Special thread: Kilimo cha umwagiliaji (Irrigation)

Special thread: Kilimo cha umwagiliaji (Irrigation)

ekari moja ukitaka kumwagilia kwa drip irrigation unaweza kutumia tank au lazima utumie pump moja kwa moja ili maji yafike mpaka mwisho naomba jibu lako
Kwanza kutumia pump sio lazima. Sasa naomba tuangalie hizi kesi!

Kwa kutumia pump, faida na changamoto zake...

Kwanza utaweza kufikisha maji shambani kwa urahisi pili hauta ingia gharama za tank incase ukiamua kutumia pump moja kwa moja! (japo unaweza nunua tank incase ukihitaji kuhifadhi maji ili utumie wakati maji yamekatika)

Changamoto kubwa ya pump ni katika gharama yaani lazima ununue mafuta au utumie umeme, pia lazima uwe na pressure regulators ambazo zitahitaji pesa kiasi fulani!

Kwa kutumia tank

Hapa utachohitaji ni tank moja lenye ujazo wa kutosha pia utahitaji pump hata ndogo ya kupeleka maji kwenye tank lako!

Uzuri wa tank ni kwamba japo utahitaji kutumia gharama za kulinunua ila ni rahisi kutumia! na unaweza ukawa na maji kwenye tank hasa wakati maji yamekatika!

Kwa hiyo kama eneo lako ni dogo unaweza tumia tank, pia itafaa zaidi kama eneo lako liko tambarare au liko level maana tank linahitaji gravitation force ili maji yaweze ku flow na kumaintain uniformity!!

USHAURI

Unaweza ukaanza na tank na itapendeza kama ukipata la kubwa itakua vizuri zaidi!! na hata kama usipokua na uwezo wa kununua tank kubwa unaweza ukagawa shamba lako sehemu nne au mbili then ukawa unazimwagilia kwa awamu kulingana na ukubwa wa tank lako!!
 
Kwanza kutumia pump sio lazima. Sasa naomba tuangalie hizi kesi!

Kwa kutumia pump, faida na changamoto zake...

Kwanza utaweza kufikisha maji shambani kwa urahisi pili hauta ingia gharama za tank incase ukiamua kutumia pump moja kwa moja! (japo unaweza nunua tank incase ukihitaji kuhifadhi maji ili utumie wakati maji yamekatika)

Changamoto kubwa ya pump ni katika gharama yaani lazima ununue mafuta au utumie umeme, pia lazima uwe na pressure regulators ambazo zitahitaji pesa kiasi fulani!

Kwa kutumia tank

Hapa utachohitaji ni tank moja lenye ujazo wa kutosha pia utahitaji pump hata ndogo ya kupeleka maji kwenye tank lako!

Uzuri wa tank ni kwamba japo utahitaji kutumia gharama za kulinunua ila ni rahisi kutumia! na unaweza ukawa na maji kwenye tank hasa wakati maji yamekatika!

Kwa hiyo kama eneo lako ni dogo unaweza tumia tank, pia itafaa zaidi kama eneo lako liko tambarare au liko level maana tank linahitaji gravitation force ili maji yaweze ku flow na kumaintain uniformity!!

USHAURI

Unaweza ukaanza na tank na itapendeza kama ukipata la kubwa itakua vizuri zaidi!! na hata kama usipokua na uwezo wa kununua tank kubwa unaweza ukagawa shamba lako sehemu nne au mbili then ukawa unazimwagilia kwa awamu kulingana na ukubwa wa tank lako!!
asante sana mkuu,sasa elevation ya tank kama unataka umwagilie eka 1 kwa drip system si itabidi tank liwe juu ili distribution iwe even
 
Habari wana jamvi!

Leo nimeona si vibaya kushare nanyi kidogo nnachojua kuhusu kilimo cha umwagiliaji, na katika uzi huu nitajaribu kuelezea kile nnachojua na pia kupata mawazo kutoka kwa wadau mbali mbali hasa wakulima ambao kwa namna moja au nyingine ndio main actors katika sector ya umwagiliaji!

Kwa miaka kadhaa iliyopita mashirika mbali mbali na serikali vimekua vikiweka mkazo sana katika kilimo cha umwagiliaji, nadhani wote tunakumbuka kilichotokea mwaka huu na mwaka jana ambapo wakulima wengi walipata hasara kwa kulima alafu mvua ikakatika mazao yakiwa katika critical stage, stage ambayo maji ni lazima yawepo kwa ajili ya mimea shambani!

Kwa kifupi katika ulimwengu wa sasa hakuna kilimo cha kibiashara kitafanikiwa bila kuwa na mfumo sahihi na mathubuti kwa ajili ya umwagiliaji!!

Kwa kuanza, leo nitaomba tujifunze/tujikumbushe aina mbali mbali za umwagiliaji au njia ambazo mkulima anaweza kufikisha maji kwenye mmea.

