Solidarity fund/uzalendo vs kujenga nchi

Solidarity fund/uzalendo vs kujenga nchi

Lukonge

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2015
Posts
1,469
Reaction score
2,086
Habari Watanzania,

Baada ya kusoma na kusiliza hoja za waziri wa fedha mheshimiwa Dr. Mwigulu Lameck Nchemba, naona kama hajaelewa msingi wa manung'uniko au kelele anazozisikia. Naomba kumweleza yafuatayo, manung'uniko ya wananchi si neno kodi au Tozo.

Manung'uniko ni jinsi haya yote yanavyofanyika. Kuna mtenda na mtendwa. Tuicheze ngoma wote.
Fuatana nami:

1: Tatizo la Watanzania si kuchangia au kutoa Tozo au kulipa kodi kwaajili ya maendel
Tatizo kuu ni kiasi cha tozo na mara ngapi tozo inatolewa kutoka kwa kipato cha mtu mmoja. Hii inakuja kufanya tozo vs kodi kuwa kubwa sana kwa Watanzania.

Inafikia wakati ukiunganisha pesa inayochukuliwa kwenye mshahara ni asilimia 60 ya kipato cha mtu, je ataishije? Hii inaumiza hata kama ni uzalendo(PAYE 25% au zaidi+VAT18+TOZO+PSSSF/NSSF+ NHIF). Hapo usiwe na mkopo benki au loan board.

Kama taifa limepitia stress nyingi, tuzigawane : post Covid19 stress , Uongozi wenye mlengo mmoja, Uchumi/Tozo unaenda kuendeleza kudumaa kwa afya ya akili ya watanzania wengi kama hautatizamwa vyema. Tunaendelea kuongeza idadi ya mtanzuko wa afya ya akili ndani ya Taifa, tuliponye kwa kulionjesha furaha na amani ya moyo kwa kila mmoja wetu. Tusione tu matukio ya ajabu yanatokea, wengi miongoni mwa watu hawako vyema kiakili kwa sababu ya mambo haya.

2: Matumizi ya Serikali baada ya kutoza tozo

Hakuna hatua yoyote iliyoonyeshwa ya wazi kwa serikali kuepuka matumizi ya ANASA. Hii inahusisha kulipana posho kwa kazi za msingi za wahusika tena zikiwa ni posho za kiwango cha juu sana.

Hii inahusisha viongozi wakuu wa serikali, wabunge, mawaziri na viongozi waandamizi wa serikali, kwani wao uzalendo hauwahusu?

Hata kama kuna policy zinasema hivyo, wakati wa dharura naamini tukiamua kufunga mikanda mambo mengine huahilishwa kwa muda. Pesa hizo zingeelekezwa kwenye hiyo miradi na kupunguzia wananchi kiasi na idadi ya TOZO.

Ununuzi wa magari ya kifahari, ziara zisizo na tija, mikutano ya ana kwa ana na semina wakati kuna teknolojia nk. Kusimamia value for money kwa miradi mingi ya serikali na kuondoa 10% nyingi.

Haya yote yanaonyeaha serikali haijawa na nia ya dhati/yanayoelezwa hayatoki moyoni, onyesheni mfano kwa kufunga mikanda ili kuonyesha njia.

3: Ni nani anahusika na uzalendo huu. Tozo vs kodi (solidarity fund).
Kinachoonekana hii inagusa wapangiwa/wasio na sauti/wasio viongozi. Hatujaona viongozi wakuu, mawaziri na wabunge etc. Wakiguswa na hili, tuongee lugha moja.

Wakiziondoa zile exemption zao kwa muda ili tukipite kipindi hiki kigumu wote. Mfano: wote tulipe kodi kwenye ujira wetu, punguza marupurupu kwa kiasi fulani au ondoa, achaneni na magari ya kifahari yanayogharimu pesa nyingi kununua, service za gharama kubwa na mafuta mengi kwa umbali mdogo.

Fanyeni kazi au vikao kwa uzalendo kwa kuondoa baadhi ya posho zenu ili uzalendo utiririke kuanzia juu mpaka chini kwa mwananchi wa kawaida naamini hakutakuwa na malalamiko.

Namalizia kwa kusema tatizo la msingi lipo kwenye: nani anachanga, kiasi gani, mara ngapi, nani anatumia na kwa mwenendo upi.

Hapa shida ni nani wa kumfunga paka kengele. Tuuvae uzalendo wa kweli.
 
