Alipoteuliwa makamba kuwa waziri wa hii wizara tulijua yafuatayo;
1. Michezo michafu ya kubinafsisha gas yetu ambayo mwendazake aliikataa kwa kuanza kujenga hili bwawa utazimwa!
2. Lengo kuu la hawa watu wa awamu ya 4 ni gas itumike kama nishati ya umeme hivyo wao kuwauzia umeme Tanesco na kuendelea kuifilisi nchi.
3. Mpango huu umeasisiwa na muuza gas mkubwa na tapeli mkubwa na hatari sana!
Kumbekeni mikataba mibovu ya gas ktk awamu ya 4 iliyopitishwa na wabunge wa ccm lengo lilikuwa hili lkn magu alikataa
Hujui kama hujui chochote kuhusu umeme na mikataba zaidi ya kwamba wewe ni mhanga wa uwongo wa Magufuli. Na nyinyi wajinga ndiyo mlikuwa mtaji wa Magufuli kwa miaka 5.
JNHPP was wastage of money. Hilo dude litabakia white elephant. Litajengwa ila halitakuja kuzalisha hizo megawati 2,100 za umeme.
Kwa maamuzi ya Dikteta mmoja mkemia asiyeamini sayansi, tumeharibu baioanuai ya selous na kukata miti yenye saizi ya ukubwa wa Mkoa wa Dar es Salaam. Hili litatugharimu milele.
Ni wakati wa kufanya maamuzi magumu kwa kusitisha kuendelea kujenga na kuendelea na umeme wa gesi. Kwa sasa Kinyerezi 1 & 2 zinachangia 60% ya umeme tunaotumia Tanzania. Na zinatumia hardly 10% ya gesi ya Mtwara
Miradi yote ya maji yaani Kidatu, Mtera, Kihansi, Nyumba ya Mungu, Hale, Pangani nk inachangia 40%. Numbers don't lie. Umeme wa kutegemea mvua siyo reliable na vile vile una athari kwa mazingira.
Kama Magufuli asingetokea mwaka 2015 tungepiga hatua kubwa sana kiuchumi kwa kuwa;
1. Kinyerezi 3 & 4 zingekamilika na kuwa chanzo kikuu cha nishati.
2. Tusingevuruga baioanuai ya Selous kwa kukata miti ili tujenge bwawa la umeme kwa ajili ya kupata Megawati 2,100 tu ambazo zinapatikana kwa kutumia 25% tu ya gesi ya Mtwara.