Speaker Sitta alikoromea gazeti la RAI

Speaker Sitta alikoromea gazeti la RAI

Huyo spika anataka kutuyeyusha... kwenye gazeti la mtanzania la leo huyo katibu anaonekana wakiwa na mhariri wa rai wanakabidhiana sijui kitu gani. inaonekana kuwa mhariri aliwatembelea rasmi, ina maana walikubali ombi lake au walimpa mwaliko
 
"Bunge mfu" maana yake nini?

Nimelisema hili hapo juu, bunge mfu ni Kiswahili potofu.Hatuna buge mfu, tunaweza kuwa na mbunge mfu (mtu) tuna bunge jifu (kama unakubaliana na hili kimantiki)

Kama vile tusivyoweza kuwa na bunge mpya, bali tunaweza kuwa na bunge jipya.
 
Last edited:
"Huyo spika anataka kutuyeyusha... kwenye gazeti la mtanzania la leo huyo katibu anaonekana wakiwa na mhariri wa rai wanakabidhiana sijui kitu gani. inaonekana kuwa mhariri aliwatembelea rasmi, ina maana walikubali ombi lake au walimpa mwaliko."
_____________________________

Mpita Njia:

Kutokana na maelezo (caption) ya picha Mhariri wa RAi Muhingo Rweyemamu, ambaye pia ni Mhariri Mkuu wa magazeti ya kampuni ya RA anamkabidhi Sitta nakala ya "Business Directory" ya 2009 iliyochapishwa na kampuni hiyo.

Ninavyohisi huyo Muhingo alisafiri hadi Dodoma kwa lengo la kufanya hiyo presentation (iliyofanyika Alhamisi) kwa na lengo la la kumlainisha Sitta asije akaja juu kuhusu RAI -- kitu ambacho alikifanya leo (ijumaa) pamoja na "hongo" hiyo.

Angalia kesho (jumamosi ) jinsi magazeti ya RA hasa Mtanzania yatakavyokuja na stori hiyo, jin si itakavyofinyangwa kuonyesha Spika ndiyo mwenye matatizo.

 
Mimi nilifikiri Sitta na RA walikuwa na alliance mpaka kuitana makanisani kwenye michango, vipi tena, alliance imekufa?
 
Sitta acha kutisha vyombo vya habari!Ni kweli kabisa tena nasisitiza Bunge la TZ sio tu mfu bali ni bunge la kishetani!Iweje wabunge kama Selelii,Mpendazoe,Dr Gama,Shibuda,Chegeni na wengine wengi waliotuhaidi kukwamishs bajeti ya kiimla ya Mkulo yenye vipengele majinuni kama vile Billion 34 za safari za JK kula kuku na Obama USA,Bilion 19 za chai na sambusa kwa mawaziri wakiwa ofisini,kufuta kodi za mafuta ghafi huku wakujua kabisa ndiyo mwisho wa mapato kwa wakulima wa mawese kule Kigoma,Alizeti kule Kilosa na kwingineko!
Lakini wangunge hao hao wakati wa kupitisha bajeti wote walikubali kwa kaluli moja"ndiyo",nawauuliza tena,ina maana hata mbunge kama Ray Mrope wa Mtwara na wewe umekubali bajeti hii inayotenga bilion nyingi kutanua barabara inayopitika ya Segera ili hali jimboni kwako hamna hata barabara moja nzuri?Mbunge Mwakyembe;na wewe umepitisha bajeti hii inayoondoa ushuru wa mawese ili hali wapiga kura wako ktk vijiji vya Ikolo,Mwaya,Itete,Ndandalo,Kandete hata Itungi wakiishi kwa kutegemea biashara ya mawese?sasa wapiga kura wako wataishi vipi?
Naama nasisitiza tena,ni kweli ni bunge lililooza na mfu,na spika sitta aache vitisho
 
Mimi nilifikiri Sitta na RA walikuwa na alliance mpaka kuitana makanisani kwenye michango, vipi tena, alliance imekufa?

Umejuaje Sitta ndio alimuita Rostam kanisani? Ukiombwa chanzo hapa usisingizie blog ya "Chemi Che Mponda."

Blueray, wewe huwa ni mtu unaejadili ma sayansi ya cosmogonic principles, kwa nini hujifunzi kuwa mtu wa kutafuta facts kama hayo ma scientific method unayoyasoma? Hukujifunza kutoka kwa yule cosmic researcher aliyekuwa anatoa ma data lakini marufuku kutoa conclusions?

Acha kutoa toa ma speculations kama kababu kapiga ramli ka Mpanda, eti kwa vile kanisa la Spika Sitta ndio hilo Rostam katoa mchango basi conclusion ni lazima Sitta kamualika.
 
