Spika Ndugai: Wanaotaka nimfukuze Cecil Mwambe Bungeni, wamwambie aniandikie barua ya kujiuzulu

Spika Ndugai: Wanaotaka nimfukuze Cecil Mwambe Bungeni, wamwambie aniandikie barua ya kujiuzulu

Influenza

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2018
Posts
1,509
Reaction score
3,756
Spika wa Bunge, Job Ndugai amewataka wale wote wanaotaka amfukuze Bungeni, Cecil Mwambe basi wamshauri (Mwambe) amwandikie Spika barua ya kujiuzulu kwake, halafu waone kama ataendelea kukaa Bungeni.

Spika Ndugai amesema hayo Bungeni leo Mei 12, 2020 na kusema kuwa maamuzi hayo yote ya kumrejesha Mwambe Bungeni, yamekuja kutokana na yeye kupata barua ya upande mmoja.

Amehoji, "Nimeeleza Mwambe amewahi kuniandikia barua lini? Hivi wewe ungekuwa Spika ungefanyaje? Huna barua ya mtu aliyejiuzulu ungefanyaje? Unamfukuza tu?"

Ameongeza "Lazima mchunguze na muangalie mzani uko wapi. Mwambe yupo hajafa, mwambieni aandike barua anikabidhi mimi. Akishanikabidhi muone kesho yake itakuwaje"

Aidha, Spika Ndugai amesema leo jioni atatolea ufafanuzi kuhusu tamko lililotolewa na CHADEMA, kwamba Wabunge wake waliojiweka karantini kwa sasa hawatorudisha posho kwa sababu wao sio wezi.
 
Spika amelikoroga anatafuta pa kutokea. Mwambe ataandika barua kwa kuwa ameambiwa then ataondolewa Bungeni kwa msemo amejiuzulu.

Amejiuzulu mara mbili hahahhh hii nchi ni Mungu tu anajua

Social Media ni Msumeno unakata huku na huku
 
Ili CCM ianguke ni lazima mambo na matukio kama haya yapete nafasi/yatokee kama ambavyo ilimbidi Mwana wa Adamu asulubiwe ili sisi wanadamu tuokolewe.

Subirini yako mengi yanakuja na yatakayowashangaza zaidi.

Wamenyimwa maarifa ili utawala wao ufike mwisho na hivyo hawajui walitendalo mithili ya Wayahudi waliomsulubisha Yesu kutimizi maandiko,hivyo na hawa CCM nao wanayatenda haya ili kutimiza anguko lao pasipo kujua.
 
Hivi wanasheria emu tupeni dondoo kidogo, mtu aliyetamka hadharani mchana kweupe na ushahidi wa ile clip bado ipo huwa haitoshi? mpaka aandike barua?

Natamani Mbowe kesho aende kwenye Media aseme nimejiuzulu ubunge Spika kweli ataendelea kumwambia wewe bado ni mbunge mpaka ulete barua?
 
Hawa waliandika barua baada ya kufukuzwa?
IMG-20200512-WA0009.jpg
IMG-20200512-WA0010.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Spika wa Bunge, Job Ndugai amewataka wale wote wanaotaka amfukuze Bungeni, Cecil Mwambe basi wamshauri (Mwambe) amwandikie Spika barua ya kujiuzulu kwake, halafu waone kama ataendelea kukaa Bungeni.

Spika Ndugai amesema hayo Bungeni leo Mei 12, 2020 na kusema kuwa maamuzi hayo yote ya kumrejesha Mwambe Bungeni, yamekuja kutokana na yeye kupata barua ya upande mmoja...
Na huyu je mbona hamrudishi
IMG-20200512-WA0005.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom