KERO SOUWASA (Ruvuma) toeni neno kuhusu ongezeko la wizi wa Mita za Maji, au kuna michezo inaendelea ili tununue Mita Mpya?

KERO SOUWASA (Ruvuma) toeni neno kuhusu ongezeko la wizi wa Mita za Maji, au kuna michezo inaendelea ili tununue Mita Mpya?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Joined
Sep 23, 2024
Posts
64
Reaction score
43
Huku kwetu katika mitaa ya Manispaa ya Songea kuna wimbi la wizi wa Mita za Maji na kila aliyeibiwa anatakiwa kulipia Sh elfu 45 ili aweze kufungiwa mita nyingine.

Tunajiuliza huu ni mchezo ambao tunachezewa na baadhi ya watu wasiowaaminifu kutoka Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Songea (SOUWASA) au ni nini hasa kinachoendelea?

Ili Mita iweze kutumika inatakiwa kusajiliwa kwenye mamlaka husika, sasa hivi zinazoibwa zinaenda kutumika wapi? Hivi zina matumizi gani ya ziada mbali na idara ya maji? Au pia inabidi tuajiri Walinzi wa Mita?

Kila anayeripoti kuibiwa anapewa control number ili akalipie afungiwe mita nyingine, mnaweza kutufanya tuanze kuamini kuna watu wanacheza michezo michafu ili tulipe tena gharama za Mita.

Maji yenyewe baadhi ya mitaa ni shida tupu kwa wiki yanatoka mara moja wakati mwingine hadi wiki mbili tunakunywa maji ya visima ambayo usalama wake ni mdogo na hawasemi lolote kama kuna mgao au lah!

Wakati huohuo, Mita zinaibwa na Mamalaka inayohusika haijatoa mwongozo au neno kuhusu kinachondelea au kama kuna matumizi zaidi ya Mita zaidi ya hizi tunazozijua ili Wananchi wachukue tahadhari zaidi, wao wanaishia kugawa control namba tukalipe.

Pia soma ~ Afikishwa Mahakamani kwa wizi wa Mita za Maji - Kinondoni
 
Kuna wimbi la wizi wa mita za maji manispaa ya Songea, na kila aliyeibiwa anatakiwa kulipia elfu 45 ili aweze kufungiwa mita nyingine. Mbona kama ni mchezo mnatuchezea SOUWASA mita zimefungwa nje ulinzi ni mdogo na zikiibwa mnatutaka tuwalipe ili iweje? Tuajiri walinzi kwa ajili ya kulinda mita?

Kila anayeripoti kuibiwa mita anapewa control namba ili akalipie afungiwe mita nyingine, ndo utaratibu huo au tunapigwa huku Songea?

Na hizi mita zina matumizi gani ya ziada mbali na idara ya maji?

Maji yenyewe baadhi ya mitaa ni shida mtupu kwa wiki yanatoka mara moja wakati mwingine hadi wiki mbili tunakunywa maji ya visima ambayo usalama wake ni mdogo na hawasemi lolote kama kuna mgao au lah, na mita zinaibwa hawasemi lolote pia zaidi ya kugawa control namba tukalipe.

Pia soma ~ Afikishwa Mahakamani kwa wizi wa Mita za Maji - Kinondoni
Ndo wamejibu Kwa mtindo huu
 

Attachments

  • Screenshot_20250110-181113.png
    Screenshot_20250110-181113.png
    529.7 KB · Views: 6
Back
Top Bottom