DOKEZO Soko la Kijichi (Temeke) limejengwa kwa Mamilioni ya mkopo wa Benki ya Dunia lakini halitumiki, nini hatima yake?

DOKEZO Soko la Kijichi (Temeke) limejengwa kwa Mamilioni ya mkopo wa Benki ya Dunia lakini halitumiki, nini hatima yake?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607

Hali ya soko la Kijichi lililopo kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Temeke ambalo lilijengwa kupitia mradi wa uboreshaji wa miundombinu katika Jiji la Dar es Salaam (DMDP).

Soko la Kijichi lililopo Halmashauri ya Manispaa ya Temeke ambalo lilijengwa kwa gharama kubwa lipo tupu na halitumiki.

Soko hilo lilijengwa kupitia mradi wa uboreshaji wa Miundombinu katika Jiji la Dar es Salaam (DMDP) kwa mkopo wa Benki ya Dunia (WB), ulizinduliwa Septemba 2019 ukihusisha uwepo wa miundombinu mbalimbali ikiwemo jengo kubwa la ghorofa ambalo lilikusudiwa kutumiwa kama ofisi na huduma mbalimbali zinazoenda sambamba maendeleo ya soko hilo.

Kwa mujibu wa Gazeti la Mwananchi la Jumatano, Agosti 21, 2019 lilieleza kuwa Mkopo huo wa Benki ya Dunia ulitumika kugharamia miradi ya soko hilo na mengine mawili ya Mbagala na Mkangarawe kwa thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 3.

Mradi huo ambao umetumia mamilioni ya shilingi, matarajio yaliyokuwepo yameyeyuka, soko lipo tupu na hakuna jambo lolote linaendelea ndani ya soko hilo.

photo_2024-07-04_10-07-03 (5).jpg
photo_2024-07-04_10-07-03 (2).jpg

Jambo la kusikitisha na kushangaza ni kwamba, Serikali iliwekeza miundombinu ya daladala pembezoni mwa soko hilo, lakini eneo hilo limebakia kama ukumbusho, hakuna kinachoendelea, licha kuwa mwaka mwishoni mwa mwaka 2022 eneo hilo liligeuzwa Stendi ya Mabasi huku jengo la ghorofa ambalo ni sehemu ya mradi wa soko likigeuzwa ofisi za kukatia tiketi.

Hata hivyo hali hiyo haikudumu zaidi ya miezi miwili, ambapo Watu wa mabasi walilalamika kisha kurejea eneo la Mbagala kama ilivyokuwa awali kabla ya kuhamishiwa Kijichi.

Inaelezwa kuwa baadhi ya viongozi hususani ngazi ya Halmashauri ya Manispaa ya Temeke wamekuwa wakitembelea mradi huo, lakini hakuna kinachoendelea soko limebakia wazi bila kuingiza chochote chenye tija kwa Serikali hata kwa wananchi kama ilivyotarajiwa.

Inaelezwa na wakazi kwamba Rais Samia Suluhu Hassan wakati akiwa Makamu wa Rais, alifanya ziara kwenye mradi huo wa soko la Kijichi, ambapo alionesha kushangazwa na mradi huo kuwekwa kwenye eneo hilo, akisimamia hoja kwamba eneo limejitenga na jamii na akashauri daladala zinazoenda Kijichi zifike hadi sokoni ili angalau kuchochea mzunguko wa biashara.
photo_2024-07-04_10-07-04.jpg

photo_2024-07-04_10-07-03 (3).jpg

photo_2024-07-04_10-07-03 (6).jpg

Kulingana na mandhari iliyopo katikati eneo la karibu linalozunguka mradi huo, umezungukwa na makazi hasa ya watu wenye uwezo kiuchumi huku makazi mengi ya eneo hilo yakionekana kwa wingi yakiwa ndani ya fensi.

Baadhi ya Wafanyabiashara ambao awali walikuwa kwenye soko hilo wanadai watu wengi ambao wanazunguka eneo hilo walikuwa hawalitegemei zaidi kupata huduma.

Pia kuwategemea wanunuzi wengine ilikuwa jambo gumu kutokana na mwelekeo lilipo soko hilo, hali ambayo ilikuwa ikipelekea bidhaa zao mara kwa mara kuoza na kuwasababishia hasara kwenye mitaji yao ambayo walikuwa wamewekeza.

Kutokana na hali hiyo ilivyo kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa, hivi mamlaka husika zinafikira nini kuhusu mradi huo, ikizingatiwa pesa zilizotumika kufanikisha uwepo wa mradi huo ni za mkopo ambazo zinatakiwa kurejeshewa.