Umejuaje Sitta ndio alimuita Rostam kanisani? Ukiombwa chanzo hapa usisingizie blog ya "Chemi Che Mponda."

Chemi che Mponda is an avid journalist of outstanding personality and achievements you couldn't dare to think in your dreams, let alone attain, how dare you soil her good person with pantomimic slapstick.

Blueray, wewe huwa ni mtu unaejadili ma sayansi ya cosmogonic principles, kwa nini hujifunzi kuwa mtu wa kutafuta facts kama hayo ma scientific method unayoyasoma? Hukujifunza kutoka kwa yule cosmic researcher aliyekuwa anatoa ma data lakini marufuku kutoa conclusions?

Hahaaa, wewe hukujifunza kutoa data kamili ili unapoongea watu wakuelewe, mbona unatoa habari nusu nusu, cosmic researcher gani? Omba msaada usaidiwe basi, kariri jina siku nyingine usionekane zumbukuku.The name is Edwin Hubble of Hubble Telescope and expansion of the Universe fame.Hubble was a wimp in my opinion and he held back scientific progress for tens of years because of his stiff upper lip, much like yours, you pretentious lot have something in common and thats why you can identify with him. He was just a notch from being a pretentious prick of a prima donna like Murray Gell-Man.


Wewe huelewi hata maana ya neno kufikiri, unajua post zangu kuzielewa lazima uelewe kuwa kila neno linapimwa kwa mzani kabla ya kuandikwa.Wapi imeandikwa hapa kwamba lazima kila unachoandika kiwe fact? Kama wewe uko stuck on kila kitu utakachoandika hapa kiwe fact basi una miss out on a lot, hii forum ni ya kujifunza pia, kwa hiyo mimi kama kuna kitu nafikiri -mind the word nafikiri- nakileta hapa kama fikara zangu tu, na wajuvi wanakuja ama kuniunga mkono fikara zangu, ama kunisahihisha.

Sasa weye unayejitia ujuvi ndiye mwenye mzigo wa kusahihisha na kuniambia si hivyo, ni hivi.Mi sijasema ninajua chochote, nimesema nilifikiri. Unajua tofauti ya kuleta kitu kama fact na kuleta kitu kama fikara? Mbona unatoka povu kwa kisa cha kutokuelewa kwako mwenyewe?

Acha kutoa toa ma speculations kama kababu kapiga ramli ka Mpanda, eti kwa vile kanisa la Spika Sitta ndio hilo Rostam katoa mchango basi conclusion ni lazima Sitta kamualika.

First off you have to apologize to all the good people, especially eldery male citizens from Mpanda for your slanderous association of their good district with some shady witchcraft business, apologies are due.

The licentious audacity that empowers you to dispense permission on what can be said and what cannot exposes more about your nature of forceful and misguided austerity than my lack of credibility.

Binadamu hataishi kwa mkate tu, bali hata kwa neno.
Vivyo hivyo progress haiji kwa facts tu, bali pia kwa imagination

Kwa kumalizia nakupa quote ya baba yao hao ma cosmogonist na cosmologist huyu hapa anakuonyesha where you are wrong to confine yourself to facts.

Ukitaka mifact tu utakuwa na mlima wa mi fact lakini utashindwa ku conect the dots, unasubiri mpaka watu wajishurutishe wenyewe kukupa facts on a silver platter.

"Imagination is more important than knowledge. For knowledge is limited to all we now know and understand, while imagination embraces the entire world, and all there ever will be to know and understand."

Albert Einstein

Don't get me started this Friday.
 
Last edited:
Sitta acha kutisha vyombo vya habari!Ni kweli kabisa tena nasisitiza Bunge la TZ sio tu mfu bali ni bunge la kishetani!Iweje wabunge kama Selelii,Mpendazoe,Dr Gama,Shibuda,Chegeni na wengine wengi waliotuhaidi kukwamishs bajeti ya kiimla ya Mkulo yenye vipengele majinuni kama vile Billion 34 za safari za JK kula kuku na Obama USA,Bilion 19 za chai na sambusa kwa mawaziri wakiwa ofisini,kufuta kodi za mafuta ghafi huku wakujua kabisa ndiyo mwisho wa mapato kwa wakulima wa mawese kule Kigoma,Alizeti kule Kilosa na kwingineko!
Lakini wangunge hao hao wakati wa kupitisha bajeti wote walikubali kwa kaluli moja"ndiyo",nawauuliza tena,ina maana hata mbunge kama Ray Mrope wa Mtwara na wewe umekubali bajeti hii inayotenga bilion nyingi kutanua barabara inayopitika ya Segera ili hali jimboni kwako hamna hata barabara moja nzuri?Mbunge Mwakyembe;na wewe umepitisha bajeti hii inayoondoa ushuru wa mawese ili hali wapiga kura wako ktk vijiji vya Ikolo,Mwaya,Itete,Ndandalo,Kandete hata Itungi wakiishi kwa kutegemea biashara ya mawese?sasa wapiga kura wako wataishi vipi?
Naama nasisitiza tena,ni kweli ni bunge lililooza na mfu,na spika sitta aache vitisho

