Soma kwa makini unipe ushauri kwa hili

Wafungulie kila mmoja kiduka cha mil 5 inayobaki pambana kiume ujikuze
Asante mkuu, nawaza je wataweza kuendesha vizuri sio mwisho wa siku mambo yakarudi kama mwanzo
 
Sawa mkuu
 
Asante kwa mchango wako kaka
 
Mkuu sifikirii kujenga, nafikilia kununua nyumba ilio kamilika (kwa mwanza napata nyumba ya ela iyo tena yenye umeme)
 
Chukua yarikiboy iko powa waongezee mitaji kidogo napo upate mapendekezo yao usiwajaze mapesa mengi lakini pia lakukaa wote sehemu moja usijaribu kubwa zaidi nikupongeze kwakupotezea mabaya yashangazi japo unaweza kumlaumu lakini pengine mateso yake yakawa ndoyalikupa nguvu yakufika hapo
 
shukrani sana mkuu
 
Wazo namba mbili liko vizuri
Kua na pesa za muendelezo ni vema zaidi ndugu ili kupata uhuru wa kufanya makubwa zaidi
 
Ushauri wangu usije kujaribu kumuweka mama yako na shangazi yako sehemu moja,kumbuka hao ni mtu na wifi yake,narudia kama unataka mama yako afe mapema fanya hivyo. Tena waweke mbali kabisa ikiwezekana wawe wanatembeleana mara chache sana. Labda nikufungue tu yaelekea huna uzoefu sana na haya maisha,hamna watu wabaya kama mashangazi,narudia tena kuwa makini na hao watu
 
asante sana mkuu kwa maneno yako ya busara, nimeyapokea kwa mikono miwili mkuu.
 
Mze wa masihara
 
Iyo hela fanya biashara iongezeke ukijengea nyumba kumbuka nyumba haizalishi iyo ni sawa nakula ada
 
Yusufu alitupwa na kaka zake shimoni akaja kuwa waziri mkuu Misri. Huyo shangazi yako sahau ubaya wake wekeza kwenye kwenye wema wake. Msaidie pale unapoweza, japo kwa kuwa kwa sasa haujawa imara sana kiuchumi, usifikirie kumjengea nyumba... Msaidie hata kulipa kodi inatosha.
Hilo milioni 20 izungushe izae zaidi... Hapo ndo utaweza mnunulia mama nyumba...
 
Sijajua mzazi wako anaishi na wakina nani zaidi, ila ningekua mimi ningemjengea banda la uani(yan vyumba viwili na sebule) then nikamuongezea kamtaji kwenye hiyo biashara yake (hapa lengo linakua asikae tu idle, ila pesa ya matumizi nakua namtumia kadiri ninavyojaaliwa).

Shangazi kwa sasa ningemuongezea tu mtaji au ningeongea na wanae tukashirikiana kumjengea hata chumba na sebule ili aachane na shida za kupanga.

Then mimi naanza from zero kukomaa na jiji.

Nawasilisha.
 
Chukua laki Tano mpe shangazi ako mshauri afungue genge...

Tenga milioni 3 mfungulie mama duka..

Chuku milion tano anzisha biashara yako nyingine weka kumbuka biashara sio rafiki sana kipindi hiki
NOTE: KAMA utajaribu kuwekeza zote 20 mill. Ukikwama hutakua na option...
Kuwa na nidhamu ya fedha kwa kiasi kikubwa
Kumbuka pia nyumba haizalishi na hakuna ujenzi mdogo.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…