Hivi mwelekeo wa Mradi huo ni nini? Serikali imeamua kuuacha ufe, kama ni mkopo, fedha za kulipa madeni zinatoka wapi au ni kwenue miradi mingine ambapo walipa kodi wanakatwa fedha zao na kulipia mradi ambao umetelekezwa?

Majibu ya Serikali kuhusu Soko la Kijichi ~ Serikali yafikiria kubadili matumizi ya Miundombinu iliyojengwa kwaajili ya Soko la Kijichi (Temeke)
 
Ndio hasara hizo za watu wa maofisini kulazimisha masoko maeneo ambayo natural factors zinakataa.

Masoko yajengwe maeneo ambayo yanatumika wakati huo
 
Mbona hata mbagala kuu na yombo masoko yake yana hali kama hii?. Masoko mengi hayajaanzaga kutengewa eneo. Watu tu wnaanzishaga vijiwe na kukua kuwa soko. Haya yanat3ngewq maeneo yanaletag shida. Hata machinga complex floor za juu kule hakuna watu na hukh chini wamejazana kujenga vibanda kwenye mitaro
 
DMDP wana lengo zuri ila wapigaji ni wengi sana kwenye miradi yake.
 
SOKO LIMEJENGWA MAENEO AMBAYO NI YA WATU WA DARAJA LA JUU KIMAISHA, MANUNUZI WANAFANYIA UKO MJINI WANAWEKA STOCK NDANI NANI APOTEZE MUDA WAKE KWENDA UKO KUFANYA MANUNUZI WAKATI MAGENGE YAPO UKO MTAANI
 
Watanzania hawapendi kua organized. Ni changamoto sana.

Ndio maana hata maduka ama shopping centres hazikai Tanzania, zinakufa mapema.

Watanzania wamezoea kwa mama ntilie.
 
View attachment 3033328
Hali ya soko la Kijichi lililopo kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Temeke ambalo lilijengwa kupitia mradi wa uboreshaji wa miundombinu katika Jiji la Dar es Salaam (DMDP).

Soko la Kijichi lililopo Halmashauri ya Manispaa ya Temeke ambalo lilijengwa kwa gharama kubwa lipo tupu na halitumiki.

Soko hilo lilijengwa kupitia mradi wa uboreshaji wa Miundombinu katika Jiji la Dar es Salaam (DMDP) kwa mkopo wa Benki ya Dunia (WB), ulizinduliwa Septemba 2019 ukihusisha uwepo wa miundombinu mbalimbali ikiwemo jengo kubwa la ghorofa ambalo lilikusudiwa kutumiwa kama ofisi na huduma mbalimbali zinazoenda sambamba maendeleo ya soko hilo.

Kwa mujibu wa Gazeti la Mwananchi la Jumatano, Agosti 21, 2019 lilieleza kuwa Mkopo huo wa Benki ya Dunia ulitumika kugharamia miradi ya soko hilo na mengine mawili ya Mbagala na Mkangarawe kwa thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 3.

Mradi huo ambao umetumia mamilioni ya shilingi, matarajio yaliyokuwepo yameyeyuka, soko lipo tupu na hakuna jambo lolote linaendelea ndani ya soko hilo.
Jambo la kusikitisha na kushangaza ni kwamba, Serikali iliwekeza miundombinu ya daladala pembezoni mwa soko hilo, lakini eneo hilo limebakia kama ukumbusho, hakuna kinachoendelea, licha kuwa mwaka mwishoni mwa mwaka 2022 eneo hilo liligeuzwa Stendi ya Mabasi huku jengo la ghorofa ambalo ni sehemu ya mradi wa soko likigeuzwa ofisi za kukatia tiketi.

Hata hivyo hali hiyo haikudumu zaidi ya miezi miwili, ambapo Watu wa mabasi walilalamika kisha kurejea eneo la Mbagala kama ilivyokuwa awali kabla ya kuhamishiwa Kijichi.

Inaelezwa kuwa baadhi ya viongozi hususani ngazi ya Halmashauri ya Manispaa ya Temeke wamekuwa wakitembelea mradi huo, lakini hakuna kinachoendelea soko limebakia wazi bila kuingiza chochote chenye tija kwa Serikali hata kwa wananchi kama ilivyotarajiwa.

