Tusimlaumu sana Ndugai kama Spika, wakulaumiwa ni mwenyekiti wake anayependa kupewa heshima na kusifiwa muda wote
Rudini nyuma mwanzo mwanzo wakati awamu hii inaanza, ilifikia mahali hadi baadhi ya wabunge wakawa wanatamani vikao viongozwe na Ndugai maana yule bi mdada ni kama alikuja na maelekezo maalumu ya ku deel na wapinzani ki ubabe ubabe tu
Hakuna asiyependa kula. Huyu mgogo mambo yalibadilika alipousoma mchezo wa kupinduliwa na bi mdada ndio akili zikahama na mafaili yakapotea kabisa
Sasa siku zote jambo la kuiga na kufuata maelekezo lazima litakuumbua tu, ndiomaana anaonekana kituko sasa hivi
Tumuhurumia, Rais ni cheo cha mwisho kabisa, hakuna mkuu mwingine wa muhimili mwenye nguvu ya kupingana nae kama bado ana njaa.
Kina Prof Assad wako wachache nchi hii.
Mimi kuna wakati huwa najiuliza, hivi Ndugai ana mke na watoto kweli? Haoni aibu kutizamana nao usoni kwa anayoyafanya?