Spika Dkt. Tulia yuko sahihi sana, CHADEMA wajifunze kufanya vitu kwa usahihi na wafanye kiusahihi

Spika Dkt. Tulia yuko sahihi sana, CHADEMA wajifunze kufanya vitu kwa usahihi na wafanye kiusahihi

Mtoa hoja hii ni Mr.Paschal au kuna mtu ametumia status yake?binafsi ni mfuasi sana wa hoja zake but this one it's one of the worst,mbona na wewe mkuu unafikiria kwa kutumia tumbo badala ya kichwa chenye ubongo?all political parties ni vya hiari!,kama hutakiwi jiondoe huwezi lazimisha, katiba ya CDM je inaruhusu kwa member to seek remedy in the courts of law?,courts haziwezi kulazimisha uanachama kwa chama cha hiari, halafu cases zote za kibunge, bunge lilikua linatumia ubabe wake kufanya maamuzi ,refer Mr.Lissu,Mrs . Simba etc etc, na yanayotokea hapa tunajionyesha ni jinsi gani tumo ndani ya shithole country, hii case ni ya kisiasa sio kikatiba na imegubikwa na uroho wa pesa, Mr.Mayala definitely u can do better than this,always Rudina kwenye uandishi wako wenye facts
Katiba ya CHADEMA ipo chini ya Katiba ya Tanzania.

Kwa kuwa hawajaipata haki yao kwenye Katiba ya Chama, wana nafasi ya kuitafuta kupitia Katiba ya Nchi.

Chama siyo mali ya mtu binafsi, ila umma.
 
Wameenda kama Wanachadema.


Hawakutenda haki katika kuwafukuza. Ni mahakama pekee ndio imepewa mamlaka Kikatiba ya kuamua uhalali au uharamu wao.


The moment walipoonesha nia ya kwenda mahakamani tayari walithibitisha kuhisi kutokutendewa haki na nia yao ya kupigania haki yao.

Katika muktadha huu, Spika anawajibika kuwalinda mpaka mahakama itakapoamua vinginevyo.

Punguzeni mahaba.
Mkuu,

Sheria inamtaka speaker kuwaondoa hao wabunge kama barua imetoka kwenye mamlaka halali ya chama.
Maswala ya haki ilitendeka au haikutendeka sio kazi ya speaker alipaswa kuachia mahakama iamue.

Kama walikua wanataka kuendelea kubaki walipaswa wampelekee speaker amri ya mahakama inayomtaka speaker asifanye maamuzi ya kuwaondoa bungeni mpaka mahakama itakapofanya uamuzi.

Je speaker ni chombo cha kutoa haki? Je huoni alichofamya speaker ni kuingilia mamlaka zingine? Je amewaacha kwa kutumia mamlaka ipi kisheria? Maana hata tamko lake hakusema kisheria.

Kwa speaker kutowafukuza ilihali hakuwa na mari ya mahakama speaker amevunja sheria. Pili kusema haki haijatendeka hivyoanaiachia mahakama ni kuiprempty mahakama kwamba haki haijafanyika wakati yeye sio chombo cha haki.

Mari ya mahakama iliyotolewa haina maana yeyote maana tayari speaker alishafanya maamuzi ya kuwalinda.
 
Du Paschal tena,

Swali rahisi sana, wakati Halima na wenzake wameenda bungeni juzi walikua ni wa chama gani mpaka speaker atoe maamuzi ya kuwalinda?

Kwa upande mmoja chama kimewafukuza na kutoa taarifa bungeni. Bunge ilipaswa kufuata sheria ....mbunge lazima atokane na chama.

Upande wa pili waathirika walisema nao wamepata taarifa za kufukuzwa kwao ila wana nia ya kwenda mahakani. Hivyo hawakuwa na amri ya mahakama inayomzuia speaker kuwafukuza.

Je speaker alipata wapi mamlaka au sheria ipi kuwaacha bungeni kabla ya amri ya mahakama?

Je nani mwenye maamuzi ya hovyo?
Refer case ya Lema, wabunge wa CUF etc.

