Spesheli ya watoto tu. Hasi na chanya

Spesheli ya watoto tu. Hasi na chanya

Kwa faida ya wengine....

Ijumaa iliyopita, nilikuwa darasani nikiwafundisha wanafunzi wangu ndipo mwanafunzi mmoja wa kike akainua mkono kuuliza swali. Nilimruhusu na akauliza swali rahisi sana ambalo nilidhani anapaswa kujua jibu lake maana tayari nilikuwa nimezungumzia mada hiyo wiki iliyopita.

"Kaa chini, tafadhari! Na sura yako mbaya! Muone!" ndilo jibu pekee nililompa. Darasa zima liliangua kicheko na alionekana kufedheheka sana.

Niliendelea na somo langu lakini nilihisi kuwa na hatia kwa sababu ya kile nilichokuwa nimesema. Nilimaliza kipindi changu na kuondoka.

Siku ya Jumapili, nilienda Kanisani. Mhubiri alikuwa akiongea juu ya nguvu ya ulimi.

Alizungumza juu ya jinsi unavyoweza kuwavunja moyo, kuwakatisha tamaa na kuwaangusha kabisa wengine kwa kile unachosema. Nilikumbuka kile kilichotokea Ijumaa na nikajiona ni mwenye hatia zaidi. Niliapa kuwa nitaenda kumuomba msamaha Jumatatu nikifika darasani.

Jumatatu alasiri, nilienda darasani lakini sikumuona yule mwanafunzi. Nilimuulizia kwa wenzake lakini hawakuonekana kujua ni nani hasa niliyekuwa nikimzungumzia.

Ndipo nikasema "ninamtafuta mtu niliyemtukana Ijumaa".

"Aah, huyo ni Furaha, mwalimu! Hayuko darasani leo"
walijibu.
Rafiki yake ni nani? Niliuliza.

"Aisha", walijibu. Lakini Aisha pia hayupo darasani.

Ghafla, msichana aliye na Hijab aliingia. "Mwalimu, huyo ni Aisha" wanafunzi wangu walinijulisha.

Yuko wapi rafiki yako? Nikamuuliza.
"Yupi?" Alijibu bila kunitazama usoni.
Furaha! Nilisema.

Yuko chumba cha kuhifadhia maiti. Alijibu.
Jibu hilo lilinishtua! Chumba cha kuhifadhia maiti ????? Kufanya nini hapo ?? Niliuliza.
"Alikufa Ijumaa" Aisha alijibu.
Imekuaje ?????? Niliuliza.

Baadaye niligundua kuwa baada ya kipindi changu Ijumaa, Furaha aligongwa na gari lililokuwa likienda kwa kasi. Alikuwa akivuka barabara bila tahadhari, labda kwa sababu ya kile nilichosema.

"Mazishi yake ni Jumamosi na umealikwa pia, mwalimu" Aisha aliendelea.

Wakati nilikuwa nimesimama nilijaribu kuudhibiti mshtuko niliokuwa nao, Aisha alisema huku akilia, "Mwalimu, umemuua rafiki yangu".

Alikuwa sahihi! Ninapaswa kuwa muuaji! Wasichana wengine darasani walikuwa tayari wanalia! Sikujua niseme nini, ikiwa ni kuomba msamaha kwa rafiki wa Furaha au kwa roho ya Furaha.

Niliwasilisha barua yangu ya kujiuzulu siku iliyofuata ikiwa na maneno haya: Wapendwa Wahadhiri na Walimu, tafadhali acheni kutukana wanafunzi wenu. Wako shuleni ili kujifunza kutoka kwenu. Ingekuwa tayari wanajua, wasingekuwa shuleni!

Tafadhali fikiria kile unachosema kwa watu wengine. Je! Maneno yako yanaleta uhai au kifo kwa wasikilizaji?

ZINGATIO: HADITHI HII NI LAZIMA ISOMWE NA HAIWAHUSU WALIMU TU BALI SISI WOTE TUNAPOKUWA TUNAWASILIANA NA BINADAMU WENZETU: WATEJA, WANAFUNZI, WAZAZI, WENZIO, MARAFIKI NA KADHARIKA

Yatupasa tuwe waangalifu sana juu ya jinsi tunavyosemezana.

