Sold out ya mchongo imebumbuluka Simba Day

Sold out ya mchongo imebumbuluka Simba Day

Hilo swali anaweza kuuliza mtu ambaye hajawahi kwenda uwanjani.

Kilichotokea hakiwezi kuhusishwa na uongozi wa Club bali lawama zinaelekezwa kwa security team iliyokuwa getini.

Ni jambo ambalo limezoeleka mapolisi kuchukua hongo na kuruhusu watu wapite.

Hata mimi nimewahi kupita bila N-card.

Ilikuwa nimechelewa mechi nafika getini tayari mechi ishaanza.

N-Card yangu ilikuwa na tiketi nipo kwenye foleni natoa N-Card nampa jamaa aipanchi akaipanchi lakini kwa ghafla zikasikika kelele za mashabiki waliopo uwanjani wakiwa wanashangilia.

Kile kitu kilifanya watu waliopo nyuma kwenye foleni ya kupanchi tiketi wakawa wanatoka kwenye foleni wanakuja mbele kutaka awe wa kwanza kupanchi tiketi.

Kila mtu akawa na usongo wa kutaka kuingia ndani baada ya kupagawa na zile kelele

Maafisa wakaamua kusitisha zoezi la kupanchi ili kutuliza watu wakae kwenye mstari wafuate utaratibu. Baada ya watu kutulia mi nikawa nataka sasa nipite nikashangaa jamaa ananiambia lete N-Card.

Nikamjibu "mbona tayari umeipanchi?" wala hakunielewa akaniona mzugaji nataka kufanya uhuni, mchizi ndio kwanza akaniweka pembeni.

Basi namimi sikutaka makelele nikasogea pembeni nikawa nanunua haraka haraka tiketi kupitia simu.

Kwa bahati mbaya napo tiketi ikagoma kununulika kwasababu kwa mujibu wa system ilionekana tayari N-Card ina tiketi.

Nikafika kwa yule jamaa anayepanchi nikajaribu kumuoneshea hiyo meseji hata hakunielewa.

Pembeni kulikuwa kuna mwela mmoja kumbe alikuwa ameliona tukio lote tangu mwanzo. Akaniambia mi nimekuona ulivyompa tiketi na nimemuona alivyopanchi hiyo Card.

Nikasema kama ndio hivyo basi ongea naye, akasema hiyo haitawezekana kwasababu hawaruhusiwi.

Nikajiongeza nikamuambia mi hapa nimebakiwa na mitatu tu (wakati huo kiingilio ni 5,000)

Yule mwela akasema weka hiyo mitatu mfukoni, huku yeye akijidai anawapanga watu kama hakuna mawasiliano ya mimi na yeye.

Nikachukua ile mitatu nikatoa buku ikawa buku mbili nikaitia kwenye mfuko wake afu nikamstua kuwa tayari.

Basi fasta fasta bila hata kukagua nilichokiweka mfukoni akasema twende.

Akamuambia yule jamaa anayepanchi "oya mpitishe huyu jamaa kaishapanchi kitambo" Ndio nikapita.

Huku nyuma jamaa inaonekana baada ya kuingiza mkono mfukoni akakuta buku 2 atakuwa alimaindi.
'Mitatu' ni minini? Yaani kuishi kwangu kote huku Uskuduswazi umenitoa kapa. Halafu tulishakubaliana kuwa misemo mipya ya kiswahili isiwe inaanzia huko kwenu ushuani. Hamkawii kuja na misemo ya pizza nyie.
 
'Mitatu' ni minini? Yaani kuishi kwangu kote huku Uskuduswazi umenitoa kapa. Halafu tulishakubaliana kuwa misemo mipya ya kiswahili isiwe inaanzia huko kwenu ushuani. Hamkawii kuja na misemo ya pizza nyie.
Elfu 3/ buku tatu.
 
SIMPLE SANA.

N-CARD IPO CHINI ya SELIKALI.

Kilochofanyika.

Uwanja unachukua watazamaji
60,000/=

Uwanja inachukua mashabiki
Zingatia Neno mashabiki.
57,000/=

Tiketi zilizokatwa ni Elfu sitini
60,000/=

Watazamaji 3000 waliingiza
WAANDISHI.
MAAFISA.
VIONGOZI WA MPIRA.
Wachezaji wastaafu.
POLISI.
ZIMA MOTO
SCAUT
Hiduma ya kwanza nk nk nk.

