Spika Ndugai: Nimechaguliwa na watu 400,000 kuwa mbunge kwa miaka 25, mara mbili nimepita bila kupingwa, unaniita ZUZU?

Spika Ndugai: Nimechaguliwa na watu 400,000 kuwa mbunge kwa miaka 25, mara mbili nimepita bila kupingwa, unaniita ZUZU?

Inawezekana katika mazuzu 400,000 wewe ndio una nafuu ndio maana wamekuchagua uwe mwakilishi wao!
HIV katika hao Laiki Nne yule uliyempiga Fimbo ya kichwa yumo?!
Mkuu umeandika kwa code myambuka
 
Ukweli lazima usemwe hata kama mchungu. Mh Ndungai J alimnyosha huyu CAG wa kale hadi akijiona hajui.
 
Mkuu mshale21, asante kwa hii, na bahati nzuri niko hapa Dodoma na hii niliisikia kwa masikio yangu mwenyewe.


P.

Ndugu Pascal we kama mchambuzi wa hotuba za viongozi tunaomba utoe maoni yako juu ya kauli hii na si kushukuru mleta uzi maana lengo lake ni kuijadili. Au bado una hofu ya kuitwa tena mjengoni.
 
Mkuu mshale21, asante kwa hii, na bahati nzuri niko hapa Dodoma na hii niliisikia kwa masikio yangu mwenyewe.


P.

hiyo clip yako haina maneno ya uzuzu aliyosema Ndugai.... unatuwekea ya nini hapa? acha kuwa mwandishi zuzu na wewe....!

na kwenye hiyo clip yako we mwenyewe umeongea utopolo.... tunawaletea mfululizo wa wiki ya Azaki .... mfululizo wa wiki maana yake wiki zitafululiza, sasa maadhimisho ya Azaki yatafululiza mpaka lini, mwaka ?
 
Mkuu metro wanasumbua machinga wanaopita sema mitaa mingi walio kwenye vizimba wale hata hawasumbuliwi ila kuzunguka kwa kuuza matunda utasumbuliwa na metro tena wakichukua mzigo fine yake kubwa kule faraday..
Mku kwa hiyo sasa siyo kama miaka 1994 - 2000 . Lakini mambo yanabadilika kuendana na nyakati.
Ww upo hump bado
 
huko ulikochaguliwa kuna nini cha ajabu?, kuna wasomi wengi?, kuna maendeleo mengi?, uchumi upo juu sana?, miundombinu ipo vizuri sana?, maisha ya mtu mmoja mmoja yapo juu sana?, mbona sisikii sifa nzuri tokea huko?. Unaweza ukapigiwa kura na watu milioni ila wasiwe si watu wa...............
 
Hawa wote Assad , Jenerali Ulimwengu pamoja na Ndugai wote akili zao ziko sawa, sijui niwaite kama aliyekuwa msemaji wa wekundu wa Msimbazi alivyowaita waandishi wa habari?
Mzee Ulimwengu ni hazina ya Wananchi wote wanahitaji kuwa huru.
Assad ni mtu anayechukia wizi wa mali za umma na aneyenda mabadiliko
Nikuommbe tu hawa Wazee usiwafanishe kabisa kwani weledi wao unaonekana na Watannzania
 
1635079473104.png
 
Ngugai atakuja kuwa na uzee wa tabu sana.historia itakuja kumtesa sana.huyu tusishangae akiandika kitabu na kuomba radhi mapema sana.
 
Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema anakerwa na tabia ya baadhi ya watu kuwaita wabunge mazuzu na kuwataka wajenge utamaduni wa kuheshimiana.

Akifungua wiki ya AZAKI jijini Dodoma Jumamosi Oktoba 23, Ndugai amesema, “Sio unaitwa Azaki basi unawasema wenzako maneno unayotaka ya hovyo. Tumewahi kugombana na baadhi ya wazee, mzee unatuita jina sisi hatulipendi…Hivi tumekosea wapi kama unamuita mtu jina la Juma anasema mimi jina hilo silitaki.

“Tatizo lako nini? Unang’anga’ania kuita hilo jina, we ni nani? Haiwezekani kama mwanadamu akikwambia hiki sina raha nacho kiache na wewe hukiachi, kama kweli wewe ni muungwana mtu wa Mungu utakiacha.”

Amesema matokeo ya kutoheshimiana ni wazee (ambao hakuwataja) wanawasema wabunge ni mazuzu wakati wana akili.

Amesema wao hawana muda wa kubishana bishana na watu wana namna hiyo.

Amesema yeye amechaguliwa na watu 400,000 kuwa mbunge kwa miaka 25 katika chaguzi mbalimbali na tena mara mbili amepita bila kupingwa.

“Hata kesho nikienda kusimama (kugombea) tafuta wa kusimama na mimi hutampata. Akisimama ni mpambe wa kusindikiza. Halafu wewe unaniita zuzu yaani wale watu una maanisha ni mazuzu wamechagua zuzu mwenzao?”amehoji.

