Lee Van free
JF-Expert Member
- Aug 14, 2024
- 1,535
- 5,332
Bado tatizo letu Watanzania la ujuaji liko pale pale.Hiyo north Korea hata usitishike nayo, duniani tunahitaji balance of power lakini kwa north Korea Bado sana, vitisho na mikwara havijawahi kushinda vita, hiyo north Korea haijawahi kushinda vita yoyote, kuwa na nuclear Saba sio sababu ya kuipa point kubwa ya kushinda vita vyake dhidi ya marekani
Yaani kwa ujasiri mkubwa kabisa unaidharau north Korea kua eti ana vitisho na mikwara ambayo haiwezi kushinda vita.
Hivi nyie watanzania hua mnajuaje mambo ya mbele ambaya hata hayajatokea?
Iko hivi north Korea anafanya majaribio ya kurusha makombora ya masafa marefu na Dunia nzima inashuhudia na wataalamu wa maroketi wanapima kujua na kuthibitisha umbali ambao roketi limeenda.
Kibaya zaidi hata wataalamu wa maroketi wa USA wanathibitisha hilo,Sasa hapa wewe Mtanzania mwenzangu unawezaje kudharau uwezo huo wa KK?
Sio TU wataalamu wa USA Bali wataalamu wa Japan,Korea kusini,china,Urusi, Australia na kwingineko wanathibitisha umbali na uwezo wa roketi.
USA siku zote anapenda kuzipiga nchi nyumbani kwao,lakini Korea kaskazini anaiogopa Kwa kua inaweza kupeleka vita USA.
Korea kaskazini Ina satellite zake angani,Ina nyambizi na aina ya silaha zinazoweza kuleta madhara kwa USA, unawezaje kuidharau nchi hii ambayo USA mwenyewe anaiheshimu?
Kusema kweli sisi watanzania ni wajuaji sana.