Paschal hujadeclare interest kwamba wewe ni CCM hivyo andiko lako liko biased na sababu zipo wazi na ndio maana utapingwa sana hapa. Pia una ajenda mbaya dhidi ya Chadema kwani kwa siku nne mfululizo umeandika mada moja umebadili jina la title. Hata kama ni spinning kuna njia ya kufanya na sio kwa njia unayotumia ipo wazi mno.

Uteuzi hauji kwa kuandika biased ideas bali kutumia critical thinking plus proffessionalism
sHULE MUHIMU SANA, KUTOA TARIFA MANA YAKE NI NIA YA KUKATA RUFAA. KWANI HATA HILI NALO LINAHITAJI DEGREE KULIFAHAMU?
 
Wanabodi
Leo tena nimepata fursa kuwaletea zile makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa" na issue iliyo mezani ni Sakata la wabunge 19 wa Chadema, Chadema imewatimua ikijua it's done with them, Spika wa Bunge amewakingia kifua, hivyo wanaendelea na ubunge wao kusubiria aumuzi wa mahakama.

Humu JF, tuko wanachama wa aina nyingi, ila pia sisi wanachama wa JF, kuna baadhi yao ambao wana command much respect humu jukwaani, hivyo bandiko hili ni kuwajibu baadhi yao.

Siku zote Chadema imekuwa ikiendesha baadhi ya mambo yake kienyeji enyeji bila kufuata Katiba sheria taratibu na kanuni na haswa timua timua zake, japo Chadema ina katiba, lakini hakuna hata timua timua moja ambayo Chadema wamefuata katiba yake. Timua timua zote ni kinyume cha katiba yake, and always they have been doing that and go away.

This time around, kwenye hili la kina
Halima Mdee, Chadema imekwaa kisiki, tena kisiki cha mpingo, ukijikwaa kwenye kisiki cha mpingo, lazima utaumia wewe, hivyo hili ni Bandiko la kuwahimiza rafiki zangu wana Chadema, Kwa Chadema as chama as well as individually, they should always seek the truth & the truth will set them free. Uamuzi wa Spika wa Bunge, Dr. Tulia Akson kuwakingia kifua, wabunge waliowatimua kikangaroo ni uamuzi sahihi, yaani uamuzi very right, done at the right time and done right.

Ushauri wangu kwa Chadema ni from now, Chadema must learn, the hard way, not only how to do the right things, but also do them right!.


Mkuu Fundi Mchundo , vitu vingine sio vya kuuliza ni kutaka tuu kumuonea Spika.
Uchaguzi unasimamiwa na NEC, Wabunge wote wanapewa barua ya utambulisho ya NEC ndio wanatinga Bungeni. Sii kazi ya Bunge au Spika kuhoji wamepatikanaje, as long as Barua ya utambulisho ya NEC imemfikia then ni authentic letter, Bunge halina sababu yoyote kuhoji utambulisho wa NEC.

Humu JF wengi wana mahaba na Chadema hivyo they are just too blind to see jinsi inavyofanya mambo ya hovyo. Hili jambo ni Chadema wenyewe wameli mishandled toka mwanzo.
Naomba niunganishe na hoja ya Mkuu Nguruvi3 nizijibu kwa pamoja kuwaonyesha makosa ya Chadema ya kijinga kabisa.