Inaelezwa na wakazi kwamba Rais Samia Suluhu Hassan wakati akiwa Makamu wa Rais, alifanya ziara kwenye mradi huo wa soko la Kijichi, ambapo alionesha kushangazwa na mradi huo kuwekwa kwenye eneo hilo, akisimamia hoja kwamba eneo limejitenga na jamii na akashauri daladala zinazoenda Kijichi zifike hadi sokoni ili angalau kuchochea mzunguko wa biashara.
Kulingana na mandhari iliyopo katikati eneo la karibu linalozunguka mradi huo, umezungukwa na makazi hasa ya watu wenye uwezo kiuchumi huku makazi mengi ya eneo hilo yakionekana kwa wingi yakiwa ndani ya fensi.

Baadhi ya Wafanyabiashara ambao awali walikuwa kwenye soko hilo wanadai watu wengi ambao wanazunguka eneo hilo walikuwa hawalitegemei zaidi kupata huduma.

Pia kuwategemea wanunuzi wengine ilikuwa jambo gumu kutokana na mwelekeo lilipo soko hilo, hali ambayo ilikuwa ikipelekea bidhaa zao mara kwa mara kuoza na kuwasababishia hasara kwenye mitaji yao ambayo walikuwa wamewekeza.

Kutokana na hali hiyo ilivyo kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa, hivi mamlaka husika zinafikira nini kuhusu mradi huo, ikizingatiwa pesa zilizotumika kufanikisha uwepo wa mradi huo ni za mkopo ambazo zinatakiwa kurejeshewa.

Hivi mwelekeo wa Mradi huo ni nini? Serikali imeamua kuuacha ufe, kama ni mkopo, fedha za kulipa madeni zinatoka wapi au ni kwenue miradi mingine ambapo walipa kodi wanakatwa fedha zao na kulipia mradi ambao umetelekezwa?
Punguza shobo kwenye ulaji wa watu
 
SOKO LIMEJENGWA MAENEO AMBAYO NI YA WATU WA DARAJA LA JUU KIMAISHA, MANUNUZI WANAFANYIA UKO MJINI WANAWEKA STOCK NDANI NANI APOTEZE MUDA WAKE KWENDA UKO KUFANYA MANUNUZI WAKATI MAGENGE YAPO UKO MTAANI
Mbon soko la mbagala kuu limefeli?
Hapa tuangalie uchumi, utamaduni na historia ya watu wa maeneo husika kabla hujawapelekea maendeleo yoyote
 
Stendi ya daladala irudishwe uko uko na wafanya biashara wanao weka /uzia bidhaa zao mabarabarani watolewe wote wapelekwe hapo sokoni wateja wata wafuata tu tofauti na hapo soko ilo litakufa pasipo kuingiza chochote
 
Zipo factor kadhaa
1. Kujengwa mahali pasipo sahihi na lengo lake
2. Gharama za pango hazifanywi halisi. Utashangaa pembeni kuna banda wakati kwebye jengo kuko wazi mf Machinga complex
3. Ukosefu wa miundo mbinu saidizi mfano uasafiriwa raia i.e bus
4. Uchumiwa eneo husika hauhusiani na kazi ya huo mradi
Hayana mengine mengi yapo masoko mengi yalijengwa miaka ya nyuma vijijjini mahali ambapo watu hawahitaji mfano kijijini ambako hawanunui mahindi
maana wanalima karibu
wote. Nchi ina wataalam wasiotumia utaalam au utaalam wao hupingwa na wana siasa
 
SOKO LIMEJENGWA MAENEO AMBAYO NI YA WATU WA DARAJA LA JUU KIMAISHA, MANUNUZI WANAFANYIA UKO MJINI WANAWEKA STOCK NDANI NANI APOTEZE MUDA WAKE KWENDA UKO KUFANYA MANUNUZI WAKATI MAGENGE YAPO UKO MTAANI
Hilo ndio walilokosea, huko kijichi soko limewekwa maeneo ambayo wakazi wake wananunua stock ya week au mwezi maeneo km kkoo, temeke stereo au ilala.
 
Daaaah 😂 😂 nakumbukaa sana walianza kwa morarii kubwaa s
View attachment 3033328
Hali ya soko la Kijichi lililopo kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Temeke ambalo lilijengwa kupitia mradi wa uboreshaji wa miundombinu katika Jiji la Dar es Salaam (DMDP).

Soko la Kijichi lililopo Halmashauri ya Manispaa ya Temeke ambalo lilijengwa kwa gharama kubwa lipo tupu na halitumiki.

Soko hilo lilijengwa kupitia mradi wa uboreshaji wa Miundombinu katika Jiji la Dar es Salaam (DMDP) kwa mkopo wa Benki ya Dunia (WB), ulizinduliwa Septemba 2019 ukihusisha uwepo wa miundombinu mbalimbali ikiwemo jengo kubwa la ghorofa ambalo lilikusudiwa kutumiwa kama ofisi na huduma mbalimbali zinazoenda sambamba maendeleo ya soko hilo.

