Somalia kuwa mwanachama wa 8 kujiunga Jumuiya ya Afrika Mashariki

Somalia kuwa mwanachama wa 8 kujiunga Jumuiya ya Afrika Mashariki

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
1674658087414.png
Sekretarieti ya EAC imetuma Timu yake ya Wataalamu kwenda Somalia kukutana na maafisa wa Serikali ili kufanya uhakiki wa utayari wa maombi ya kujiunga na Jumuiya.

Katibu Mkuu wa EAC, Dkt. Peter Mathuki amesema "Baada ya Timu ya Jumuiya kukutana Somalia, wataandaa ripoti na kuipeleka Baraza la Mawaziri wa EAC wanaotarajia kukutana Februari 23, 2023 na ripoti itapelekwa kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi Februari 25 kwa ajili ya hatua zinazofuata,".

Endapo Somalia itakamilisha taratibu za Kisheria, itakuwa ni Nchi ya 8 kuwa mwanachama wa EAC. Nchi wanachama hadi sasa ni Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Sudani Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

===============

Maombi ya Taifa la Somalia kujiunga na Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC) yameanza kufanyiwa kazi baada ya Sekretarieti ya EAC kutuma timu yake ya wataalamu kwenda nchini humo kukutana na maofisa wa Serikali ya nchi hiyo.

Watalaam hao wa EAC wanatarajiwa kuanza kufanya uhakiki wa utayari wa maombi ya Somalia kujiunga na Jumuiya ya Afrika ya Mashariki.

Kama Somalia ikikamilisha taratibu za kisheria kujiunga na EAC, itakuwa ni nchi ya nane kuwa mwanachama wa EAC nchi nyingine wanachama ni Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Sudani Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 25, 2023 makao makuu ya EAC jijini Arusha, Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo, Dk Peter Mathuki amesema timu hiyo ya wataalamu tayari imefika Somalia na imeanza kazi.

"Baada ya kukutana pamoja wataandaa ripoti na kuipeleka Baraza la Mawaziri wa EAC wanaotarajia kukutana Februari 23 mwaka huu na kisha kupelekwa ripoti hiyo kwenye mkutano wa wakuu wa nchi utakaofanyika Februari 25 kwa ajili ya hatua zinazofuata," amesema.

Somalia kwa muda mrefu imekuwa ikiomba kujiunga na Jumuiya ya Afrika ya Mashariki na katika kikao cha mwisho cha wakuu wa nchi kilichofanyika jijini Arusha, Rais wa nchi hiyo Hassan Sheikh Mohamud alishiriki kama mgeni mwalikwa.

MWANANCHI
 
Nauona mwisho wa Al Shabaab, hii technique inayotumiwa na EAC ni kali sana, Karibu hapa tutaona amani ya kudumu hapo DRC
 
congo amani inaanza kurudi baada ya kuingia EAC,sudani kusini nayo imeanza kurudi baada kuingia EAC,somalia karibu ila al shabibi mtafute kwenda yemen
 
Jumuiya Ya Mchongo Inashindwa Kujisimamia Yenyewe
Congo , Rwanda Kuna Mivutano Ya Siasa Pamoja Na Vita


Viongozi Wapo Kama Pambo Hawana Sauti Hawasikilizwi
Kila Nchi Inamuogopa Mwenzake Hakuna Hatua Nzuri Zaidi Bhalaa Bhalaa
 
Nimewaza tu vyuo vyetu vimelala sana havifanyo advising huko kwa majirani kabisa sasa tutafahamika vipi na kuinua elimu yetu kuwa ya kimataifa.

Tutangaze scholarship kwa watoto wa kike wa somali na rwanda hao nasikiaga wanaakili sana.
Ushauri tu lakini.
 
Jumuiya Ya Mchongo Inashindwa Kujisimamia Yenyewe
Congo , Rwanda Kuna Mivutano Ya Siasa Pamoja Na Vita


Viongozi Wapo Kama Pambo Hawana Sauti Hawasikilizwi
Kila Nchi Inamuogopa Mwenzake Hakuna Hatua Nzuri Zaidi Bhalaa Bhalaa
Kwa mfano wewe ndo rais sasa wa tanzania ungefanyaje kutatua mgogoro baina ya wa watu wajivuni na wagomvi wa rwanda na watu wajeuri wa congo.??
 
Kwa mfano wewe ndo rais sasa wa tanzania ungefanyaje kutatua mgogoro baina ya wa watu wajivuni na wagomvi wa rwanda na watu wajeuri wa congo.??
Hao Wanapewa Fimbo, Na Mikakati Ambayo Iko Bayana
Unataka Kusema Kwa Ukubwa Jumuiya Imeshindwa Kujua Tatizo Na Namna Ya Kulitatua. Viongozi Wapo, Intelligence Ipo


Uamuzi Ndiyo Una Ukakasi, Mwenyekiti Afanye Uamuzi Mgumu Jumuiya Iwe Angalau Na Heshma. Kila Siku Mnaongeza Wanachama Halafu Ya Ndani Ya Jumuiya Yameshindwa Kupatiwa Utatuzi
 
Mhh hao waunde horn of Africa ( Ethiopia, Eritrea, Djibouti, somalia, Somaliland)
 
Wana mademu wana shape nzuri, karibu akina dada wa somali mtupunguzie ghasia
Hawa ni kama wahindi, na waarabu huwa hawataki jamii nyingine kutumia dada zao. Tena huwa nasikia wakiwa wadogo Kuna namna wanawashona ilibtendo lisiwezekanike.
 
Back
Top Bottom