Econometrician
JF-Expert Member
- Oct 25, 2013
- 16,879
- 31,253
Ndio maana mirembe iliwekwa Dodoma kwa ajili ya kusogeza huduma kwa Wananchi kwenye hali hizo,nasema uongo ndugu zangu!.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Haa umenikumbusha waliokuwa wamebeba mabegi yaliyojaa kwenye vituo vya kupigia kura, huu ulikuwa ni uchaguzi huru wa CCMKwani uongo sio Wananchi wa Kongwa tu-Tanzania sisi ni Mazuzu hatujielewi.
Karne ya 21 eti Wabunge karibu 100 wanapitaje bila kupingwa halafu tunajisifu.
Kwani zuzu hana haki ya kuchaguliwa au kupita bila kupingwa😜!? Afu Asad mwenyewe naye ni mazuzu walewale, sasa anakelwa nini chizi akikuita chizi, mtu timamu si atapuuzia tu!?Kweli kila zama na kitabu chake. Leo hii Ndugai anapiga yowe bila kuchukua hatua zidi ya Assad,ingekuwa kipindi cha Kayafa sasa hivi Assad angekuwa mikononi mwa Polisi kwa amri ya Ndugai. Haya ni maneno ya Ndugai.
"Kuna Mzee anatukosea sana Wabunge,anatuita mazuzu,nina miaka 25 pale Kongwa na vipindi viwili nimepita bila kupingwa,na hata kesho nikienda nitapita bila kupingwa,kwanini uniite zuzu? Wananchi wa Kongwa ni mazuzu wamechagua zuzu mwenzao?"
Credit: Dar Mpya.
Sent using Jamii Forums mobile app
Aya majina ya JUMA ni bure kabisa.
Ona hapa:-
[emoji117]Juma jux
[emoji117]Juma lokole
Huyu si alikuwa anapiga fimbo kichwani wengine? Ndo maana anapita bila kupingwa maana wenye akili wakija anawapiga fimbo vichwani anataka abakili yeye na mazuzu wenzake!Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema anakerwa na tabia ya baadhi ya watu kuwaita wabunge mazuzu na kuwataka wajenge utamaduni wa kuheshimiana.
Akifungua wiki ya AZAKI jijini Dodoma Jumamosi Oktoba 23, Ndugai amesema, “Sio unaitwa Azaki basi unawasema wenzako maneno unayotaka ya hovyo. Tumewahi kugombana na baadhi ya wazee, mzee unatuita jina sisi hatulipendi…Hivi tumekosea wapi kama unamuita mtu jina la Juma anasema mimi jina hilo silitaki.
“Tatizo lako nini? Unang’anga’ania kuita hilo jina, we ni nani? Haiwezekani kama mwanadamu akikwambia hiki sina raha nacho kiache na wewe hukiachi, kama kweli wewe ni muungwana mtu wa Mungu utakiacha.”
Amesema matokeo ya kutoheshimiana ni wazee (ambao hakuwataja) wanawasema wabunge ni mazuzu wakati wana akili.
Amesema wao hawana muda wa kubishana bishana na watu wana namna hiyo.
Amesema yeye amechaguliwa na watu 400,000 kuwa mbunge kwa miaka 25 katika chaguzi mbalimbali na tena mara mbili amepita bila kupingwa.
“Hata kesho nikienda kusimama (kugombea) tafuta wa kusimama na mimi hutampata. Akisimama ni mpambe wa kusindikiza. Halafu wewe unaniita zuzu yaani wale watu una maanisha ni mazuzu wamechagua zuzu mwenzao?”amehoji.
Ndugai alipongeza Azaki kwa kazi nzuri wanazofanya lakini akasema wachache wao wamekuwa wakitumika na wana ajenda zisizokuwa za kwao na kwamba Azaki chache zimekuwa na ajenda za kupata fedha kutoka mahali fulani (hakukutaja).
“Sasa kama we njaa yako ni hela ndio maana lazima zitungwe sheria sasa zinazokufuata kwenye hela. Eeeeh utatuambia nani amekupa, kiasi gani, ziko wapi, utazitumiaje na utaleta taarifa kwa kila shilingi zamani haikuwa hivyo tuliaminiana lakini baada ya kuona mwenendo usio ridhisha ndio tukatunga sheria,”amesema.
Ndugai amesema kama wasipoweka sera ya kuambiana na kurekebishana (wao kwa wao mashirika) basi hata sheria zitakazotungwa siku za usoni zitakuwa kali zaidi.
inawezekana ata anaowaongoza pia ni mazuzu labda 🤣🤣Kweli kila zama na kitabu chake. Leo hii Ndugai anapiga yowe bila kuchukua hatua zidi ya Assad,ingekuwa kipindi cha Kayafa sasa hivi Assad angekuwa mikononi mwa Polisi kwa amri ya Ndugai. Haya ni maneno ya Ndugai.
"Kuna Mzee anatukosea sana Wabunge,anatuita mazuzu,nina miaka 25 pale Kongwa na vipindi viwili nimepita bila kupingwa,na hata kesho nikienda nitapita bila kupingwa,kwanini uniite zuzu? Wananchi wa Kongwa ni mazuzu wamechagua zuzu mwenzao?"
Credit: Dar Mpya.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahaaaa......wewe unaona hawafanani?!WELEMA alimuita Kafurila TUMBILI
HeheKwani uongo sio Wananchi wa Kongwa tu-Tanzania sisi ni Mazuzu hatujielewi.
Karne ya 21 eti Wabunge karibu 100 wanapitaje bila kupingwa halafu tunajisifu.