Special thread: Kilimo cha umwagiliaji (Irrigation)

Special thread: Kilimo cha umwagiliaji (Irrigation)

Tatzo la watanzania tunaumizana sana...mtu anataka 1.8-2m kwa drip pipes za heka moja while for io hela ukiagiza kutoka china unapata pipes za heka 5....
+86 150 7569 8509 add hio no then anza kuchat na huyo dada watsap mpe requirements zako atakutengenezea design na kukuuzia drip pipes na kukutumia hadi tz unachotakiwa ni kulipia gharama za bandari,wakala na tra utoe mzigo wako...
+8675533556323 hii no ni kwa wale wanaohitaji solar water pump systems kwa wale ambao hawapo karibu na mito...with solar power pump system & drip irrigation u r one point close kua mkulima wa kisasa...Goodluck guys
Finally, naona dalili za waTanzania kuanza kubadilika na kuona maana ya maendeleo kwa upana wake. Dunia ya leo, kwa asilimia kubwa sana, hakuna mipaka kwenye vitu vingi sana, hasa uzalishaji wa chakula. Lakini kabla ya watu wengi sana kufikia jinsi ya kuzitafuta hizo soko, tuanzie hapo kwenye uzalishaji. Na hizi juhudi za mtu mmoja mmoja kuanza kufunguka na kuwa na moyo wa ku share information za kufanikiwa kwenye hatua za uzalishaji kupitia mbinu za kisasa kwa bei nafuu, ni mfano wa kuigwa.

Tusisahau kwamba changamoto za zahiri na zilizo jificha haikosekani popote pale! Kwa hiyo, pale inapojitokeza/zinapojitokeza, tusianze kuogopa na kurudi nyuma kwa visingizio za kusema/kufikiria kwamba tulikuwa bora tulipo tokea kwani ni ndani ya uelewa wetu au uwezo wetu (in other words, "comfort zone")

Maendelo hayaji kirahisi rahisi tu. Lazima juhudi, fikra na uthubutu haswa ziwepo kwenye hiyo listi ya kufanya, ili kitu kipya kionekane.

Big up! Tanzania mpya tarajiwa na waTanzania wapya watarajiwa pia.
 
SEHEMU YA KWANZA.

MAMBO YA KUZINGATIA UNAPOTAKA KUANZA KILIMO CHA UMWAGILIAJI!

Habari wana jamvi…

Awali ya yote naomba mnisamehe kwa kuto fulfill my promise kushindwa kuweka somo kila wiki kama nilivyo ahidi, okey leo nlitaka kushare nanyi kitu cha kwanza ambacho mtu anatakiwa kumbuka kama anataka anzisha kilimo cha umwagiliaji. Tumeshaona maana ya kilimo cha umwagiliaji katika pati ya utangulizi, sasa leo nlitaka tujadili mambo machache ambayo ni vyema yazingatiwe pale mtu anapotaka kuanzisha kilimo cha umwagiliaji!

1. Maji na upatikanaji wa maji (availability of water)

Maji katika kilimo cha umwagiliaji ni kama mafuta kwenye gari, kwa lugha ingine kilimo cha umwagiliaji hakiwezi fanikiwa kama hakuna maji tena maji bora nay a kutosha (quality and quantity)! Kuna madhara makubwa sana ambayo yanaweza tokea kama ubora wa maji (quality) ukiwa mbovu, kwa mtazamo wangu haya ndiyo mabaya Zaidi ya yote katika kilimo cha umwagiliaji…embu angalia mashamba kama lower moshi na tpc ambayo kwa kiasi kikubwa yameathiriwa na magadi/chumvi chumvi (salinity)!! Japo tunahitaji maji kwa umwagiliaji ila maji haya yasipo angaliwa yanaweza kuwa bomu baya sana kwa kilimo!! Katika part hii pia ni vyema kujua allocation ya chanzo cha maji, je kipo karibu au mbali na shamba husika!!! Je kipo mlimani au mremkoni??

2. Aina ya zao (crop type).

Tukishajua upatikanaji wa maji,sasa ni vyema tukajifunza kwanini ni vyema kujua aina ya zao kabla yaku set sistimu wa umwagiliji. Mfano kuna mazao ambayo ni lazima utumie umwagiliaji wa mifereji au boda, na kuna aina ya mazao ambayo sio lazima mfano mahindi na mboga mboga! Mfano katika drip irrigation aina ya zao itakuwezesha kupata ni mipira (drip lines) ngapi utahitaji katika eneo fulani! Hapa nitapawekea somo lake maana kuna mengi yaku cover.