Maana yake WATU karibu 3000 hawakuingia.

N-CARD IPO CHINI YA SELIKALI.
WEZI.
Polisi na zimamoto wanakaa kwenye siti???
 
Huwa siwashangai mkiandikaga ujinga kwa Sababu inajulikana huko wenye akili ni wawili tu. Huo ni utafiti wa Manara
 
Wengi walioachwa nje ni ambao wamekuja saa 10 jioni hao wote waliambiwa waondoke uwanja umejaa
 
Simple kama kibegi tu kiliwatesa, kitu ambacho nilikuwa nakidharau sana, strange enough kumbe kimewachoma moyo sana baadhi ya watu.

Sold out nayo imekuwa shida.

Msubiri kipigo Sasa, Mwaka wa shidah huu.

NB. Tunaweza laumu walinzi kupitisha watu zaidi, Kwa mtazamo wangu hili ni tatizo la watanzania wengi, kupenda favor Hata kama hastahili, unakuta wawenzako wamewahi unataka ushawishi Kwa Hela ya kubrashia uwe wa kwanza. Mtu huna tiketi unaenda uwanjani kufanya nini na umesikia sold out, simple tu unataka uchukue nafasi ya mtu mwingine. Tiketi yako ya elfu tatu unataka ukae VIP A, simple tu unataka upole nafasi ya mtu, japo hutumia mtutu unatumia ushawishi wa Fedha.
 
Mbona yanga ilikuwa bure kabisa AKA fungulia mbwa na Bado hamkujaza hata nusu ya uwanja?
Lengo kuu la Yanga lilikuwa kupata fedha za kuhudumia timu sio kujaza watu uwanjani. Mo lengo lake lilikuwa kujaza watu uwanjani sio fedha. Binafsi nimemuelewa kwakuwa sio vema kumuita Rais wa nchi kwenye uwanja mtupu.
 
Na kwenye mechi zingine,hasa za kimataifa,tiketi huwa unazinunua wewe?Pambaneni na ulofa wenu!😂😂🐸🐸🐸🐸🐸
Mechi zenu za kimataifa kiingilio ni 3000 mzunguuko na Kuna wakati ilikuwa bure. Ndio maana mo anadai kupata hasara kila wakati. Kimapato Yanga imeingiza hela nyingi siku Yao ya mwananchi kuliko Simba kwenye Simba Day
 
Simple kama kibegi tu kiliwatesa, kitu ambacho nilikuwa nakidharau sana, strange enough kumbe kimewachoma moyo sana baadhi ya watu.

Sold out nayo imekuwa shida.

Msubiri kipigo Sasa, Mwaka wa shidah huu.

NB. Tunaweza laumu walinzi kupitisha watu zaidi, Kwa mtazamo wangu hili ni tatizo la watanzania wengi, kupenda favor Hata kama hastahili, unakuta wawenzako wamewahi unataka ushawishi Kwa Hela ya kubrashia uwe wa kwanza. Mtu huna tiketi unaenda uwanjani kufanya nini na umesikia sold out, simple tu unataka uchukue nafasi ya mtu mwingine. Tiketi yako ya elfu tatu unataka ukae VIP A, simple tu unataka upole nafasi ya mtu, japo hutumia mtutu unatumia ushawishi wa Fedha.
Dili la sold out limebumbuluka.
 
Yani ilikua sold out mpka ikapitiliza
Simba raha bwana
🐸 🐸 🐸 🐸
 
Hilo swali anaweza kuuliza mtu ambaye hajawahi kwenda uwanjani.

Kilichotokea hakiwezi kuhusishwa na uongozi wa Club bali lawama zinaelekezwa kwa security team iliyokuwa getini.

Ni jambo ambalo limezoeleka mapolisi kuchukua hongo na kuruhusu watu wapite.

Hata mimi nimewahi kupita bila N-card.

Ilikuwa nimechelewa mechi nafika getini tayari mechi ishaanza.

N-Card yangu ilikuwa na tiketi nipo kwenye foleni natoa N-Card nampa jamaa aipanchi akaipanchi lakini kwa ghafla zikasikika kelele za mashabiki waliopo uwanjani wakiwa wanashangilia.