Kwa faida ya wengine naomba nianzie mbali.
  1. Hili jambo limeanzishwa na Chadema kususia kutambua matokeo ya uchaguzi mkuu uliopita, ikasema hailitambui Bunge na haitambui Rais
  2. NEC ikatoa nafasi 19 za viti maalum, Chadema wakasema hawateua na hawana time.
  3. Mdee of course, accompanied by Bulaya, wakam consult a very high ranking Kigogo wa Chadema on the benefits of hizo nafasi 19, Kigogo huyo not only gave them a go ahead, but also facilitated them!.
  4. Introduction credentials from Chadema (a bone of contention) introduced the 19 to NEC.
  5. NEC wakawapa barua za utambulisho, authentic bonafide genuine certificates wakaziwasilisha Bungeni, hivyo Kibunge, hawa ni Wabunge halali kabisa!.
  6. Spika/Bunge has nothing to do with the process iliyotumika kumpata mbunge yoyote, as long as ameteuliwa na NEC.
  7. Kukitokea mgogoro wowote wa Uchaguzi, kwa mtu yoyote kupinga ushindi wa mgombea mahakamani, huyo Mbunge ataendelea kuwa mbunge mpaka mahakama itakapotoa hukumu.
  8. Na kukitokea mgogoro wa kichama, mbunge yoyote kufutwa uanachama na chama chake, anapaswa kupoteza ubunge wake automatically ila akiliarifu Bunge kuwa amepinga mahakamani kuvuliwa kwake uanachama, Bunge litamkingia kifua kusubiria aumuzi wa mahakama.
  9. Hivi ndivyo ilivyofanyika kwa Hamad Rashid Mohammed, David Kafulila na Zitto Kabwe. Na baada ya uamuzi wa mahakama, walivuliwa ubunge, Zitto alijivua na kuaga rasmi Bunge.
  10. Hivyo jana asubuhi kupitia Bunge live, Spika alizungumza huku nikimuona kwa macho yangu na kumsikia kwa masikio yangu, alitangulia kupokea taarifa ya kina Mdee kufungua kesi mahakamani kupinga kuvuliwa uanachama, kwa kutaja siku, saa na dakika, kabla ya kupokea taarifa rasmi ya Chadema kuwafuta uanachama. Hivyo Spika Tulia yuko right na Bunge liko right kuwakingia kifua.
  11. Haya sasa ninayoendelea nayo ni yangu. Watu wengi humu wana mahaba niue na Chadema, na siku zote mapenzi yakizidi huleta upofu hivyo hamuoni makosa ya Chadema.
  12. Baada tuu ya Wabunge hao kuapishwa na Chadema kuwakana, sisi washauri wa bure tukawashauri Chadema wafanye a due process wameingiaje Bungeni, barua ya utambulisho toka Chadema imeandikwa na kusainiwa na nani.
  13. Hii due process ingebainisha kuna forgery, forgery ni jinai, walipaswa kuripoti polisi ili uchunguzi wa kijinai ufanyike na hiyo barua yao ya utambulisho, iwe authenticated na ingebainika ni forgery, wala sio Bunge bali ni NEC ndio wangetengua zile barua zao za uteuzi na wangevuliwa ubunge.
  14. Chadema ina katiba yake katiba hiyo imeweka sheria taratibu na kanuni za nidhamu. CC ni mamlaka ya nidhamu ya wabunge, kwanini waliliendesha shauri la wabunge hao Kikangroo bila kufuata taratibu na kanuni zao. Kwanini CC ya Chadema wawatimue wabunge hao bila kufanyika kwanza kwa a due process?!
  15. CC ya Chadema sio mamlaka ya nidhamu ya Mwenyekiti wa Bawacha, Halima Mdee, mwisho wa mamlaka ya CC ya Chadema kwa Mwenyekiti wa Bawacha ni kumsimamisha tuu, lakini mamlaka yake ya nidhamu ni Baraza Kuu, sasa hiyo CC ya Chadema, ilipata wapi mamlaka ya kumtiimua Halima Mdee?.
  16. Kikao cha Baraza Kuu kilipoitishwa kwanini hawakupeleka shauri la Mdee kwenye mamlaka yake sahihi ya rufaa?.
  17. Baraza Kuu linapokaa kama mamlaka ya rufaa kwa wale wabunge 18, ukimuondoa Halima Mdee, kabla ya kupiga kura kuridhia maamuzi ya CC, walipaswa kujiridhisha kuwa taratibu zilifuatwa.
  18. Kile kikao cha CC ya Chadema mimi nimekiita CC ya Chadema imekaa kama a Kangaroo Court, na ule uamuzi wa CC ya Chadema, mimi niliuita ni uamuzi wa Kikangroo, kitendo cha Baraza Kuu kuyabariki maamuzi batili ya Kikangroo bila kufanyika kwanza kwa a due process, kumepelekea Baraza Kuu Chadema kufanya Ukangaroo as well.
  19. A way forward ni Mahakama ambayo ni a proper court itayapindua maamuzi ya Kikangroo ya CC ya Chadema yaliyobarikiwa na Baraza Kuu na kuamuru a due process ifanyike.
  20. Wito wangu kwa wapenzi wa Chadema, seek the truth and the truth will set you free. Iambieni Chadema ukweli, ndio mtaijenga Chadema kuwa ni chama mbadala kuireplace CCM. Kwa haya madudu na maroroso kama haya, Ikulu yetu wangeweza?.
Paskali
Twakumbuka zile siri alizokuwa nazo Mhe Lwakatare. Yaonekana ulikuwa pamoja na Kamanda Sirro. Haya twakusubiri