3. Aina ya udongo (Soil type).

Wote tunajua tunapo mwagilia maji katika mashamba yetu maji yanaenda ardhini, basi kwanini hasa niweke sababu hii kama kigezo cha kucheki unapotaka kumwagilia shamba?? Kuna aina nyingi za udongo ila common ni mfinyanzi, kichanga na tifutifu au loam. Kila udongo una sifa yake katika kutunza maji kwa ajili ya mmea. Utunzaji wa maji wa mfinyanzi/clay ni tofauti na mchanga! Mfano clay inavyonza maji haraka na kutunza maji tofauti na mchanga!

4. Mwonekano wa ardhi na hali ya hewa (topography and climate).

Kuna baadhi ya maeneo kuna milima, miinuko na mabonde. Sehemu kama hizi mara nyingi njia inayofaa kutumia ni njia yeyote ya umwagiliaji inayohitaji presha na hasa kama kuna milima na maji niya kupandisha mlimani. Kama eneo liko tambarare umwagiliaji wa mifereji unaweza tumika tofauti na kwenye miinuko! Umwagiliaji wa mifereji kwenye milima unaweza faa kama mifereji itawekwa across the slope na pia angalizo lichukuliwe kuangalia spidi ya maji ili kuzuia mmomonyoko wa ardhi!

5. Mazingira (environment)

Maji yanahitajika katika kila sekta inayomuhusu mwanadamu, japo maji ni uhai ila maji yanaweza hatari zaidi ya bomu kama hayatatumiwa kwa uangalifu yakinifu. Maji ya umwagiliaji yanaweza kuwa chanzo cha magonjwa hasa kichocho (water borne desease), malaria (water related deseases) na hata kuwa maficho ya wanyama hatari. Magonjwa na mmonyoko wa ardhi unachangiwa sana umwagiliaji wa mifereji na kutumia boda system kama za kwenye kilimo cha mpunga. Maji pia yanaweza kuwa chanzo cha uharibifu wa udongo hasa katika miinuko. Ni vyema kabla hujafikiria kutumia umwagiliaji ujue pia ni vyema ukaangalia mazingira yako na jamii pia.

6. Cost/gharama

Kukiweka cha mwisho haimaanishi kwamba hakina umuhimu, na nnaeza sema nimeweka mwisho ili iwe rahisi kukumbuka! Kuna njia nyingi za umwagiliaji, kuna ambazo ni za gharama ndogo mfano umwagiliaji wa mifereji na kuna ambazo ni za gharama kubwa mfano drip irrigation systems, centre pivot na sprinkler irrigation systems. Mifumo hii kwa namna moja au ingine inahitaji gharama kubwa katika kuianzisha na pia muda mwingine katika kuiendesha. Pia inakua logical kama utatumia mifumo ya gharama kubwa katika kilimo chenye faida kubwa mfano kilimo cha high valuable crops nyanya, kabeji na mengine yenye uhitaji mkubwa sokoni!!

Hizo ni baadhi tu, ziko nyingi! nakaribisha mawazo na challenge hasa washika dau katika sekta hii

Link Things to consider before you start to irrigate

Snipper Red Giant sun Shark moniccca iyengamuliro
Somo zuri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Njoo tulime kilimo chetu.
Drip zipo za level mbalimbali kulingana na level ya mkulima kuanzia Mil 1.8/Acre ambazo hazina dripper ambazo huwa zinasaidia flow ya maji japo zinahitaji shamba ambalo halina miinuko....mpka Mil 10.0/Acre.
Kwa utaalamu zaidi nicheki inbox.
Inbox ya nini mkuu... bora ukasema wote tukaelewa, come on buddy!
 
SWALI:
Mimi nahitaji design kwa na usimamizi katika kilimo cha pilipili mbuzi katika eneo langu dogo lenye upana wa 30m x 25m...

Inaweza kugharimu kiasi gani kwa miundombinu?
MAJIBU:

Cha kwanza je chanzo chako cha maji ni kipi? kisima au mto? au mfereji? je eneo lako liko mkoa/au sehem gani?

Haya ni makadirio ya vitu utakavyohitaji:

1. Drip lines (drip pipes)

Umesema eneo lako lina upana wa 30m kwa urefu wa 35m!, roughly ni kama nusu eka!