Asante.
Kweli kabisa
 
Ma legend kwenye utoto wao
FB_IMG_1657136865105.jpg
 
Mtoto wa kike (5) mkazi wa Soga Kibaha mkoani Pwani, amejeruhiwa vibaya na mfanyakaz wa ndani aliyejuljkana kama Rehema baada ya kumwagiwa mafuta ya moto sehemu mbalimbali za mwili wake na kisha mtuhumiwa huyo kutorokea kusikojulikana.
20220707_045108.jpg
 
Mtoto wa kike (5) mkazi wa Soga Kibaha mkoani Pwani, amejeruhiwa vibaya na mfanyakaz wa ndani aliyejuljkana kama Rehema baada ya kumwagiwa mafuta ya moto sehemu mbalimbali za mwili wake na kisha mtuhumiwa huyo kutorokea kusikojulikana.View attachment 2283027
Wasichana wa kazi wamekuwa mashetani kabisa, mtoto hana hatia si afanye kitu kingine aache kuumiza mtoto? Halafu na yeye ni mama mtarajiwa.
 
Tazama picha za mazishi ya vijana 21 waliofariki katika klabu moja ya usiku huko London Mashariki, Afrika Kusini. Vijana kati ya umri wa miaka 13 na 17 walianza kufa mmoja baada ya mwingine katika baa ya Enyobeni mwezi uliopita. Mamlaka bado zinachunguza vifo vya watu waliofariki.




FB_IMG_1657164037193.jpg
FB_IMG_1657164026783.jpg
FB_IMG_1657164023284.jpg
 
Mama Mmarekani Mweusi akiwafundisha watoto nambari na alfabeti nyumbani kwa sharecropper, Transylvania, Louisiana, Januari 1939 Picha na Russell Lee Picha kwa hisani ya: Kituo cha Schomburg cha Utafiti katika utamaduni wa Weusi, Kitengo cha Picha na Chapa
FB_IMG_1657371230222.jpg
 
Pichani ni Mtoto Daniel Opiyo umri wa miaka 7 mbaye inaelezwa kuwa Ameuwawa na Mama Wa Kambo anaitwa Grace Otieno Katika mtaa wa Engosengiu Kata ya Sinoni Arusha ambaye kwasasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Arusha
Na siku za nyuma Mama huyu wa Kambo alimvunja Mtoto Mkono kama anavyonekana hapo kwenye Picha
R.I.P Mtoto Daniel umekatizwa Ndoto zako.
FB_IMG_1657432706826.jpg
 
Pichani ni Mtoto Daniel Opiyo umri wa miaka 7 mbaye inaelezwa kuwa Ameuwawa na Mama Wa Kambo anaitwa Grace Otieno Katika mtaa wa Engosengiu Kata ya Sinoni Arusha ambaye kwasasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Arusha
Na siku za nyuma Mama huyu wa Kambo alimvunja Mtoto Mkono kama anavyonekana hapo kwenye Picha
R.I.P Mtoto Daniel umekatizwa Ndoto zako.View attachment 2285960
Alipomvunja mkono alichukuliwa hatua gani?
 
Pichani ni Mtoto Daniel Opiyo umri wa miaka 7 mbaye inaelezwa kuwa Ameuwawa na Mama Wa Kambo anaitwa Grace Otieno Katika mtaa wa Engosengiu Kata ya Sinoni Arusha ambaye kwasasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Arusha
Na siku za nyuma Mama huyu wa Kambo alimvunja Mtoto Mkono kama anavyonekana hapo kwenye Picha
R.I.P Mtoto Daniel umekatizwa Ndoto zako.View attachment 2285960
Aisee yan nikioma hiv ata wazo la kuja kuoa siku moja naona ni upuuzi tu bora kulea .wenyewe mtoto wako tu
Inawezekana waliyamaliza kifamilia
Na hili ndio tatzo letu tunapenda kurahusisha mambo kwa kuyamaliza kiramilia kwa kisingizio cha atabadirika
 
Back
Top Bottom