Waliitwa kwenye kamati ya chama wakalainika.😱
 
Interesting story in a wrong place.Laiti ingekuwa RAI ile ya kina Ulimwengu....so far sasa hivi Balile&co wako at the crossroad: kwa upande mmoja wanataka ku-maintain reputation ya RAI lakini at the same time wanapaswa kutetea maslahi ya bwana wao RA.

Sitta nae yuko katika nafasi kama hiyo ya RAI.Upande mmoja anajifanya mmoja wa wapinga ufisadi,mostly kwa kauli tupu while at the same time "yeye ni samaki,na samaki yake ni maji".Huyu ni fisadi vilevile.Na kwa namna anavyochanganya mahesabu yake hovyo,si ajabu mwakani akabaki kuwa historia tu,and I would lose my sleep on that!
 
Interesting story in a wrong place.Laiti ingekuwa RAI ile ya kina Ulimwengu....so far sasa hivi Balile&co wako at the crossroad: kwa upande mmoja wanataka ku-maintain reputation ya RAI lakini at the same time wanapaswa kutetea maslahi ya bwana wao RA.

Sitta nae yuko katika nafasi kama hiyo ya RAI.Upande mmoja anajifanya mmoja wa wapinga ufisadi,mostly kwa kauli tupu while at the same time "yeye ni samaki,na samaki yake ni maji".Huyu ni fisadi vilevile.Na kwa namna anavyochanganya mahesabu yake hovyo,si ajabu mwakani akabaki kuwa historia tu,and I would lose my sleep on that!

...you probably meant otherwise.
 
The problem is that Rai's story wasnt fair because it used very abusive languange in presenting its story. Journalism is always about fairness. But since we know why Rai has been attacking the MPs especially Sita, then they are right to serve their masters.

Sitta is being accused by the RA camp of causing the downfall of Edward Lowassa last year, therefore that camp among other things has vowed to ensure that all MPs who claim to be fighting graft are dealt with effectively.

The biggest tool to do this job is the defunct Rai under the control of reckless Muhingo Rweyemamu-a journalist turned a boot licker-after he was sacked from Mwananchi for cropping Dr. Salim's pictures in 2005.

So I am not suprised because this is one of his noble mission. Go back to Salva's letter to RA posted in Jamii Forums website. Due to ill-fated journalism, Rai's cirvulation has declined dramatically to 9000 copies from 60,000 copies reached in 2002-2005, while Raia Mwema-a newly launched weekly has been growing steadily with an average of 40,000 print order.

Watanzania know the real journalists as well as the boot lickers and they dont need anyone to tell them who is who in the media. Hongera Rai for serving RA interests blindly although finally who carries the blame of misusing the media is Reginald Mengi.

Salva wrote this: What do you expect from unprofessional journalists like Manyerere, Muhingo, Balile etc? Ofcourse they are well educated but are unprofessional due to their misconduct.
 
Wakuu nadhani habari iliyomchefua spika ni hii hapa, hebu tuiangalia kama kweli inachafua au mzee 6 ameghafilika tu



Wasomi wachambua ubinafsi wa wabunge

:: Wakosoa namna wanavyochangia bajeti
:: Wasema wanatazama uchaguzi ujao pekee
:: Profesa Baregu aliita bunge la ‘marehemu’

Na Sarah Mossi

BAADHI ya wasomi wamekosoa aina ya uchangiaji mjadala wa bajeti ya Serikali ya mwaka 2009/2010 unaofanywa na wabunge wakidai uchangiaji huo haulengi kuisaidia serikali katika kuinua uchumi wa kitaifa, badala yake unatazama kuwanufaisha wabunge ‘kisiasa’.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili juzi, wasomi hao walisema, mjadala wa bajeti unaofungwa leo mjini Dodoma haukulenga kutazama maslahi ya kunyanyua uchumi wan chi badala yake wabunge walitumia kila nafasi waliyopata kujinufaisha wao kisiasa kwa kuzungumza lugha tamu zinapendwa kusikika na wapiga kura.

Mmoja wa wasomi hao ambaye ni Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM) Dk Richard Mushi aliliambia Rai kuwa; wabunge wengi hawakutazama jukumu lao la kutoa hoja za kitaifa badala yake wanawaza kuhusu uchaguzi mkuu unaofanyika mwakani.