Unarikiwe muanzisha mada umeandika mambo mazuri kabisa mwenye akili aelewa na kuongezewa maarifa.
 
Mojawapo ya bandiko bora kabisa kuhusu Tozo na Kodi na uzalendo feki unaohubiriwa na kina Mwigulu.
 
Habari Watanzania,

Baada ya kusoma na kusiliza hoja za waziri wa fedha mheshimiwa Dr. Mwigulu Lameck Nchemba, naona kama hajaelewa msingi wa manung'uniko au kelele anazozisikia. Naomba kumweleza yafuatayo, manung'uniko ya wananchi si neno kodi au Tozo.

Manung'uniko ni jinsi haya yote yanavyofanyika. Kuna mtenda na mtendwa. Tuicheze ngoma wote.
Fuatana nami:

1: Tatizo la Watanzania si kuchangia au kutoa Tozo au kulipa kodi kwaajili ya maendel
Tatizo kuu ni kiasi cha tozo na mara ngapi tozo inatolewa kutoka kwa kipato cha mtu mmoja. Hii inakuja kufanya tozo vs kodi kuwa kubwa sana kwa Watanzania.

Inafikia wakati ukiunganisha pesa inayochukuliwa kwenye mshahara ni asilimia 60 ya kipato cha mtu, je ataishije? Hii inaumiza hata kama ni uzalendo(PAYE 25% au zaidi+VAT18+TOZO+PSSSF/NSSF+ NHIF). Hapo usiwe na mkopo benki au loan board.

2: Matumizi ya Serikali baada ya kutoza tozo

Hakuna hatua yoyote iliyoonyeshwa ya wazi kwa serikali kuepuka matumizi ya ANASA. Hii inahusisha kulipana posho kwa kazi za msingi za wahusika tena zikiwa ni posho za kiwango cha juu sana.

Hii inahusisha viongozi wakuu wa serikali, wabunge, mawaziri na viongozi waandamizi wa serikali, kwani wao uzalendo hauwahusu?

Hata kama kuna policy zinasema hivyo, wakati wa dharura naamini tukiamua kufunga mikanda mambo mengine huahilishwa kwa muda. Pesa hizo zingeelekezwa kwenye hiyo miradi na kupunguzia wananchi kiasi na idadi ya TOZO.
Ununuzi wa magari ya kifahari, ziara zisizo na tija, mikutano ya ana kwa ana na semina wakati kuna teknolojia nk. Kusimamia value for money kwa miradi mingi ya serikali na kuondoa 10% nyingi.

Haya yote yanaonyeaha serikali haijawa na nia ya dhati/yanayoelezwa hayatoki moyoni, onyesheni mfano kwa kufunga mikanda ili kuonyesha njia.

3: Ni nani anahusika na uzalendo huu. Tozo vs kodi (solidarity fund).
Kinachoonekana hii inagusa wapangiwa/wasio na sauti/wasio viongozi. Hatujaona viongozi wakuu, mawaziri na wabunge etc. Wakiguswa na hili, tuongee lugha moja.

Wakiziondoa zile exemption zao kwa muda ili tukipite kipindi hiki kigumu wote. Mfano: wote tulipe kodi kwenye ujira wetu, punguza marupurupu kwa kiasi fulani au ondoa, achaneni na magari ya kifahari yanayogharimu pesa nyingi kununua, service za gharama kubwa na mafuta mengi kwa umbali mdogo.

Fanyeni kazi au vikao kwa uzalendo kwa kuondoa baadhi ya posho zenu ili uzalendo utiririke kuanzia juu mpaka chini kwa mwananchi wa kawaida naamini hakutakuwa na malalamiko.

Namalizia kwa kusema tatizo la msingi lipo kwenye: nani anachanga, kiasi gani, mara ngapi, nani anatumia na kwa mwenendo upi.

Hapa shida ni nani wa kumfunga paka kengele. Tuuvae uzalendo wa kweli.
Hakika!
Na ashukuriwe Mungu kwa ajili ya watanzania wachache ambao bado akili zao ziko sawa sawa kama za mtoa hoja.

Kuna baadhi ya watu hudhani kuwazungumzia maskini ni ushamba na kuwasifia matajiri ni ufahari.

Ukiwa na shibe na bado ukawakumbuka wenye njaa, utapata thawabu kubwa!
Mwenyezi Mungu aliponye taifa letu!
Malalamiko toka kwa wananchi wa kawaida ni mengi mno ni Mungu tu atusaidie!