Hapa nimechukulia spacing ya mimea ni mstari kwa mstari iwe mita moja na mmea paka mmea iwe 60cm au 50cm!

Mahitaji ya drip lines yatakua 30*35 = 1050m, so utahitaji drip line yenye urefu wa mita 1050 (approx. 1500 au bunda mbili zenye 1000 mita kila moja)! sasa kwa sababu maduka mengi wanauza bunda moja yenye 1000m net, incase ukipata wanapoweza kukupa mita 1500 au kama ukikosa unaweza chukua bunda 2 kwa usalama zaidi!!

2. Tank moja

Kwa eneo lako utakua na mimea sio chini ya 2100 na kila mmea utahitaji sio chini ya lita moja za maji kwa siku so utahitaji tank lenye ujazo sio chini ya lita 3000 na ukipata kubwa zaidi itakua vyema zaidi!

3. Koki atleast 3pcs

Hii ni mwimu maana ndiyo utakua unafungua na kufungia maji na pia utatumia kama pressure requlator, usinunue zile za bombani, nunua zile ambazo ziko wazi pande zote! uwe makini maana hapa size zake zitategemea size za main (inayochukua maji kutoka kwenye tank) na submain pipe inayopeleka maji kwenye drip shambani!

4 .Filter (tumia disc filter)(size ya hii itategemea size ya main pipe yako ambayo itatoka kutoka kwenye tank mpaka kwenye submain, ila by any chance itahitajika 3/4inch au 1 inch). Kuna capacity ya filter hii ni ya mwimu sana ukazingatia! nyingi zinaanzia 100mesh mpaka 200mesh au zaidi!! inategemea na usafi wa maji yako, ila ukipata 150mesh au 200mesh ila ukipata kubwa zaifi ya hapo itakua vizuri zaidi.

NB: Kama maji yako ni machafu unaweza ukahitaji sand filter na disc filter kwa pamoja au DISC FILTER YENYE UWEZO MKUBWA ZAIDI!

5. Main pipe. hii itatoa maji kutoka kwenye tank mpaka kwenye submain yako. unaweza chuku 3/4inch au 1inch. NB chukua nyeusi maana kuna part utaifukia ardhini!
6. Sub mains. hizi zipo special za drip, ila kama ukikosa unaweza chukua hata PVC nyeusi si mbaya. NB: kama ukichukua main pipe ya 1inch basi hii iwe 3/4 inch (three quoter ich)! kama utachukua main ya 3 quota submain iwe ndogo yake ili kumaintain pressure. Kama ukikosa kabisa unaweza chukua zinazofanana haitakua mbaya sana! last time nilinunua zilikua zinachezea 90k mpaka 110k kwa bunda moja la 100mita.

7. T-Joint na Elbow joint! hizi sintaweza sema utahitaji ngapi maana itategemea na configuration ya system yako, again bei zake ni kuanzia 3000 mpaka 5000 maeneo mengi hapa bongo!

6.Driller au puncher/punch. hii utahitaji moja tu, ukiwa na submain za drip utahitaji puch ambayo raisi ila ukitumia PVC ngumu utahitaji driller ambayo kidogo ni ghali, all in all ukifika dukani watakupa mwangaza zaidi!

7.Manati. haya yatatumika kuzuia leakeges inacase zikiwepo!

8.Pipe taper (nimesahau jina kamili). ila ni nyeupe na laini zinatumia kwenye joints za pipe kama ukiunga ili kuepuka leakage!

9. End-cap na Connectors: makadirio zisiwe chini ya 30 maana zote zitategemea configuration ya shamba lako!

NB: Kwa sababu hautumii pump kupeleka maji shambani moja kwa moja, then sizani kama utahitaji complicated pressure regulators, back flow preventers and all those stuffs...

Haya ni makadirio na tutapata actual approximations kama tungefika site na kuona shamba!!
 
Mleta uzi huu ubarikiwe sana, wachangiaji mbarikiwe sana,
Nimeelewa vitu vingi kwenye huu uzi,
Yote ni yote SHUKRANI ZA KIPEKEE KABISA ZIMFIKIE @ cumins
Mkuu unaroho ya kitajiri! Unaroho ya kusaidia, unaroho ya kupenda mwende na wenzako sio kwenda peke yako!
Maana nimesoma humu watu wametoa contact za China unapiga unakutana na Mtu kati nae aweke cha juu,,
Ila @ cumins hajataka mizunguko amemwaga mchele uwanjani mwenye kuhitaji anajichotea tu.hakuna cha mtu kati wala wa pembeni.
BARIKIWA SANA,
Kweli maendeleo tutayaleta wenyewe tukishirikiana.
 
