Spika Ndugai: Mbowe alikuwa Ulaya sasa katumwa na watu wake anapotosha kuhusu ripoti ya CAG

Queries zinatoa majibu ya kweli amesimamishawa ili kupisha uchunguzi. Utaratibu wa audit upo hivyo lazima mkaguzi auibue hoja kisha majibu.
Mbona Kigwangalla ameachwa wakati yeye ametajwa kabisa kwenye ripoti ya CAG?
 
Nyau tangu lini akawika kama jogoo. Subwoofer tulia wanaume waongee.
 
Hivi Ndugai hawezi kujenga hoja zake (vihoja) bila kuwataja watu?
Hawezi,ni poyoyo na anchoweza ni miaasho na taarab.Alikuwa kama kiatu cha Jiwe kila mahala alimfuata na kumsifia Mara kashamgeuka.Ukitaka kufahamu upoyoyo wa hawa watu,subiri hiyo ripoti itakavyochakachuliwa na hizo kamati.
 
Sijaona mahali popote Mbowe amezungumzia ripoti ya CAG au mimi sijasikia vizuri?
 
mangi hizo ni audit queries na opinions sio final conclussion.
Waambie Mkuu....mi huwa naangalia michango ya wengi humu wasojua chochote kuhusu ukaguzi nacheka tu.

Ila nitailaumu serikali yangu ya CCM kuwaacha mitaani waliomaliza form four 2012. Walitakiwa kuwa jela wote....ndo wanatusumbua humu jamvini.
 
Spika sindano imemuingia inabidi akubali dozi apone...
Huyu hafai kuendelea kuliongoza bunge chini ya mama samia maana Ndugai ni mnafiki
 
Spika angepambana na CAG kwa hoja badala ya kumshambulia Mbowe kwamba anapotosha ripoti ya CAG
 
Huyu jamaa asipomtaja Mbowe huwa hawezi kuishi? Ni dhambi kubwa tutakayoijutia kwa vizazi vingi vijavyo kuwa na mtawala mwenye mawazo mgando dizain hii
 
Afadhali Polepole anapost video za kucheza mdumange na kupika makande!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…