Kile kitu kilifanya watu waliopo nyuma kwenye foleni ya kupanchi tiketi wakawa wanatoka kwenye foleni wanakuja mbele kutaka awe wa kwanza kupanchi tiketi.

Kila mtu akawa na usongo wa kutaka kuingia ndani baada ya kupagawa na zile kelele

Maafisa wakaamua kusitisha zoezi la kupanchi ili kutuliza watu wakae kwenye mstari wafuate utaratibu. Baada ya watu kutulia mi nikawa nataka sasa nipite nikashangaa jamaa ananiambia lete N-Card.

Nikamjibu "mbona tayari umeipanchi?" wala hakunielewa akaniona mzugaji nataka kufanya uhuni, mchizi ndio kwanza akaniweka pembeni.

Basi namimi sikutaka makelele nikasogea pembeni nikawa nanunua haraka haraka tiketi kupitia simu.

Kwa bahati mbaya napo tiketi ikagoma kununulika kwasababu kwa mujibu wa system ilionekana tayari N-Card ina tiketi.

Nikafika kwa yule jamaa anayepanchi nikajaribu kumuoneshea hiyo meseji hata hakunielewa.

Pembeni kulikuwa kuna mwela mmoja kumbe alikuwa ameliona tukio lote tangu mwanzo. Akaniambia mi nimekuona ulivyompa tiketi na nimemuona alivyopanchi hiyo Card.

Nikasema kama ndio hivyo basi ongea naye, akasema hiyo haitawezekana kwasababu hawaruhusiwi.

Nikajiongeza nikamuambia mi hapa nimebakiwa na mitatu tu (wakati huo kiingilio ni 5,000)

Yule mwela akasema weka hiyo mitatu mfukoni, huku yeye akijidai anawapanga watu kama hakuna mawasiliano ya mimi na yeye.

Nikachukua ile mitatu nikatoa buku ikawa buku mbili nikaitia kwenye mfuko wake afu nikamstua kuwa tayari.

Basi fasta fasta bila hata kukagua nilichokiweka mfukoni akasema twende.

Akamuambia yule jamaa anayepanchi "oya mpitishe huyu jamaa kaishapanchi kitambo" Ndio nikapita.

Huku nyuma jamaa inaonekana baada ya kuingiza mkono mfukoni akakuta buku 2 atakuwa alimaindi.
Shida yote hiyo ya nini? Ungeenda zako Kisuma au Liquid ukanywe bia.
 
Hakuna mwenye akili atakae tilia mashaka hili jambo la simba kujaza uwanja tena kwa tiketi halali...ni wenye akili mbovu tuu ndo watakaoona tofauti...Simba iliiuza tiketi mpk ikapitilizaaa...
 
Hakuna mwenye akili atakae tilia mashaka hili jambo la simba kujaza uwanja tena kwa tiketi halali...ni wenye akili mbovu tuu ndo watakaoona tofauti...Simba iliiuza tiketi mpk ikapitilizaaa...
Fanya uchunguzi waliobaki nje na ticket zao wengi wao ni watu wasiokuwa na matawi na waliotoka nje ya DSM. Tiketi za bure ziligawiwa kimya kimya, mo aliinunua shughuli nzima
 
'Mitatu' ni minini? Yaani kuishi kwangu kote huku Uskuduswazi umenitoa kapa. Halafu tulishakubaliana kuwa misemo mipya ya kiswahili isiwe inaanzia huko kwenu ushuani. Hamkawii kuja na misemo ya pizza nyie.
Buku 3
 
Waliojinunulia tiketi kwa hela Yao walibaki nje ya uwanja na wenye tiketi za boss walikuwa ndani ya uwanja. Kuna swali tena hapo?
Mtoto wa kiume unaweza kujikuta unaenda hospital kujifungua kumbe Ni maumivu ya mtani kuujaza uwanja.

Dunia nzima inajua kulikua na Simba day 2023.

Nb:Huko kigamboni Avic Town waliahirisha mechi ya kirafiki na mazoezi ili wangalie Simba day.

Mashaka yangu Ni jinsia yako. Wanaume hatuko hivi ulivyo.
 
Back
Top Bottom