IGP SIRRO - MBOWE SIO MALAIKA, WALIPANGA KUCHOMA VISIMA Vya MAFUTA, ASEME UKWELI...
IGP SIRRO - "MBOWE SIO MALAIKA, WALIPANGA KUCHOMA VISIMA Vya MA
7.4K views9 months ago
YouTubeGlobal TV Online
Sirro: Chadema wanaona mwenyekiti wao ameonewa, lakini yeye si malaika anajua ukweli
Sirro: Chadema wanaona mwenyekiti wao ameonewa, lakini yeye si malaika anaju
15K views9 months ago
YouTubeBBC News Swahili

1652771462120.png


1652771935841.jpeg


1652771936115.jpeg
 
Siku kibatala atakapo omba nakala na barua toka CHADEMA iliyowateua Hawa covid 19 , na Nusrat fomu yake ya iteuzi aliosaini saa ngapi akiwa mahabusu na alitolewa mahabusu kwa sheria ipi hapo ndipo paskali utakapo tafuta bandiko jipya ....
 
Mhuni hapo ni CHADEMA au Mbowe? CDM kama taasisi wako sahihi kabisa, kama Akina Mdee na Mbowe walifanya makubaliano ya kihuni huko vichochoroni hili ni lao wamalizane wenyewe. Lakini chama kama chama lazima kisimame.

Unadhani ndani ya CDM hawajui kama kulikuwa na makubaliano ya pembeni? Wamekaza kwa makusudi kabisa, hata mwenyekiti ajue hayuko juu ya chama.

You nailed it. Ukitazama mabandiko yote ya Paskali sio utetezi wa kisheria, bali ni makubaliano ya kina Mdee na Mbowe huko vichochoroni. Hayo yako sehemu yoyote. Sisi tunaangalia makubaliano ya wazi na sio hizo porojo za nje ya uwanja. Nimepongeza sana msimamo wa wajumbe wa CDM, hayo makubaliano ya kihuni ya Mbowe na hilo genge lake watajuana.
 
Kuna mambo ambayo leo hii watu hawaelewi mtu X mwenye uthibitisho wote alini PM tena bado yuko CDM kuwa mwenye kujua Suala hili kote ni mbowe ndo maana akawa anahangaika sana akina Mdee wajiondoe wenyewe kabla ya kamati kuu kulinda heshima yake!

Kwa logic tu Kwanini anamtuma mtu mpaka amfuate Nairobi kwamba jitoe, baada ya kugundua kwamba mambo yamekuwa mazito akaona credibility yake inaendelea kushuka!

Mbowe anasema ya Kwenda Nairobi na Gerezani tu , Mbona ya hotelini hajayasema?

Mbona wakati wa msiba wa familia Kwa mbowe Matiko , Mdee Na Bulaya walikaa masaa mawili wakimwambia Heche awape Nafasi kidogo hayasemwi? Kama lilikuwa Suala la afya Kwanini Heche aondolewe!

Mbona hawasemi kwamba Mbowe katembelewa kila Jumapili kule Gerezani ? Na maongezi yamekuwa jinsi ya kuongelea haya?

Emanuel Mugaya ananielewa Kwa nayo andika hapa!

Mdee inaonekana ana heshima sana Kwa mbowe tena sana Mbona mazungumzo ya kabla ya Mkutano mkuu mbowe hayagusii?

Mchezo mchezo wenye uhuni

Wanadanganyana tu na wadanganyane wao kila siku itakuwa Chadema ndo ya Mahakamani wakati Vyama vinginevyo vinajijenga!!!

