LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
Kuna defector mmoja wa Urusi niliwahi msoma nikapuuza alisema Russia haiondoi silaha zake za zamani kwenye matumizi. Kwenye pitapita zangu nikakutana na jamaa ame-paraphrase lile chapisho nikakumbuka.

Russia hadi sasa vifaru vyao vyote ni weak, wamebaki na T-14 Armata ambavyo tunaviona kwenye magwaride tu. Russia ilifanya modernization ya silaha zake ila inashangaza kuona nyingi zinazoonekana hapa ziko in poor condition na bad shape. Kama vifaru hivi unakuta vina explosive reactive armour mbovu mara zimefungwa na nyaya mara zimeninginia, kwingine unaona blocks za armour zimechomoka. Itakuwa either Russian military planners wanapuuza, au fedha zinazotolewa hazitoshi, au kuna rushwa kubwa na ubadhirifu kwenye majeshi. Wana silaha mbovu nyingi tu kwenye uwanja wa mapambano mfano kuona matairi yaliyoisha ni kawaida sana wakati Ukraine ni muda wa snow sasahivi ikiyeyuka ni bora ukutane na mvua.

Silaha nyingi kama vifaru, infrantry fighting vehicles (IFVs) na self propelled howitzer kama Msta na Akatsiya zinatunza ammunition kwenye weak compartment within the vehicle ambapo ikipigwa missile ikapenya kwenye armour ya nje inakuja kufanya ignition ya ammo. Hili tatizo Russia wamelikwepa kwenye T-14 Armata compartment ya crew iko very protected ila Marekani huwa wanaprotect ammo na hutumia mtu mmojawapo kwenye crew kama loader wa ammunition. Ammo iko kwenye compartment nyuma uko imefungwa vizuri yeye anatoa anafeed kwenye gun, hasara ni kufanya kifaru kuwa na crew ya watu wanne ila kwa Russia new designs wanatumia crew ya watatu na loading ni automatic. Hasara ya automatic loading ni kuweka ammo magazine karibu na feed na ikipigwa hapo kinalipuka hapo hata mfupa wa mtu huuoni.

Kupona anti tank missile ni kazi sana. Ile Javelin ya Marekani inaweza penetrate 800mm = mita 0.8 = futi 2.7 za steel. Na inabebwa na mtu mmoja alafu ni 'fire and forget' yani unalenga shabaha unafyatua alafu unaondoka zako na system nzima ina kilo 22 tu na urefu wa mita 1.2
 
Warusi humu hawataki Ukraine apewe sifa.
 
Unapocomment huna haja ya kuanza na blah blah za "sina upande" wakati kati kati ya comment unakuwa umeegemea upande.Wasiokuwa na upande humu comment zao zinaeleweka na wala hawatumii maelezo mengi kujieleza kwanza kuwa hawana upande kama ulivyoanza wewe.Hicho ndicho tunachokukatalia na tunakuambia ukweli wako.Haya endelea sasa na comment zako za kutokuwa na upande 🙂
 
The fact that you man not know about.

Asilimia 99% program zote za Android zimewezekana kwa sababu ya Ukraine.
haaahaaa.
Ukrine walikuharibu kabisa, tatizo ulitoka Tanzania ukaenda moja kwa moja Ukrine.....Ungebahatika kutembelea Matifa makubwa sidhani kama ungesema hivyo.

Degree ya Ukrine ni sawa na form 6 ya Tanzania.
 
Naangalia Al jeezera naona kuna msafara mrefu wa vifaru vya Russia yaani vinalipuliwa sana. Hivi hawa Russia kabla ya kuingia Ukraine haikufanya Planning!!!! Yaani utafikiri walijisemea tu twende Ukraine. Pia ninahisi Kivita na Intelligence ilikuwa kipindi cha USSR tu(KGB) . Russia hii inabebwa tu na Kivuli cha USSR lakini kiuhalisia ni wakawaida tu na walikuwa OVERRATED. Hii vita imewavua nguo.

Hizi silaha zinazolipua vifaru inaweza zikawa zile ATGM alizosema USA na UK wamewapa Ukraine.
 
Nakumbusha tu.
Hata Afghanistan ilikuwa underdog kwa USA.
Hata Vietnam ilikuwa underdog kwa USA

Muhimu Russia ashinde vita halafu mengine baadae.
 
Day 1:Ndani ya siku tatu Ukraine itakuwa chini ya urusi hii ni operation tu sio vita.

Day 3: Warusi wamesitisha vita kupisha mazungumzo.

Day 5: Mazungumzo yameshindikana sasa ndani ya saa 24 Ukraine itakuwa majivu.

Day 7: ukraine wanatumia raia wake kama ngao, wanatakiwa watoke kwanza.

 
Day 8; Kwanza Russia hatumii silaha zake za kisasa katika hii Vita
Day 9; Russia imegundua kuna mamluki wengi kutoka NATO wanaisaidia Ukraine
Day 10; To be continued.........................
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…