Mimi nahitaji mwongozo/hatua za ujenzi wa gh,vipimo na kiasi cha material na pa kuyapata nataka nijenge mwenyewe niko katavi
 
SWALI:

MAJIBU:

Cha kwanza je chanzo chako cha maji ni kipi? kisima au mto? au mfereji? je eneo lako liko mkoa/au sehem gani?

Haya ni makadirio ya vitu utakavyohitaji:

1. Drip lines (drip pipes)

Umesema eneo lako lina upana wa 30m kwa urefu wa 35m!, roughly ni kama nusu eka!

Hapa nimechukulia spacing ya mimea ni mstari kwa mstari iwe mita moja na mmea paka mmea iwe 60cm au 50cm!

Mahitaji ya drip lines yatakua 30*35 = 1050m, so utahitaji drip line yenye urefu wa mita 1050 (approx. 1500 au bunda mbili zenye 1000 mita kila moja)! sasa kwa sababu maduka mengi wanauza bunda moja yenye 1000m net, incase ukipata wanapoweza kukupa mita 1500 au kama ukikosa unaweza chukua bunda 2 kwa usalama zaidi!!

2. Tank moja

Kwa eneo lako utakua na mimea sio chini ya 2100 na kila mmea utahitaji sio chini ya lita moja za maji kwa siku so utahitaji tank lenye ujazo sio chini ya lita 3000 na ukipata kubwa zaidi itakua vyema zaidi!

3. Koki atleast 3pcs

Hii ni mwimu maana ndiyo utakua unafungua na kufungia maji na pia utatumia kama pressure requlator, usinunue zile za bombani, nunua zile ambazo ziko wazi pande zote! uwe makini maana hapa size zake zitategemea size za main (inayochukua maji kutoka kwenye tank) na submain pipe inayopeleka maji kwenye drip shambani!

4 .Filter (tumia disc filter)(size ya hii itategemea size ya main pipe yako ambayo itatoka kutoka kwenye tank mpaka kwenye submain, ila by any chance itahitajika 3/4inch au 1 inch). Kuna capacity ya filter hii ni ya mwimu sana ukazingatia! nyingi zinaanzia 100mesh mpaka 200mesh au zaidi!! inategemea na usafi wa maji yako, ila ukipata 150mesh au 200mesh ila ukipata kubwa zaifi ya hapo itakua vizuri zaidi.

NB: Kama maji yako ni machafu unaweza ukahitaji sand filter na disc filter kwa pamoja au DISC FILTER YENYE UWEZO MKUBWA ZAIDI!

5. Main pipe. hii itatoa maji kutoka kwenye tank mpaka kwenye submain yako. unaweza chuku 3/4inch au 1inch. NB chukua nyeusi maana kuna part utaifukia ardhini!
6. Sub mains. hizi zipo special za drip, ila kama ukikosa unaweza chukua hata PVC nyeusi si mbaya. NB: kama ukichukua main pipe ya 1inch basi hii iwe 3/4 inch (three quoter ich)! kama utachukua main ya 3 quota submain iwe ndogo yake ili kumaintain pressure. Kama ukikosa kabisa unaweza chukua zinazofanana haitakua mbaya sana! last time nilinunua zilikua zinachezea 90k mpaka 110k kwa bunda moja la 100mita.

7. T-Joint na Elbow joint! hizi sintaweza sema utahitaji ngapi maana itategemea na configuration ya system yako, again bei zake ni kuanzia 3000 mpaka 5000 maeneo mengi hapa bongo!

6.Driller au puncher/punch. hii utahitaji moja tu, ukiwa na submain za drip utahitaji puch ambayo raisi ila ukitumia PVC ngumu utahitaji driller ambayo kidogo ni ghali, all in all ukifika dukani watakupa mwangaza zaidi!

7.Manati. haya yatatumika kuzuia leakeges inacase zikiwepo!

8.Pipe taper (nimesahau jina kamili). ila ni nyeupe na laini zinatumia kwenye joints za pipe kama ukiunga ili kuepuka leakage!

9. End-cap na Connectors: makadirio zisiwe chini ya 30 maana zote zitategemea configuration ya shamba lako!

NB: Kwa sababu hautumii pump kupeleka maji shambani moja kwa moja, then sizani kama utahitaji complicated pressure regulators, back flow preventers and all those stuffs...