Watu wakisema, wanaambiwa hawana utaalam wa uchumi. Je, wazee wa zamani walikuwa wasomi wa uchumi? Elimu ya mkoloni imeathiri fikra za walio wengi!
Nadharia za darasani wakati mwingine hazina uhusiano na uhalisia uliopo kwenye jamii!
Mwenyezi Mungu aliponye taifa la Tanzania!
 
Kigali, Rwanda

TOZO NA KODI ZINAPOSHINDWA KUKIDHI BAJETI YA NCHI, SERIKALI IFANYE MKAKATI GANI? GAVANA MSTAAFU AFAFANUA


Gavana mstaafu aelezea njia mbadala ya serikali inavyoweza kukwepa kuchukua mikopo ghali ya kutoka nje ya nchi ili kuziba nakisi ya bajeti pale tozo na kodi kwa ujumla wake zikishindwa kufikia jumla kubwa ya kufadhili bajeti iliyopangwa.

Nchi za South Africa, Kenya zimeweza kutumia hati fungani, mifuko ya pensheni, mifuko ya bima kukopa ndani, Mfuko wa Wana-Diaspiora n.k ili kufidia pale palipopungua badala ya kukopa mikopo kutoka mabenki ya nje ambayo riba ni kubwa na pia masharti yake ni magumu.

Gavana wa benki kuu mstaafu anafafanua kuwa njia hii mbadala ya kukusanya mitaji kutoka vyanzo vya ndani imeanza tangu 2009 na wadau wa maendeleo kama Benki ya Dunia WB, Fuko la Fedha la Dunia IMF, serikali ya Norway, Umoja wa Ulaya EU wameu sapoti mkakati huo ili nchi zinazoendelea vijitathimini kwa kijiangalia kutoka ndani (local) ili kupata mapato zaidi ili kugharamia miradi mikubwa ya maendeleo na miundombinu.

Wadau hao wa maendeleo wa kimataifa walikuja na shauri hilo baada ya mtikisiko wa kifedha duniani na hivyo kupendekeza nchi zinazopewa misaada na mikopo kujitafutia vyanzo vya ndani mbadala kuwa ndiyo nafuu kwa nchi zinazoendelea kujikwamua zenyewe kwa kutafuta vyanzo mbadala na kutanua wigo wa kodi (tax base)

Ukusanyaji kodi ni sawa na mfuko mkubwa wa vikoba (crowd funding), ndivyo ambavyo serikali inatakiwa kutazama makusanyo ya kodi na tozo hivyo katika vikoba ni muhimu serikali kuwa na uwazi pia kubana matumizi ya kifahari na anasa ya kuendesha serikali ili fedha zitumike vizuri ktk vitu wanavyotaka 'wanachama wa vikoba' a.k.a walipa kodi, anafafanua gavana wa benki kuu mstaafu.

Tatizo lingine la nchi za kiafrika ni suala la kutokuwepo sera endelevu bila kusahau mipango ya muda mrefu na hii hutokea pale utawala mpya unapoingia madarakani wanakuja na mipango yao anasisitiza tatizo hili lijadiliwe kwa mapana anatia mkazo gavana wa benki kuu mstaafu.

Uwepo wa sera endelevu huvutia uwekezaji na hata wakulima wadogo wawe wa kahawa n.k wote wanataka uhakika wa sera za serikali ziwe endelevu kwa muda mrefu badala ya kubadilika badilika ktk muda mfupi kupitia mikutano ya ufafanuzi, serikali kukurupuka kuweka tozo mpya au pale utawala unapobadilika n.k

Vitu vyote vikiwekwa wazi na kuwekewa uendelevu basi Afrika zina nafasi ya kupata maendeleo ya haraka tunayoyatamani na pia kuondoka ktk umasikini anamalizia gavana wa benki kuu mstaafu Prof. Njuguna S. Ndung'u .
Source : Uongozi Institute
Njuguna S. Ndung'u is a Kenyan economist, university professor, and economic researcher who served as Governor of the Central Bank of Kenya for two consecutive four-year terms, from March 2007 until March 2015
 
Kigali, Rwanda

TOZO NA KODI ZINAPOSHINDWA KUKIDHI BAJETI YA NCHI, SERIKALI IFANYE MKAKATI GANI? GAVANA MSTAAFU AFAFANUA


Gavana mstaafu aelezea njia mbadala ya serikali inavyoweza kukwepa kuchukua mikopo ghali ya kutoka nje ya nchi ili kuziba nakisi ya bajeti pale tozo na kodi kwa ujumla wake zikishindwa kufikia jumla kubwa ya kufadhili bajeti iliyopangwa.