Kwa mujibu wa Gazeti la Mwananchi la Jumatano, Agosti 21, 2019 lilieleza kuwa Mkopo huo wa Benki ya Dunia ulitumika kugharamia miradi ya soko hilo na mengine mawili ya Mbagala na Mkangarawe kwa thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 3.

Mradi huo ambao umetumia mamilioni ya shilingi, matarajio yaliyokuwepo yameyeyuka, soko lipo tupu na hakuna jambo lolote linaendelea ndani ya soko hilo.

Jambo la kusikitisha na kushangaza ni kwamba, Serikali iliwekeza miundombinu ya daladala pembezoni mwa soko hilo, lakini eneo hilo limebakia kama ukumbusho, hakuna kinachoendelea, licha kuwa mwaka mwishoni mwa mwaka 2022 eneo hilo liligeuzwa Stendi ya Mabasi huku jengo la ghorofa ambalo ni sehemu ya mradi wa soko likigeuzwa ofisi za kukatia tiketi.

Hata hivyo hali hiyo haikudumu zaidi ya miezi miwili, ambapo Watu wa mabasi walilalamika kisha kurejea eneo la Mbagala kama ilivyokuwa awali kabla ya kuhamishiwa Kijichi.

Inaelezwa kuwa baadhi ya viongozi hususani ngazi ya Halmashauri ya Manispaa ya Temeke wamekuwa wakitembelea mradi huo, lakini hakuna kinachoendelea soko limebakia wazi bila kuingiza chochote chenye tija kwa Serikali hata kwa wananchi kama ilivyotarajiwa.

Inaelezwa na wakazi kwamba Rais Samia Suluhu Hassan wakati akiwa Makamu wa Rais, alifanya ziara kwenye mradi huo wa soko la Kijichi, ambapo alionesha kushangazwa na mradi huo kuwekwa kwenye eneo hilo, akisimamia hoja kwamba eneo limejitenga na jamii na akashauri daladala zinazoenda Kijichi zifike hadi sokoni ili angalau kuchochea mzunguko wa biashara.

Kulingana na mandhari iliyopo katikati eneo la karibu linalozunguka mradi huo, umezungukwa na makazi hasa ya watu wenye uwezo kiuchumi huku makazi mengi ya eneo hilo yakionekana kwa wingi yakiwa ndani ya fensi.

Baadhi ya Wafanyabiashara ambao awali walikuwa kwenye soko hilo wanadai watu wengi ambao wanazunguka eneo hilo walikuwa hawalitegemei zaidi kupata huduma.

Pia kuwategemea wanunuzi wengine ilikuwa jambo gumu kutokana na mwelekeo lilipo soko hilo, hali ambayo ilikuwa ikipelekea bidhaa zao mara kwa mara kuoza na kuwasababishia hasara kwenye mitaji yao ambayo walikuwa wamewekeza.

Kutokana na hali hiyo ilivyo kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa, hivi mamlaka husika zinafikira nini kuhusu mradi huo, ikizingatiwa pesa zilizotumika kufanikisha uwepo wa mradi huo ni za mkopo ambazo zinatakiwa kurejeshewa.

Hivi mwelekeo wa Mradi huo ni nini? Serikali imeamua kuuacha ufe, kama ni mkopo, fedha za kulipa madeni zinatoka wapi au ni kwenue miradi mingine ambapo walipa kodi wanakatwa fedha zao na kulipia mradi ambao umetelekezwa?
Daah nakumbukaa 😂 🤭 walianza kwa morari kubwaa saana na kuhakikisha magari yotee ya mikoanii yanaishiaa kijichii kule bondeni naa sio mbagalaa terminal tenaa,, ilii wakuzee stendi yao .haikuchukua hata miezi sitaa ,, watu waakadai kulee ni mbali na ni porini,, sanaa
Ushauri wangu Halmashauri iwarudishee tenaaa 🙈 🙊 🙊 🙊.
 
Ndio hasara hizo za watu wa maofisini kulazimisha masoko maeneo ambayo natural factors zinakataa.

Masoko yajengwe maeneo ambayo yanatumika wakati huo
Mbona hawawajibishwi? Hawa ni wahujumu kama wahujumu wengine. 10% zinaharibu sana nchi yetu, na naona kama imekuwa ruksa.
Actions speak louder than words. Kumbe ndio message wanayotupa!!! we dont bother or care?
 
Back
Top Bottom