LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
hakuna anaeongea ukweli kila mtu anapiga propaganda, takwimu zinazotolewa na ukraine na urusi zote ni za uongo kila mtu kapoteza mara kadhaa zaidi ya hao sema huwez sema ukweli wakati watu wako vitani unashusha morali na kuingiza uoga
Sawa,

Ila ukiangalia mtiririko wa matukio utajua aliyeelemewa na vita na anayepoteza watu wengi zaidi
 
Russia ametumia uweledi mkubwa sana katika hichi wanachokiita operesheni ya kijeshi..ndo maana hata imechukua mda mrefu lengo ni kupunguza madhara makubwa kwa raia..mara nyingi majeshi ya Russia yamekutana na resistance ya wananchi lakini wamekua wakitumia busara sana wao wanaatack tu miundombinu ya jeshi na wanajeshi.
Ingekua ni wamarekani hii operesheni ingeisha ndani ya siku 3 sababu wao wanaua tu hawajali kama walivyofanya iraq
. Huyu raisi wa ukraine asalimu amri kuokoa mauaji ya raia kwan yeye ndo anamotivate raia wasio na millitary knowledge kuvaa combat na Russia akija anapiga tu akijua ni wanajeshi.
 
Huyu raisi wa ukraine asalimu amri kuokoa mauaji ya raia kwan yeye ndo anamotivate raia wasio na millitary knowledge kuvaa combat na Russia akija anapiga tu akijua ni wanajeshi.
Mkuu bora hata angekuwa anawapa hizo combat hao raia, jamaa anachotoa ni bunduki tu na gumboots utadhani wanaenda kwenye kazi za shambani, huku wakipigana na jeans/tracksuit wakijificha kwenye mavazi ya uraia. Wanatumika kama ngao.

 
Combat hazina msaada hapo, mnapigania mjini maadui zenu wamevaa sare na wanajeshi wenu wamevaa sare zao mnazijua. Combat zinazuia risasi ama kitu gani zinaongeza
 
Na kwa akili yako unafikiri huo umoja wa nchi za Ulaya na Usa watakubari Russia aichukue Ukrain unapaswa kufikirisha akili yako vyema mzee wangu
Kwa kauli yako hii ni wazi wewe ndiye hufikirishi akili yako...Russia Hana Nia ya kuchukua Ukraine Bali anataka Yale majimbo mawili yawe huru na tayari ameyatambua....halafu anataka uongozi wa sasa wa Ukraine uondoke madarakani na uwepo uongozi wenye mwelekeo wa kulinda maslahi ya Russia
 
nadhani jamaa kakuelewa sanaa
maana anaiongelea RUSSIA kama anaiongelea CHAD
jamaa nayaheshimu sana mawazo yake na hua namkubali mnooo ila kwa hapa kajifanya MUCH KNOW sana mpaka katupiga CHAII
 
Eti wanaongea kwa lugha ya unyonge kabisa "Demanding Russia" demand maana kuiasa Russia. Siyo "Forcing Russia"

Hapo Putin anacheka tu huku akila bagia home. Yaani hapo ndio mwisho wa uwezo wao. Hakuna kitu kingine cha kufanya zaidi ya hapo.
Ushabiki kwenye level yake, hii ndio bongo land
 
Combat hazina msaada hapo, mnapigania mjini maadui zenu wamevaa sare na wanajeshi wenu wamevaa sare zao mnazijua. Combat zinazuia risasi ama kitu gani zinaongeza
Combat zinasaidia kutambulisha wanajeshi wa pande zote wanaopambana (waweze kuwindana wao kwa wao) na kuwatofautisha na raia ili kuwakinga raia wasidhurike.

Kitendo cha kupigana vita huku baadhi ya watu wakijifananisha na raia wa kawaida (kwa kuvaa nguo za raia) ili kupunguza uwezekano wa wao kushambuliwa (kuchukuliwa kama raia wa kawaida) na kuongeza uwezekano wa wao kushambulia kina hatarisha usalama wa raia wa kawaida ambaye hahusiki hata na mapigano. Raia wa kawaida waweza kudhaniwa nao ni ktk wapiganaji waliojificha kwenye mavazi ya raia na hivyo kushambuliwa/kuuawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…