Nchi za South Africa, Kenya zimeweza kutumia hati fungani, mifuko ya pensheni, mifuko ya bima kukopa ndani, Mfuko wa Wana-Diaspiora n.k ili kufidia pale palipopungua badala ya kukopa mikopo kutoka mabenki ya nje ambayo riba ni kubwa na pia masharti yake ni magumu.

Gavana wa benki kuu mstaafu anafafanua kuwa njia hii mbadala ya kukusanya mitaji kutoka vyanzo vya ndani imeanza tangu 2009 na wadau wa maendeleo kama Benki ya Dunia WB, Fuko la Fedha la Dunia IMF, serikali ya Norway, Umoja wa Ulaya EU wameu sapoti mkakati huo ili nchi zinazoendelea vijitathimini kwa kijiangalia kutoka ndani (local) ili kupata mapato zaidi ili kugharamia miradi mikubwa ya maendeleo na miundombinu.

Wadau hao wa maendeleo wa kimataifa walikuja na shauri hilo baada ya mtikisiko wa kifedha duniani na hivyo kupendekeza nchi zinazopewa misaada na mikopo kujitafutia vyanzo vya ndani mbadala kuwa ndiyo nafuu kwa nchi zinazoendelea kujikwamua zenyewe kwa kutafuta vyanzo mbadala na kutanua wigo wa kodi (tax base)

Ukusanyaji kodi ni sawa na mfuko mkubwa wa vikoba (crowd funding), ndivyo ambavyo serikali inatakiwa kutazama makusanyo ya kodi na tozo hivyo katika vikoba ni muhimu serikali kuwa na uwazi pia kubana matumizi ya kifahari na anasa ya kuendesha serikali ili fedha zitumike vizuri ktk vitu wanavyotaka 'wanachama wa vikoba' a.k.a walipa kodi, anafafanua gavana wa benki kuu mstaafu.

Tatizo lingine la nchi za kiafrika ni suala la kutokuwepo sera endelevu bila kusahau mipango ya muda mrefu na hii hutokea pale utawala mpya unapoingia madarakani wanakuja na mipango yao anasisitiza tatizo hili lijadiliwe kwa mapana anatia mkazo gavana wa benki kuu mstaafu.

Uwepo wa sera endelevu huvutia uwekezaji na hata wakulima wadogo wawe wa kahawa n.k wote wanataka uhakika wa sera za serikali ziwe endelevu kwa muda mrefu badala ya kubadilika badilika ktk muda mfupi kupitia mikutano ya ufafanuzi, serikali kukurupuka kuweka tozo mpya au pale utawala unapobadilika n.k

Vitu vyote vikiwekwa wazi na kuwekewa uendelevu basi Afrika zina nafasi ya kupata maendeleo ya haraka tunayoyatamani na pia kuondoka ktk umasikini anamalizia gavana wa benki kuu mstaafu Prof. Njuguna S. Ndung'u .
Source : Uongozi Institute

Hii ni thesis/hoja kwa Serikali inayolenga kwenda kwenye mafanikio kwa ulinganifu. Kama ukisikiliza ukiwa na mawazo huru/open minded.
 
Kwa kuwa ametutaka tushauri, nashauri kuziita tozo solidarity fund hakusaidii na pengine kuna haribu. Kwanza, kuna ishu ya wakati. Tumetoka kwenye uchaguzi ambao umetugawa kwa kiasi ambacho hakijawahi tokea. Kwa maoni yangu, wananchi wengi wanajiona disenfranchised, hawana uwakilishi. Bunge live lilirudi na wengi hawakujigusa kutazama. Wanaowawakilisha wanajua wanakosa legitimacy. Na wengine lugha na matendo yao yanajionyesha. Kwenye mazingira kama hayo, kuhubiri solidarity ni kujidanganya.
Pili kuna ishu ya mjumbe. Kwenye macho ya wengi, ni mjivuni. Kama si usomi wake, ni utajiri anaosemekana kujilimbikizia. Kwa mtu ambaye nje ya siasa tena kwa kipindi kifupi, hana historia ndefu ya ajira, biashara, wala hajaonyesha personal accomplishment vinavyoweza kujustify ukwasi huo. Lakini pia anawakisha daraja, a political class, ambayo wanaonekana kuwa na sense ya entitlement. Viongozi lazima wawe wao, akitoka hapa anawekwa pale. Na kama viongozi, wanastahili ma vieite. Kwamba mnataka viongozi tutumie pick-up au RAV4, kwenye jamii ambayo sehemu kubwa mlo wa kila siku ni changamoto. Ukiongezea na kauli za "hamieni Burundi", si mtu sahihi kuhubiri solidarity.
 
