Watakuja kukubishia kwa kuandika sentensi moja yenye emoji za kuchekacheka waishie hapo. Hawawezi toa facts kupinga unalosema, hawatozungumzia hizo rations, actually zile ni MRE {meals ready to eat}. Rations huwa wanapewa raia kwamba nchi iko vitani hivyo maghala yataishiwa, au fedha za kuagiza nje hamna, au supplies ni ngumu, n.k hivyo raia kula hivi na hivi.
Hawatosema suala la kuishiwa mafuta. Tumesema sana humu logistics ya Russia ilivyo mbovu kwenye vita hii. Yani wanajeshi frontline wanalazimika kutelekeza silaha kisa zimeishiwa mafuta, wakati huo kuna ambush zinawasubiri mbele na air cover hawana.
Mpaka sasa nasubiri mtu anirudishie imani kwamba Russia ana uwezo mkubwa kwa sababu hizi aziorodheshe, hawapo. Watakuja hapa waseme kwani kati ya Ukraine na Russia nani anapigwa kwao? Utadhani Ukraine nalo jeshi la maana humu duniani