Mhadhiri huyo alisema; “tungetegemea wabunge wasimame na kuzungumzia masuala kama fedha za Halmashauri ziongezwe, suala la barabara na sio kuzungumzia masuala yao ya majimbo pekee,” anazungumza na kuongeza:

"Kule bungeni kuna watu wachache wazuri sana, lakini sasa hivi wana presha kubwa ya kuchaguliwa mwakani na wanazikumbuka zile ahadi walizotoa katika uchaguzi mkuu uliopita."

Msomi mwingine aliyezungumza na Rai ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Mwesiga Baregu ambaye alisema; sasa hivi wabunge hawawezi kuzungumzia masuala ya kitaifa kwa kuwa wanawaza zaidi majimbo yao.

Kufuatia hali hii, Profesa Baregu alifafanua kuwa, mahudhurio ya wabunge kwa sasa ni hafifu pia ukilinganisha na mabunge mengine yaliyopita na hii inatokana na hali ya wabunge kuwa na mguu mmoja ndani ya bunge na mwingine nje ya bunge.

“Hili si bunge la kujenga taifa. Ni la mkao wa uchaguzi wa mwakani, hata mahudhurio unayaona. Watatoka kwenda kwenye majimbo yao, hili ni bunge marehemu kwani nyoyo na fikra za wabunge zinatazama uchaguzi tu,” anasema Profesa Baregu na kuongeza:

"Sijui kama uwezo wao wa kuzungumzia masuala ya kitaifa kama ni mdogo ama vipi...Lakini ninachoweza kusema kwamba safari hii wanazungumza wengi na hata wale wanaolala hawatalala kwenye bunge hili. Akili zao zimeanza kuota kurudi ama kutorudi.

"Na hili angalau vyombo vya habari mmeliona mapema na mnapaswa kulipigia kelele, labda wanaweza kurudi," anasema Profesa Baregu.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba ambaye ni Mchumi Kitaaluma, aliliambia Rai kuwa wabunge katika bunge hili wameonyesha upeo mdogo wa mambo ya kitaifa.

"Lakini wengine wanaelewa wanachofanya, lakini wao ni wanasiasa wameweka mbele maendeleo ya maeneo yao. Wanataka wasikike kile wanachofanya sasa na tutarajie hilo na hapatakuwa na chochote cha kufanya na wao kama wanasiasa watataka wananchi wawasikie, hili ni jambo la kisiasa," anasema Profesa Lipumba.

habari zaidi hapa

Likini hapa hebu angalieni kidogo: Kwenye habari Profesa Baregu amesema ni Bunge Marehemu.

Lakini Sub Editor/Editor wa Rai kichwa kidogo cha habari yenyewe anaandika: Bunge la Marehemu.

Kipi ni kipi kati ya hivi, na kwa nini Spika asione nia ovu ndani yake, lakini pia huyu Marehemu anayemiliki Bunge ni nani kulingana na kichwa kidogo cha habari yenyewe.

Bunge Marehemu angalau inaweza kuelezeka kuwa ni Bunge lisilo la Uhai.
 
Swali ni moja tu kwa Mh. Sitta:

-- Kama siyo Bunge Mfu, kwanini Budget 2009/10 imepita ilihali kuna kasoro kibao zimeainishwa na kujadiliwa na wabunge wenyewe, haswa kuhusiana na posho za safari na chai??[/QUOTE

Je sitta ni Dictetar kwa kuzuia "freedom of speech"?
 
Kama Bunge linaona limekosewa, lilipaswa kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria na sio kutoa onyo.
 
Hivi wabunge wa CCM wanapokubali kuamrishwa kukaa kama kamati ya chama na kulazimishwa kuchukua msimamo wa pamoja hasa pale serikali inapobanwa maana yake ni nini ?

Hivi wanapotoka nje ya kikao baada ya kukubaliana kutetea hoja sisizo na tija zozote kwa taifa halafu wengine wao kuanza kudai kuwa wanapiga vita ufisadi maana yale ni nini ?

Hivi kwenye hivyo vikao wanachanganyana na hao mafisadi ? Na kama ni hivyo huyo anayeendesha hivi vikao yeye yuko upande gani ama na yeye hujiweka neutral ?

Hivi spika wa bunge baada ya kuhudhuria hivi vikao anaporudi bungeni kuendesha vikao vya bunge akijua fika kuwa maamuzi ya kamati yatapita na yeye anakuwa spika mfu ?

Katika hali kama hii kuna kosa gani kuliita bunge mfu ? Kwa maoni yangu bunge linaendeshwa kimfu mfu na ndio maana na maamuzi mengi ya bunge hili ni maamuzi mfu.
Hapana Spika tuna bunge mfu - huo ndio ukweli ingawa mchungu.
 
Back
Top Bottom