Hii ni thesis/hoja kwa Serikali inayolenga kwenda kwenye mafanikio kwa ulinganifu. Kama ukisikiliza ukiwa na mawazo huru/open minded.

Serikali sikivu na haya waende kuyatekeleza haraka
 
Hakika!
Na ashukuriwe Mungu kwa ajili ya watanzania wachache ambao bado akili zao ziko sawa sawa kama za mtoa hoja.

Kuna baadhi ya watu hudhani kuwazungumzia maskini ni ushamba na kuwasifia matajiri ni ufahari.

Ukiwa na shibe na bado ukawakumbuka wenye njaa, utapata thawabu kubwa!
Mwenyezi Mungu aliponye taifa letu!
Malalamiko toka kwa wananchi wa kawaida ni mengi mno ni Mungu tu atusaidie!

Watu wakisema, wanaambiwa hawana utaalam wa uchumi. Je, wazee wa zamani walikuwa wasomi wa uchumi? Elimu ya mkoloni imeathiri fikra za walio wengi!
Nadharia za darasani wakati mwingine hazina uhusiano na uhalisia uliopo kwenye jamii!
Mwenyezi Mungu aliponye taifa la Tanzania!
Inauma Sana tena Sana fedha ileile mtumaji yuleye kukatwa kodi Mara mbili halafu wanafiki akina Mwigulu ambao hawafahamu dhiki tunazozipitia wakuja na uzandiki wao eti solidarity fund!
 
Baba Thabo Mbeki rais mstaafu aliongoza jopo kuangalia mianya ya kodi ambazo nchi za kiAfrika wakikusanya basi kutakuwepo na hatua kubwa ya kupiga maendeleo. Uwigo wa Kodi ambazo bado nchi za kiafrica hawakusanyi vizuri ni ktk sekta ya madini ambayo inawekezwa na wawekezaji wakubwa wa bara la Marekani ya Kaskazini, bara ulaya na bara Australi/asia hivyo kutengeneza mianya ya kukwepa kulipa kodi stahiki

Mbeki panel ramps up war against illicit financial flows​

Tax evasion by multinational companies, drug trafficking, smuggling, bribery and embezzlement are the main conduits
Kingsley Ighobor
From Africa Renewal:
April 2016
By:
Kingsley Ighobor
Mr. Thabo Mbeki (middle) led a High-Level Panel on IFF to    the United States. Photo:  Africa Renewal/Paddy Ilos
AR/Paddy Ilos
Mr. Thabo Mbeki (middle) led a High-Level Panel on IFF to the United States. Photo: Africa Renewal/Paddy Ilos
On matters pertaining to Africa’s socioeconomic and political development, former South African president Thabo Mbeki’s voice, tempered by age and experience, continues to be heard.
Seven years since leaving office, Mr. Mbeki doesn’t hide his impatience with Africa’s failure to fulfill its great potential. At the moment Mr. Mbeki is leading a war against illicit financial flows (IFFs) from Africa, as the head of African Union’s 10-member High-Level Panel on IFFs.
Africa is losing at least $50 billion annually to illegal transactions. Some reports suggest the continent may have lost up to $1 trillion in the past 50 years. Global Financial Integrity, a Washington, D.C based nonprofit research and advisory organization heavily involved in the IFF fight, lists the main channels for IFFs as: nefarious commercial activities of multinational companies, drug trafficking and smuggling, and bribery and embezzlement. Some companies also engage in over-invoicing or underpricing trade deals, transfer pricing (avoiding taxes by setting prices in trading between their divisions), offshore banking and the use of tax havens.
In view of the scale of IFFs from Africa, isn’t Mr. Mbeki swimming against the current?
Shared interest
“Illicit financial flows are a challenge to us as Africans, but clearly the solution is global. We couldn’t resolve this thing by just acting on our own as Africans,” Mr. Mbeki began, in an interview with Africa Renewal in New York.
The former president has laid bare his sharp criticisms in a provocative foreword written for a report published in 2015 by his panel. “Africa is a net creditor to the rest of the world,” he maintains, implying that illicit financial outflows from the continent far outstrip official development aid.
In February, Mr. Mbeki led his panel to the United States to promote its report and consequently raise global awareness about IFFs from Africa. A recurring theme in his speeches at the various forums in New York and Washington, D.C. was the urgent need to tackle these IFFs.
As billions are earned and extracted from the continent, more than 400 million Africans live on less than $1.25 a day (the threshold for absolute poverty), and the gross domestic product per person on the continent is just $2,000, which is a fifth of the global average, according to Mr. Mbeki’s panel’s report, titled Track It! Stop It! Get It!
Is the West ready to cooperate with Africa to fight IFFs? “Yes,” Mr. Mbeki responded, because “[cooperation] is of material relevance to the West; not so much that they have suddenly fallen in love with the Africans or the developing world, but because there is a shared interest between the developed and developing
ountries to deal with this matter.”

