Mkuu, na mimi naandika kwa tahadhari sana ninapoizungumzia RUssia, Russia ni taifa kubwa inafahamika vema
Hata hivyo, Russia hawezi kushindana na nguvu za NATO hata iweje, na ijulikane kwamba, NATO bado haijaingia Russia kiwaziwazi mkuu
Itakapofikia rasimi NATO ameingiza miguu yote, Nakuhakikishia kwamba, Putin watamnyonga kama USA walivyofanya kwa Sadamu
Ni nani aliyeamini kwamba Ukraine anaweza kuvuka mipaka yake na kuingia moja kwa moja ndani ya aridhi ya Russia?
Tuupe muda ujitetee, kusema moja kwa moja itakuwa hivi, ni mapema mno mkuu
Bwana Utam am
Yaani nyie pro USA na NATO sijui hua ni utoto au kutokua na ufahamu wa kutosha wa Geopolitics ndio hua unawasumbua!?
Hapa ukweli umeongea kitoto mno,hoja Yako imekosa weledi na urali.
Hivi Kwa akili za kitoto kabisa ,hasa watoto wa darasa la sita au la saba wanapojadili mada hii hawawezi kutoa ulinganifu dhaifu kama wako.
Hivi kweli mmawezaje kulinganisha Nchi dhaifu kijeshi ya Iraq enzi za Sadam Husein dhidi ya nchi za NATO?
Kweli mtu umemaliza hata form four TU katika Discussion hawezi kulinganisha Iraq na NATO.
Nchi ya Iraq kuilinganisha na NATO hakiwezi kutoa majibu sahihi kua NATO ni umoja wenye nguvu za kijeshi Bora kabisa hapa duniani,kwa sababu Iraq ni nchi dhaifu sana ,wala haikua inaunda silaha zake zaidi ya ku modify vikombora vichache kutoka Urusi.
Waliweza kumodify kombora la kizamani la USSR la Scud B na kuliita El Abbas na jingine El Hussein, na vijisilaha vingine vidogo vidogo.
zaidi ya hapo Iraq hawatengenezi silaha.
Iraq hawakua na mfumo wa maana wa ulinzi wa anga ,hawakua na navy ya maana,wala airforce ya maana kuweza kulinganisha na airforce,navy na ground forcces ya NATO.
Hebu fikiria vizuri wewe mtoto, USA ambayo nyinyi mnaamini ndio number one super power inatengeneza Kila aina ya silaha hapa duniani na silaha nyingine ambazo hata nchi nyingine hawana,hebu fikiria nchi kama UK, German na nchi nyingine zote za NATO Kwa wakati huo huku ukiiondoa ufaransa ambayo haikuenda vitani pamoja na NATO,zitazame nchi hizo uwezo wao wa kuzalisha silaha na uwezo wao kijeshi kisha zilinganishe na Iraq ndio mtajua kua nyie ni watu wa aina Gan.
Leo hii NATO kupata ushindi dhidi ya nchi kama Iraq hii ni aibu kubwa mno.
Kumbuka Iraq haikua ikisaidiwa na nchi yoyote hapa duniani.
Hoja ya pili katika makala Yako ni kuilinganisha NATO na Urusi.
Hoja hii moja Kwa moja inaipa ukuu na heshima kubwa mno Urusi.
Na hoja hii ndio inatufungia mjadala wetu juu ya nani zaidi kati ya Urusi na USA.
Nadhani nyie pro NATO wote humu hua mnaipa Urusi heshima kubwa mno kwa kuilinganisha na NATO.
Kwa sababu nyote humu na sehemu nyingine duniani hua mnasema USA ndio superpower Sasa kama super power wenu peke yake hawezi kukabiliana peke yake na Urusi mpaka awe na ushirikiano na nchi nyingine kubwa kijeshi duniani za ulaya ambazo ndio zinaunda umoja wa NATO, basi maana yake huyo superpower wenu haiwezi Urusi akiwa peke yake.
Haya sio maneno yangu Bali ni maneno Yako wewe mwenyewe hapo juu,umesema kua NATO wakiingia vitani kamili dhidi ya Urusi basi Urusi itapigwa na Putin atanyongwa kama Sadam Husein.
Hapa wewe mwenyewe unakili kwa kinywa chako kua hakuna nchi moja ya ulaya Magharibi peke yake inaweza kuishinda Urusi peke yake bila kushirikiana na nchi nyingine zinazounda umoja unaoitwa NATO.
Kwamba hata super power wenu USA hawezi kuishinda Urusi bila nchi nyingine zinazounda NATO.
Hii ndio tafasiri ya hoja zako.
Mimi nilitarajia ungesema kua USA akiingia vitani na Urusi USA itaishinda Urusi na kumnyonga Putin.
Hapa Kwa maana nyingine umemaanisha kua Urusi moja inaweza kushindwa na nchi 32 pekee.
Nchi moja peke yake haiwezi kuipiga Urusi.
Labda nikuambie kitu Cha mwisho hapa unqpoona sio NATO pekee inayokabiliana na Urusi,Bali ni all collective west,sio TU wanapeleka silaha,Bali pia wameiwekea vikwazo ili idhoofike kiuchumi ishindwe kugharamia vita.
je kwa akili Yako wewe unavyoona Urusi hii ya Putin Hadi tarehe hii ya Leo imeshindwa kugharamia vita baada ya kuwekewa vikwazo?
Unajua kua USA akitaka kupitisha ajenda yake hashindwi?
alikataliwa na UN kua Iraq isipigwe kwa sababu Haina WMD lakini kwa ubabe USA wakaenda kumpiga.
Sasa kwa Nini wasimpe Ukraine uanachama wa NATO kibabe kisha wapate sababu ya kuingia vitani kama NATO, ili kumpiga Urusi?
Kumbuka Kuwait na Kosovo hazikua Wanachama wa NATO lkn NATO walizipigania.
Hata Iraq na Libya zilipigwa na NATO.
Lakini pia napenda nikuambie kua,wanajeshi wa NATO wanashiriki vita hii Kwa jina la marcenaries(mamluki) je wamebadilisha Nini.?
Mfano mwingine NATO waliweza kuyaangusha makombora na droni za Iran zilizokua zinaelekea kuipiga Israel,lakini zelensky kawaomba na kuwasihi waweke No fly zone wamekataa alipoona Israel imepata huduma hiyo akawalaumu sana alisema kwa Nini mnatubagua sisi Ukraine mbona Israel mmeipa huduma ya kudungua makombora yaliyopigwa na Iran?
Jibu ni kwamba Urusi sio sawa na Iraq wala sio sawa na Iran.
Ila napenda nikuhakikishie kua Urusi nae ana washirika ambao NATO wakiingia hawatakaa wakitazama,nao wataingia kuisaidia Urusi.
Ni akina nai hao? Mimi sijui ila wapo.
Je vita itakuaje?
Mimi sijui.
Tafakari.