Haya ni makadirio na tutapata actual approximations kama tungefika site na kuona shamba!!
Naomba namba ya simu.
 
ekari moja ukitaka kumwagilia kwa drip irrigation unaweza kutumia tank au lazima utumie pump moja kwa moja ili maji yafike mpaka mwisho naomba jibu lako
Habari wana jamvi!

Leo nimeona si vibaya kushare nanyi kidogo nnachojua kuhusu kilimo cha umwagiliaji, na katika uzi huu nitajaribu kuelezea kile nnachojua na pia kupata mawazo kutoka kwa wadau mbali mbali hasa wakulima ambao kwa namna moja au nyingine ndio main actors katika sector ya umwagiliaji!

Kwa miaka kadhaa iliyopita mashirika mbali mbali na serikali vimekua vikiweka mkazo sana katika kilimo cha umwagiliaji, nadhani wote tunakumbuka kilichotokea mwaka huu na mwaka jana ambapo wakulima wengi walipata hasara kwa kulima alafu mvua ikakatika mazao yakiwa katika critical stage, stage ambayo maji ni lazima yawepo kwa ajili ya mimea shambani!

Kwa kifupi katika ulimwengu wa sasa hakuna kilimo cha kibiashara kitafanikiwa bila kuwa na mfumo sahihi na mathubuti kwa ajili ya umwagiliaji!!

Kwa kuanza, leo nitaomba tujifunze/tujikumbushe aina mbali mbali za umwagiliaji au njia ambazo mkulima anaweza kufikisha maji kwenye mmea.

1. Umwagiliaji wa maji kwa kutumia mifereji (furrow/surface irrigation method)

Huu ni umwagiliaji ambao mkulima anatumia mifereji kufikisha maji shambani, umwagiliaji huu unaaminika kutumiwa miaka mingi sana iliyopita, kwa kifupi ndio umwagiliaji mkongongwe (oldest) kushinda njia nyingine za umwagiliaji! Pamoja na faida zake ila umwagiliaji huu unahitaji maji mengi sana na pia unapelekea upotezaji mwingi sana wa maji shambani na uharibifu wa ardhi. Kwa kifupi sio bora ukilnganisha na njia nyingine za umwagiliaji. Katika kundi hili pia kuna border irrigation method

2. Umwagiliaji wa matone (drip irrigation)

Huu ni umwagiliaji wa kisasa kabisa ambao unatumia maji machache na katika njia ambayo ni fanisi. Umwagiliaji huu unaingina katika kundi la “pressurized irrigation” ambapo mara nyingi mtumiaji anahitaji pump kama mechanism ya kulift/kupush/kusukuma maji. Lakini pia umwagiliaji huu unaweza kutumia njia ya “gravitation” ambapo mmwagiliaji anaweka maji kwenye pipa lililo juu (la simtank) na kuruhusu maji yashuke kwa kani mvutano kwenda kwenye drip pipes!

3. Sprinkler irrigation

Hii inatumia njia ambayo maji yanarushwa hewani kama mvua na kushuka kwenye mimea, hii njia pia inaangukia kwenye kundi la “pressurized irrigation” kama ilivyo drip irrigation. Katika njia hii ni lazima mmwagiliaji awe na pump au mechanism yoyote itayotoa pressure!

Ziko njia nyingi za umwagiliaji lakini hizi ndio common kwa maeneo mengi hapa kwetu Tanzania na duniani kwa ujumla!! Katika uzi huu tutajifunza umwagiliaji kwa ujumla, mahitaji ili kuanzisha kilimo cha umwagiliaji, changamoto zake kupitia kwa members wengine humu ambao pia watakua na mawazo au mchango kwenye hii sector na zaidi ya yote tutapitia njia moja baada ya nyingine na kujifunza kwa undani zaidi!

Kama una nia ya kufanya kilimo biashara, basi hakuna jinsi utakwepa kilimo cha umwagiliaji hasa ukizingatia mabadiliko ya hali ya hewa katika miaka ya hivi karibuni

Karibuni sana wanajamvi kwa maswali, mawazo katika hii sector ya kilimo hasa cha umwagiliaji!

SEHEMU YA KWANZA Link: Things to consider before you start to irrigate
SEHEMU YA PILI : Madumuni ya umwagiliaji, post namba 75
 
Back
Top Bottom