His panel has twice met with officials of the US government (in 2014 and in 2016), including Vice President Joe Biden. “The US government gave us their own reports regarding what they are doing about tax issues, corruption, and domestic legislation. So we agreed to work together in a structured way to pursue these issues and work is going on.”

In its advocacy for a global alliance to combat IFFs, the success of Mr. Mbeki’s panel will depend on how effectively it can communicate that a victory concerning IFFs is potentially a win-win for everybody. The former president is upbeat about progress made in
enlisting the support of international institutions such as the United Nations, the World Bank, the International Monetary Fund, the Organisation for Economic Co-operation and Development (OECD) and so on.

In addition, “The G7 and the G20 have been discussing how to deal with the illicit financial flows because it is a matter of concern to everybody,” Mr. Mbeki said.

Picking up the gauntlet

While in the United States, Mr. Mbeki and his team held talks with the World Bank and IMF in Washington, D.C. They met with United Nations officials in New York, including Secretary-General Ban Ki-moon and the UN Economic and Social Council (ECOSOC). Earlier they had been in Paris, France, to meet with the OECD, and to the European Parliament in Brussels to engage with the World Customs Organization. The results of their outreach are impressive. The World Bank is currently preparing a programme of action on IFFs, the IMF has expressed its commitment to fighting IFFs, and the UN is ready to help.

“The UN Secretary-General Ban Ki-moon indicated the commitment of the whole UN system, not just ECOSOC, to make sure that at various levels they have a practical focus on this matter,” Mr. Mbeki confirmed.

The panel is soliciting global support, but Africans are also picking up the gauntlet, he said. “We have interacted with African civil society and there is a great enthusiasm to act on IFFs.” He referred to the “Stop the Bleeding” campaign to end IFFs, led by Trust Africa Foundation, as an example of civil society’s commitment to the cause. “It’s not that the African continent is saying to the rest of the world, ‘You do this about illicit financial flows.’ What we are saying is, ‘We as a whole have to act on this.’”

The former president said that Africa’s customs authorities, the police, central banks, the banking system, and financial intelligence units must step up, although he did not deny that a lack of capacity in these institutions will inhibit overall efforts.

“The capacity of these institutions is insufficient. The action agenda that came out of the Financing for Development Conference in Addis Ababa [in July 2015] calls on the rest of the world to assist the African continent to deal with this capacity issue,” he said, adding that tax information exchanged within the global financial system “may become of very little use without the capacity to process it.”

Notwithstanding this insufficiency of capacity, African leaders are determined to confront IFFs, Mr. Mbeki said. The establishment of his panel demonstrates a political will. “We are convinced that there is a keenness on the part of the African governments to act on this matter.”

How to safeguard recovered funds

An undeniable perception of corruption afflicts many governments and institutions in Africa. What would Mr. Mbeki say to critics who argue that monies tracked and recovered could be embezzled once back in Africa? “What drove this whole initiative was how to generate more resources to address development challenges,” he argued. Given that his panel is expected to submit to the AU an annual report on IFFs, in the future such reports could include information
regarding the use of recovered funds.

“Let’s say that the continent is able to recover $25 billion. It would be natural to say that from that $25 billion, two bridges were constructed and 20,000 km of road were built,” he says.

Mr. Mbeki’s panel understands the enormity of the task ahead. Before the interview with Africa Renewal ended, he sought to highlight the relationship between IFFs and natural resources. “Natural resources are important sources of these illicit outflows. Remember that during the war in Liberia, illegal logging was one of the sources of funds to perpetuate the war. So the
elected government hired an international firm to mark every log exported from Liberia and follow such a log until it is offloaded in Rotterdam [in Holland] or somewhere in Europe.