Chama kina ka Uhuni fulani kwenye maamuzi ni maigizo


Unaweza fika hatua ukaona bora ubaki bila Chama Au ujishkize CCM tu


Britanicca
Oooh najiondoa Jamiiforums...teh teh akili za kisoda
 
Kwanini wasimpige chini?

Chama kimefanyiwa Uhuni mara kadhaa
Wanakaa Kimya

Mwisho wa uhuni umefika na sio kwa shinikizo la ccm, bali kwa ushahidi usioacha shaka. Hata hapo alipo Mbowe sasa anaanza kujua fika watu wamemshtukia. Sitegemei kama atafika 2025 akiwa bado mwenyekiti. Vuta subira utaelewa. Alifanikiwa kuchomoka kwenye ile blunder ya Lowassa, lakini kwa sasa hachomoki.
 
Magufuli hakukosea kukuita njaa maana njaa imekuharibu mpaka umekuwa mtu wa hovyo kabisa, Lissu alipinga kufukuzwa mahakamani kwanini Ndugai hakusubiri uamzi wa mahakama na wabunge wa CUF walipinga mahakamani kwanini Ndugai hakusubiri uamzi wa mahakama? umekuwa mtu wa hovyo sn unapewa rushwa unauza utu wako. Kwahiyo wewe unaijua katiba ya CHADEMA kuliko CHADEMA wenyewe? shame on you
Bunge ni taasisi, mahakama isingeweza kuingilia mamlaka ya bunge, kama ilivyotokea jana kwamba kina Halima wameshaenda mahakamani hivyo spika anasubiri maamuzi ya mahakama

Umeelewa sasa
 
Mafanikio ya Chadema yanaumiza wengi sana ile consistence yao inawapa wakati mgumu mmegawana kila kona kupiga kwa namna tofauti ila kundi halitawanyiki ila ipo siku isiyonajina mtakubali matokeo let's wait and see.
 
Kuna mambo ambayo leo hii watu hawaelewi mtu X mwenye uthibitisho wote alini PM tena bado yuko CDM kuwa mwenye kujua Suala hili kote ni mbowe ndo maana akawa anahangaika sana akina Mdee wajiondoe wenyewe kabla ya kamati kuu kulinda heshima yake!

Kwa logic tu Kwanini anamtuma mtu mpaka amfuate Nairobi kwamba jitoe, baada ya kugundua kwamba mambo yamekuwa mazito akaona credibility yake inaendelea kushuka!

Mbowe anasema ya Kwenda Nairobi na Gerezani tu , Mbona ya hotelini hajayasema?

Mbona wakati wa msiba wa familia Kwa mbowe Matiko , Mdee Na Bulaya walikaa masaa mawili wakimwambia Heche awape Nafasi kidogo hayasemwi? Kama lilikuwa Suala la afya Kwanini Heche aondolewe!

Mbona hawasemi kwamba Mbowe katembelewa kila Jumapili kule Gerezani ? Na maongezi yamekuwa jinsi ya kuongelea haya?

Emanuel Mugaya ananielewa Kwa nayo andika hapa!

Mdee inaonekana ana heshima sana Kwa mbowe tena sana Mbona mazungumzo ya kabla ya Mkutano mkuu mbowe hayagusii?

Mchezo mchezo wenye uhuni

Wanadanganyana tu na wadanganyane wao kila siku itakuwa Chadema ndo ya Mahakamani wakati Vyama vinginevyo vinajijenga!!!

Chama kina ka Uhuni fulani kwenye maamuzi ni maigizo


Unaweza fika hatua ukaona bora ubaki bila Chama Au ujishkize CCM tu


Britanicca
Mwisho wa siku na wewe unabuni tu. Maana ungeweka alichoongea nao ungeeleweka. Mala heche mala msiba mala afya mala gerezani kila jumapili. Lishikwe lipi?
 
Kuna mambo ambayo leo hii watu hawaelewi mtu X mwenye uthibitisho wote alini PM tena bado yuko CDM kuwa mwenye kujua Suala hili kote ni mbowe ndo maana akawa anahangaika sana akina Mdee wajiondoe wenyewe kabla ya kamati kuu kulinda heshima yake!