Ndugai alipongeza Azaki kwa kazi nzuri wanazofanya lakini akasema wachache wao wamekuwa wakitumika na wana ajenda zisizokuwa za kwao na kwamba Azaki chache zimekuwa na ajenda za kupata fedha kutoka mahali fulani (hakukutaja).

“Sasa kama we njaa yako ni hela ndio maana lazima zitungwe sheria sasa zinazokufuata kwenye hela. Eeeeh utatuambia nani amekupa, kiasi gani, ziko wapi, utazitumiaje na utaleta taarifa kwa kila shilingi zamani haikuwa hivyo tuliaminiana lakini baada ya kuona mwenendo usio ridhisha ndio tukatunga sheria,”amesema.

Ndugai amesema kama wasipoweka sera ya kuambiana na kurekebishana (wao kwa wao mashirika) basi hata sheria zitakazotungwa siku za usoni zitakuwa kali zaidi.
Sawa
 
Ndugu Pascal we kama mchambuzi wa hotuba za viongozi tunaomba utoe maoni yako juu ya kauli hii na si kushukuru mleta uzi maana lengo lake ni kuijadili. Au bado una hofu ya kuitwa tena mjengoni.
Akikujibu nitag unajua mzee wetu P anachekesha Sana ukiisoma akili yake Ni km yupo kwenye mtanziko...

Inabidi avae koti jeusi kuficha rangi yake...
 
Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema anakerwa na tabia ya baadhi ya watu kuwaita wabunge mazuzu na kuwataka wajenge utamaduni wa kuheshimiana.

Akifungua wiki ya AZAKI jijini Dodoma Jumamosi Oktoba 23, Ndugai amesema, “Sio unaitwa Azaki basi unawasema wenzako maneno unayotaka ya hovyo. Tumewahi kugombana na baadhi ya wazee, mzee unatuita jina sisi hatulipendi…Hivi tumekosea wapi kama unamuita mtu jina la Juma anasema mimi jina hilo silitaki.

“Tatizo lako nini? Unang’anga’ania kuita hilo jina, we ni nani? Haiwezekani kama mwanadamu akikwambia hiki sina raha nacho kiache na wewe hukiachi, kama kweli wewe ni muungwana mtu wa Mungu utakiacha.”

Amesema matokeo ya kutoheshimiana ni wazee (ambao hakuwataja) wanawasema wabunge ni mazuzu wakati wana akili.

Amesema wao hawana muda wa kubishana bishana na watu wana namna hiyo.

Amesema yeye amechaguliwa na watu 400,000 kuwa mbunge kwa miaka 25 katika chaguzi mbalimbali na tena mara mbili amepita bila kupingwa.

“Hata kesho nikienda kusimama (kugombea) tafuta wa kusimama na mimi hutampata. Akisimama ni mpambe wa kusindikiza. Halafu wewe unaniita zuzu yaani wale watu una maanisha ni mazuzu wamechagua zuzu mwenzao?”amehoji.

Ndugai alipongeza Azaki kwa kazi nzuri wanazofanya lakini akasema wachache wao wamekuwa wakitumika na wana ajenda zisizokuwa za kwao na kwamba Azaki chache zimekuwa na ajenda za kupata fedha kutoka mahali fulani (hakukutaja).

“Sasa kama we njaa yako ni hela ndio maana lazima zitungwe sheria sasa zinazokufuata kwenye hela. Eeeeh utatuambia nani amekupa, kiasi gani, ziko wapi, utazitumiaje na utaleta taarifa kwa kila shilingi zamani haikuwa hivyo tuliaminiana lakini baada ya kuona mwenendo usio ridhisha ndio tukatunga sheria,”amesema.

Ndugai amesema kama wasipoweka sera ya kuambiana na kurekebishana (wao kwa wao mashirika) basi hata sheria zitakazotungwa siku za usoni zitakuwa kali zaidi.
Azaki ndo nini
 
Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema anakerwa na tabia ya baadhi ya watu kuwaita wabunge mazuzu na kuwataka wajenge utamaduni wa kuheshimiana.

Akifungua wiki ya AZAKI jijini Dodoma Jumamosi Oktoba 23, Ndugai amesema, “Sio unaitwa Azaki basi unawasema wenzako maneno unayotaka ya hovyo. Tumewahi kugombana na baadhi ya wazee, mzee unatuita jina sisi hatulipendi…Hivi tumekosea wapi kama unamuita mtu jina la Juma anasema mimi jina hilo silitaki.

“Tatizo lako nini? Unang’anga’ania kuita hilo jina, we ni nani? Haiwezekani kama mwanadamu akikwambia hiki sina raha nacho kiache na wewe hukiachi, kama kweli wewe ni muungwana mtu wa Mungu utakiacha.”