“It’s more challenging with other resources. For example, a country that produces copper may refine it to a certain degree, not completely, and then export it to somewhere else for final processing,” he said. “Such a country cannot know how much copper has been exported because it had not been completely processed locally. So we need a similar tracking system so that the country of origin knows exactly the quantity of exported copper.”

Despite such difficulties, Mr. Mbeki’s bottom-line message is that Africa cannot afford any further depletion of its resources through IFFs.
Source : Mbeki panel ramps up war against illicit financial flows.
 
Ripoti ya Thabo Mbeki yachambuliwa na mapendekezo ya jinsi nchi za kiAfrika zinaweza kukusanya kodi toka kwa wawekezaji wakubwa



Katika mahojiano haya mapendekezo ya kuwezesha TRA iwe na uwezo wa kufuatilia bei za manunuzi ya mfano mitambo ya sekta ya madini ili kufahamu gharama zake halisi na kuweza kuwakadiria tozo / kodi sahihi maana kwa sasa tunategemea kile anachosema / declare mwekezaji ni sahihi wakati hakujafanyika utambuzi wa usahihi wa gharama za uendeshaji na manunuzi anayofanya mwekezaji wa kutoka nje.


Pia serikali ipendekeze kwa jumuiya za kikanda kama EAC Jumuiya ya Afrika ya Mashariki au SADC Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika kwa pamoja kuanzisha kitego cha kuweza kufuatilia makampuni haya makubwa ya madini, gesi n.k ili kwa solidarity ya pamoja inawezekana kuwaita mezani wawekezaji hao huku nchi zikiwa na taarifa sahihi.


Mfano hata Umoja wa Ulaya EU nchi wanachama kwa kukusanya nguvu za taasisi zao wameweza kuibana GOOGLE kampuni kubwa duniani kulipa faini na tozo, kitu ambacho nchi moja moja ingekuwa vigumu kuburuzana na kampuni hilii kubwa la kimataifa.

In this episode of In Focus, we explore the impact of Illicit Financial Flows from Africa on the continent's development as well as measures for combating it with Dr. Vera Songwe, Executive Secretary of United Nations Economic Commission for Africa (UNECA).
Source : Uongozi Institute
 
Kigali, Rwanda

TOZO NA KODI ZINAPOSHINDWA KUKIDHI BAJETI YA NCHI, SERIKALI IFANYE MKAKATI GANI? GAVANA MSTAAFU AFAFANUA


Gavana mstaafu aelezea njia mbadala ya serikali inavyoweza kukwepa kuchukua mikopo ghali ya kutoka nje ya nchi ili kuziba nakisi ya bajeti pale tozo na kodi kwa ujumla wake zikishindwa kufikia jumla kubwa ya kufadhili bajeti iliyopangwa.

Nchi za South Africa, Kenya zimeweza kutumia hati fungani, mifuko ya pensheni, mifuko ya bima kukopa ndani, Mfuko wa Wana-Diaspiora n.k ili kufidia pale palipopungua badala ya kukopa mikopo kutoka mabenki ya nje ambayo riba ni kubwa na pia masharti yake ni magumu.

Gavana wa benki kuu mstaafu anafafanua kuwa njia hii mbadala ya kukusanya mitaji kutoka vyanzo vya ndani imeanza tangu 2009 na wadau wa maendeleo kama Benki ya Dunia WB, Fuko la Fedha la Dunia IMF, serikali ya Norway, Umoja wa Ulaya EU wameu sapoti mkakati huo ili nchi zinazoendelea vijitathimini kwa kijiangalia kutoka ndani (local) ili kupata mapato zaidi ili kugharamia miradi mikubwa ya maendeleo na miundombinu.

Wadau hao wa maendeleo wa kimataifa walikuja na shauri hilo baada ya mtikisiko wa kifedha duniani na hivyo kupendekeza nchi zinazopewa misaada na mikopo kujitafutia vyanzo vya ndani mbadala kuwa ndiyo nafuu kwa nchi zinazoendelea kujikwamua zenyewe kwa kutafuta vyanzo mbadala na kutanua wigo wa kodi (tax base)

Ukusanyaji kodi ni sawa na mfuko mkubwa wa vikoba (crowd funding), ndivyo ambavyo serikali inatakiwa kutazama makusanyo ya kodi na tozo hivyo katika vikoba ni muhimu serikali kuwa na uwazi pia kubana matumizi ya kifahari na anasa ya kuendesha serikali ili fedha zitumike vizuri ktk vitu wanavyotaka 'wanachama wa vikoba' a.k.a walipa kodi, anafafanua gavana wa benki kuu mstaafu.

