Spika sikiliza ushauri wa Mpina, iundwe tume kuchunguza kwa nini January Makamba amechelewesha mradi wa JNHP. Pia mizengwe ya bei ya mbolea

Atafukuzwa kwenye chama, hapo amemgusa Rostam Azizi
 
Mkuu kwani ikiundwa tume kuna shida gani? issue siyo bwawa kuna mbolea, petrol, bidhaa mbalimbali kupanda bei n.k
 
Mkuu, mataifa mengine hayajapata taarifa ya vita ya Ukraine. Sisi tuko mbele ya muda taarifa ilitufikia mapema hivyo madhara yake kuwa makubwa ncini kwetu
 
Alipoteuliwa makamba kuwa waziri wa hii wizara tulijua yafuatayo;
1. Michezo michafu ya kubinafsisha gas yetu ambayo mwendazake aliikataa kwa kuanza kujenga hili bwawa utazimwa!
2. Lengo kuu la hawa watu wa awamu ya 4 ni gas itumike kama nishati ya umeme hivyo wao kuwauzia umeme Tanesco na kuendelea kuifilisi nchi.
3. Mpango huu umeasisiwa na muuza gas mkubwa na tapeli mkubwa na hatari sana!
Kumbekeni mikataba mibovu ya gas ktk awamu ya 4 iliyopitishwa na wabunge wa ccm lengo lilikuwa hili lkn magu alikataa
 
Hujui kama hujui chochote kuhusu umeme na mikataba zaidi ya kwamba wewe ni mhanga wa uwongo wa Magufuli. Na nyinyi wajinga ndiyo mlikuwa mtaji wa Magufuli kwa miaka 5.

JNHPP was wastage of money. Hilo dude litabakia white elephant. Litajengwa ila halitakuja kuzalisha hizo megawati 2,100 za umeme.

Kwa maamuzi ya Dikteta mmoja mkemia asiyeamini sayansi, tumeharibu baioanuai ya selous na kukata miti yenye saizi ya ukubwa wa Mkoa wa Dar es Salaam. Hili litatugharimu milele.

Ni wakati wa kufanya maamuzi magumu kwa kusitisha kuendelea kujenga na kuendelea na umeme wa gesi. Kwa sasa Kinyerezi 1 & 2 zinachangia 60% ya umeme tunaotumia Tanzania. Na zinatumia hardly 10% ya gesi ya Mtwara

Miradi yote ya maji yaani Kidatu, Mtera, Kihansi, Nyumba ya Mungu, Hale, Pangani nk inachangia 40%. Numbers don't lie. Umeme wa kutegemea mvua siyo reliable na vile vile una athari kwa mazingira.

Kama Magufuli asingetokea mwaka 2015 tungepiga hatua kubwa sana kiuchumi kwa kuwa;
1. Kinyerezi 3 & 4 zingekamilika na kuwa chanzo kikuu cha nishati.

2. Tusingevuruga baioanuai ya Selous kwa kukata miti ili tujenge bwawa la umeme kwa ajili ya kupata Megawati 2,100 tu ambazo zinapatikana kwa kutumia 25% tu ya gesi ya Mtwara.
 
January ndiye rais?
January ndiye VP?
January ndiye PM?
January ndiye Baraza la mawaziri?

Hivi mleta mada unadhani waziri January ana nguvu kiasi cha kuchelewesha mradi ambao rais na serikali yake wote wanataka uishe?

Acha utoto.
No more funds are available for the project. I see it as a failing elephant.
 
January ndiye rais?
January ndiye VP?
January ndiye PM?
January ndiye Baraza la mawaziri?

Hivi mleta mada unadhani waziri January ana nguvu kiasi cha kuchelewesha mradi ambao rais na serikali yake wote wanataka uishe?

Acha utoto.
Hilo nalo neno !! Mnyonge mnyongeni !
 
Hoja hapa ni kuunda tume kuchunguza kucheleweshwa mradi wa JNHP
Ukweli iundwe tume tujue mbivu na mbichi,Luhaga kuna jambo analijua linafanyika kuhusu huu mradi.
Ikumbukwe January Makamba alipokuwa wizara ya mazingira alikuwa kikwazo kuhusu huu mradi ,Magufuli alimtumbua.

Tujiulize pia ni kwanini mradi ambao ulitakiwa uwe umekamilika leo hii umesogezwa miaka miwili mbele ?.

Nasema kuna hujuma haswa ,alianza na visingizio vingi,mara crane mara milango imekosewa.
Sasa kaja na mradi wa kufanyia ukarabati miuondo mbinu ya tanescco akiweka bajeti kubwa wakati bwa la nyerere la umeme likipewa fedha kiduchu,huyu ni muhuni tu
 
Atakapoona Jina la January kugombea urais ndo atajua kuwa hajui.
 
Mpina aache kumsakama Makamba , Rais alishakata mzizi wa fitina pale Tabora na kusema wachape kazi wasisikilize maneno ya watu!
Lamz tukumbuke kuwa Makamba aliukuta huo mradi ulishaanza na watu wengine si ajabu mpaka sasa hata kuna mambo mengine yahusuyo mradi huo akawa hayajui sawasawa!........Kwa anayejua Mpina na Makamba walikotoka atafahamu tu ni kwanini kila wakati anashughulika sana na wizara ya Makamba kuliko wizara nyingine! Tuliona maliasili kulitokea madudu alikaa kimya! Tamisemi , wizara ya elimu, Afya , maji, na nyinginezo hakupo sawa lakini huko hagusi anamtafuta Makamba tuu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…