Kwa logic tu Kwanini anamtuma mtu mpaka amfuate Nairobi kwamba jitoe, baada ya kugundua kwamba mambo yamekuwa mazito akaona credibility yake inaendelea kushuka!

Mbowe anasema ya Kwenda Nairobi na Gerezani tu , Mbona ya hotelini hajayasema?

Mbona wakati wa msiba wa familia Kwa mbowe Matiko , Mdee Na Bulaya walikaa masaa mawili wakimwambia Heche awape Nafasi kidogo hayasemwi? Kama lilikuwa Suala la afya Kwanini Heche aondolewe!

Mbona hawasemi kwamba Mbowe katembelewa kila Jumapili kule Gerezani ? Na maongezi yamekuwa jinsi ya kuongelea haya?

Emanuel Mugaya ananielewa Kwa nayo andika hapa!

Mdee inaonekana ana heshima sana Kwa mbowe tena sana Mbona mazungumzo ya kabla ya Mkutano mkuu mbowe hayagusii?

Mchezo mchezo wenye uhuni

Wanadanganyana tu na wadanganyane wao kila siku itakuwa Chadema ndo ya Mahakamani wakati Vyama vinginevyo vinajijenga!!!

Chama kina ka Uhuni fulani kwenye maamuzi ni maigizo


Unaweza fika hatua ukaona bora ubaki bila Chama Au ujishkize CCM tu


Britanicca

Ww hujishikizi ccm, bali uko ccm. Kama ni kweli hutaki chama cha kihuni basi ccm ilipaswa kuwa saratani kwako kuliko ilivyo CDM. Unajifanya hauko ccm, lakini sentensi zako hazikubebi kwenye hilo, mahaba hayajifichi.
 
Du Paschal tena,

Swali rahisi sana, wakati Halima na wenzake wameenda bungeni juzi walikua ni wa chama gani mpaka speaker atoe maamuzi ya kuwalinda?

Kwa upande mmoja chama kimewafukuza na kutoa taarifa bungeni. Bunge ilipaswa kufuata sheria ....mbunge lazima atokane na chama.

Upande wa pili waathirika walisema nao wamepata taarifa za kufukuzwa kwao ila wana nia ya kwenda mahakani. Hivyo hawakuwa na amri ya mahakama inayomzuia speaker kuwafukuza.

Je speaker alipata wapi mamlaka au sheria ipi kuwaacha bungeni kabla ya amri ya mahakama?

Je nani mwenye maamuzi ya hovyo?
Refer case ya Lema, wabunge wa CUF etc.

Paschal hujadeclare interest kwamba wewe ni CCM hivyo andiko lako liko biased na sababu zipo wazi na ndio maana utapingwa sana hapa. Pia una ajenda mbaya dhidi ya Chadema kwani kwa siku nne mfululizo umeandika mada moja umebadili jina la title. Hata kama ni spinning kuna njia ya kufanya na sio kwa njia unayotumia ipo wazi mno.

Uteuzi hauji kwa kuandika biased ideas bali kutumia critical thinking plus proffessionalism
Hivi nyie manazi wa chadema msichoelewa ni nini?

Umeambiwa wameshaenda mahakamani kupinga kufukuzwa uanachama, sasa spika angefanyaje maamuzi juu ya suala lililoko mahakamani?
 
Katiba ya CHADEMA ipo chini ya Katiba ya Tanzania.

Kwa kuwa hawajaipata haki yao kwa kupitia Katiba ya Chama, wana nafasi ya kuitafuta kupitia Katiba ya Nchi.

Chama siyo mali ya mtu binafsi, ila umma.
Mbona hiyo Katina haikumlinda Lisu? Aliposhambulia Kuna watu mazezeta Sana hii nchi.
 
Barua yenye sahihi ya mtu mmoja tubhaiwezi kuwa kiambatanisho sahihi, chama ni kikundi cha watu na maamuzi yanafanyika kwa pamoja , je hiyo barua iliambataniswa na resolution (muhtasar)inayonakili maamuzi hayo
 
Back
Top Bottom