1. Umwagiliaji wa maji kwa kutumia mifereji (furrow/surface irrigation method)

Huu ni umwagiliaji ambao mkulima anatumia mifereji kufikisha maji shambani, umwagiliaji huu unaaminika kutumiwa miaka mingi sana iliyopita, kwa kifupi ndio umwagiliaji mkongongwe (oldest) kushinda njia nyingine za umwagiliaji! Pamoja na faida zake ila umwagiliaji huu unahitaji maji mengi sana na pia unapelekea upotezaji mwingi sana wa maji shambani na uharibifu wa ardhi. Kwa kifupi sio bora ukilnganisha na njia nyingine za umwagiliaji. Katika kundi hili pia kuna border irrigation method

2. Umwagiliaji wa matone (drip irrigation)

Huu ni umwagiliaji wa kisasa kabisa ambao unatumia maji machache na katika njia ambayo ni fanisi. Umwagiliaji huu unaingina katika kundi la “pressurized irrigation” ambapo mara nyingi mtumiaji anahitaji pump kama mechanism ya kulift/kupush/kusukuma maji. Lakini pia umwagiliaji huu unaweza kutumia njia ya “gravitation” ambapo mmwagiliaji anaweka maji kwenye pipa lililo juu (la simtank) na kuruhusu maji yashuke kwa kani mvutano kwenda kwenye drip pipes!

3. Sprinkler irrigation

Hii inatumia njia ambayo maji yanarushwa hewani kama mvua na kushuka kwenye mimea, hii njia pia inaangukia kwenye kundi la “pressurized irrigation” kama ilivyo drip irrigation. Katika njia hii ni lazima mmwagiliaji awe na pump au mechanism yoyote itayotoa pressure!

Ziko njia nyingi za umwagiliaji lakini hizi ndio common kwa maeneo mengi hapa kwetu Tanzania na duniani kwa ujumla!! Katika uzi huu tutajifunza umwagiliaji kwa ujumla, mahitaji ili kuanzisha kilimo cha umwagiliaji, changamoto zake kupitia kwa members wengine humu ambao pia watakua na mawazo au mchango kwenye hii sector na zaidi ya yote tutapitia njia moja baada ya nyingine na kujifunza kwa undani zaidi!

Kama una nia ya kufanya kilimo biashara, basi hakuna jinsi utakwepa kilimo cha umwagiliaji hasa ukizingatia mabadiliko ya hali ya hewa katika miaka ya hivi karibuni

Karibuni sana wanajamvi kwa maswali, mawazo katika hii sector ya kilimo hasa cha umwagiliaji!

SEHEMU YA KWANZA Link: Things to consider before you start to irrigate
SEHEMU YA PILI : Madumuni ya umwagiliaji, post namba 75
Dogo hongera kwa kutumia elimu vizuri
 
Shukrani kwa ushauri wako mkuu ila naomba kidogo nku-challenge hapo kwenye spacing.. kuna baadhi ya wakulima nimewasikia wanasema spacing inategemeana na hali ya hewa ya kipindi husika, je unaliongeleaje hilo kwa hio recomendatoin yako ya 1m*3m hapo juu?? Jamaa yangu mmoja anadai kipindi cha jua kali ni vizuri kuweka mashimo karibu ili mashina yakutane na kutengeneza kivuli kwa matunda but kipindi cha baridi mashimo yawe mbali sababu mashina hurefuka sana kipindi hicho na yanahitaji kuachana ili yapate mwanga wa jua vizuri kwa ajili ya photosynthesis.
Mrejesho wa spacing katika Tikiti wenye ufanisi UPI.!
Mimi nataka kutumia 0.6*0.6*3.5m double row umwagiliaji wa mfereji itafaa.?
 
Kwa tikiti mkoa wa pwani unaweza kulima.Tikiti linapenda Sandy soil,au Sandy clay( kichanga,au Kichanga mfinyanzi, usiwe mfinyanzi tupu, kwa spacing ya tikiti,tumia mita 1 kutoka shimo hadi shimo ndani ya mstari,na mita 3 kutoka mstari hadi mstari. Mbegu nazopendekeza kutumika ni Sukari F1, Zebra f1 ( Balton Tanzania), Kito F1 ( toka Seedco), na Juliana F1 toka Kiboseed .Kiasi cha Mbegu kwa aina ya Sukari F1 tumia gram 150 kwa eka 1 unapanda mbegu 1 kwa shina, kwa kito F1 tumia gram 500 unapanda mbegu 2 kwa shina. ,mbegu zingine gram 300-500 zinatosha kwa eka 1.

Kwa spacing ya 0.6*0.6*3.5-4 double row kwa umwagiliaji wa mfereji itafaa kwa MKURANGA.?
 
Mungu angekuwa mbinafsi kama sie angetengeneza drip raining system...purposely kwa mimea tuu iliyopandwa
Hakika ingekuwa faida sana kwa mabepari na dunia ingekuwa sehemu ya kutisha sana
 
Back
Top Bottom