Tatizo lingine la nchi za kiafrika ni suala la kutokuwepo sera endelevu bila kusahau mipango ya muda mrefu na hii hutokea pale utawala mpya unapoingia madarakani wanakuja na mipango yao anasisitiza tatizo hili lijadiliwe kwa mapana anatia mkazo gavana wa benki kuu mstaafu.

Uwepo wa sera endelevu huvutia uwekezaji na hata wakulima wadogo wawe wa kahawa n.k wote wanataka uhakika wa sera za serikali ziwe endelevu kwa muda mrefu badala ya kubadilika badilika ktk muda mfupi kupitia mikutano ya ufafanuzi, serikali kukurupuka kuweka tozo mpya au pale utawala unapobadilika n.k

Vitu vyote vikiwekwa wazi na kuwekewa uendelevu basi Afrika zina nafasi ya kupata maendeleo ya haraka tunayoyatamani na pia kuondoka ktk umasikini anamalizia gavana wa benki kuu mstaafu Prof. Njuguna S. Ndung'u .
Source : Uongozi Institute



27 September 2022
Nairobi, Kenya

Aliyekuwa gavana wa benki kuu ya Kenya, Prof Njuguna Ndung'u ataeuliwa kama waziri wa fedha ktk serikali ya Rais Ruto


President William Ruto has appointed former Central Bank of Kenya governor Njuguna Ndung'u as the National Treasury Cabinet Secretary.

What should Kenyans expect from Prof. Njunguna Ndung'u,
 
28 September 2022

Rais Ruto aanza kazi kwa kasi kuweka mazingira ya hustlers / wanyonge / mamantilie/ mamamboga yawe bora zaidi mfano riba ndogo, masharti nafuu n.k



Mheshimiwa Rais William Ruto anakumbushia hata nchi hupatiwa huduma za kifedha toka IMF Fuko la Fedha la Kimataifa na World Bank WB Banki ya Dunia kwa kuangalia uwezo wa nchi hivyo kupewa mikopo ya riba ndogo,

Sasa kutokana na hilo taasisi za kifedha Kenya zifuate muundo huo huo wa IMF / World Bank kwa kuwapa huduma za kifedha kwa riba, tozo nafuu wananchi wanyonge wa Kenya.

Kukiwepo mazingira mazuri basi kila mmoja ikiwemo wanyonge kufungua akaunti banki badala ya kuzikimbia kutokana na riba, tozo na huduma zisizoridhisha. Raia kuwa na uwezo wa kukopa na pia kuweka akiba benki ni hatua yenye faida kwa wote yaani mzunguko wa kifedha kufaidisha mabenki, wanyonge walio wengi pia kuwa serikali itakuwa imetimiza azma ya wengi kujiajiri binafsi.

Rais Ruto amesema anafurahi kuongea na taasisi hizo za washika-dau (stakeholders) wakubwa wa kifedha pia kusikia mipango yao ya kuwapa wanyonge nafasi ya kupata huduma hizo za mikopo, tozo, bank overdraft n.k kufuatana na hali halisi ya wateja wadogo badala ya kuwafungia milango na kuwanyima huduma.
 
28 September 2022
Nairobi, Kenya

CBK gavana Dr. Patrick Njoroge hotuba yake mbele ya kongamano shirikishi la taasisi za kifedha KCB, NCBA, Safaricom inayolenga kutambua mahitaji ya wanyonge / hustlers kama vinyozi wa nywele, wenye saluni, mama mboga, wenye biashara ndogo ndogo ambao wana mahitaji maalum ya mikopo


Gavana wa benki kuu ya Kenya Dr. Patrick Njoroge apongeza taasisi za kifedha kukutana ingawa waziri mtarajiwa Prof. Njunguna Ndung'u wa wizara ya fedha na mipango bado hajaingia ofisini akisubiria Bunge la Kenya kumuidhinisha.


Gavana wa benki kuu akiendelea na hotuba akumbushia taasisi hizo za kifedha mambo matatu makubwa muhimu.

Mosi na la muhimu ni kuwaheshimu wateja wawe wadogo, wanyonge au wakubwa kwa kutoa huduma nzuri.


Gavana wa benki kuu akumbushia kuwa Bidhaa za kifedha na huduma ziwe zina unafuu badala ya kukazia kupata faida marudufu hivyo kuwatenga wanyonge .

Tatu taasisi hizi zilenge kuinua maisha ya wanyonge wengi wanaojishughulisha na kazi za kujiajiri
 
Back
Top Bottom