Amesema matokeo ya kutoheshimiana ni wazee (ambao hakuwataja) wanawasema wabunge ni mazuzu wakati wana akili.

Amesema wao hawana muda wa kubishana bishana na watu wana namna hiyo.

Amesema yeye amechaguliwa na watu 400,000 kuwa mbunge kwa miaka 25 katika chaguzi mbalimbali na tena mara mbili amepita bila kupingwa.

“Hata kesho nikienda kusimama (kugombea) tafuta wa kusimama na mimi hutampata. Akisimama ni mpambe wa kusindikiza. Halafu wewe unaniita zuzu yaani wale watu una maanisha ni mazuzu wamechagua zuzu mwenzao?”amehoji.

Ndugai alipongeza Azaki kwa kazi nzuri wanazofanya lakini akasema wachache wao wamekuwa wakitumika na wana ajenda zisizokuwa za kwao na kwamba Azaki chache zimekuwa na ajenda za kupata fedha kutoka mahali fulani (hakukutaja).

“Sasa kama we njaa yako ni hela ndio maana lazima zitungwe sheria sasa zinazokufuata kwenye hela. Eeeeh utatuambia nani amekupa, kiasi gani, ziko wapi, utazitumiaje na utaleta taarifa kwa kila shilingi zamani haikuwa hivyo tuliaminiana lakini baada ya kuona mwenendo usio ridhisha ndio tukatunga sheria,”amesema.

Ndugai amesema kama wasipoweka sera ya kuambiana na kurekebishana (wao kwa wao mashirika) basi hata sheria zitakazotungwa siku za usoni zitakuwa kali zaidi.
Kwanza inapasa itukubalishe kama hawo wapiga kura 400000 walipiga klura kwa ridha zao au ndio iliutmika nguvu na uchakachuwaji wa kura.

naamini leo ikifanywa kura ya wazi basi hapati hizo anazojisifia.
 
“Hata kesho nikienda kusimama (kugombea) tafuta wa kusimama na mimi hutampata. Akisimama ni mpambe wa kusindikiza. Halafu wewe unaniita zuzu yaani wale watu una maanisha ni mazuzu wamechagua zuzu mwenzao?”amehoji.
Yule aliyemtandika bakora nusra amtoe roho hamkumbuki?

ZUZU ni zuzu tu, hata hajui anachokisema. Kura 400,000 alizipata lini huyu kilaza.

'Phase' hii ya hawa viongozi mazuzu, imeibadili sana Tanzania ionekane kuwa ni nchi ya hovyo hovyo sana. Chukulia tokea mwaka alioingia huyu zuzu Bungene, hapo ndipo tulipoanza kuwa na viongozi wasiokuwa na sifa za kuwa viongozi.
 
Crisis management!! Hakuna mfumo unaojiendesha unaotatua vimigogoro vinavyojitokeza! Mwanasiasa kaitwa zuzu imekuwa agenda wanatangaziwa nchi nzima!
Hizo azaki zenye kufadhili hazina mifumo ya ufuatiliaji wa fedha zao hadi atokee Job fulani kuwasaidia? Nijuavyo mimi, kwa Tz kuchaguliwa miaka mingi haina maana kama mbunge umelineemesha jimbo lako vilivyo. Lakini pia kuna wkt tulisikia alipata ubunge baada ya kumlabua mpinzani kwa bakora na kumsababishia matatizo ya kiafya - hilo hajalisema. Huenda huko kwao pia liko tatizo la vyoo vya shule, maji, barabara au hata wazee wanaokufa kwa kukosa huduma stahiki za matibabu na hajagusia hayo! Au kwa Job mambo ni saafi?
Tz tuna safari ndefu
 
Aseme yote, ila zile gharama za matibabu yake zilikuwa ni kubwa sana, kiasi cha kuishtua hata ofisi ya CAG. Pengine suala la " imbecile" linaweza kuamzia hapo.
Na ndiyo bifu lake na Professor Assad lilipoanzia. Huyu kibushuti alitumia makumi ya mabilioni ya kodi zetu kiboya sana.
 
Yule aliyemtandika bakora nusra amtoe roho hamkumbuki?

ZUZU ni zuzu tu, hata hajui anachokisema. Kura 400,000 alizipata lini huyu kilaza.

'Phase' hii ya hawa viongozi mazuzu, imeibadili sana Tanzania ionekane kuwa ni nchi ya hovyo hovyo sana. Chukulia tokea mwaka alioingia huyu zuzu Bungene, hapo ndipo tulipoanza kuwa na viongozi wasiokuwa na sifa za kuwa viongozi.
Alisema Professor Assad, 60% ya watendaji wa serikali (akiwemo huyo zuzu ndugai) walikuwa hawana sifa za kuwa kwenye nafasi hizo wanazoshikilia, kwa hiyo kama taifa tuna hasara kwa asilimia 60
 
Back
Top Bottom