top Bottom