Jerlamarel
JF-Expert Member
- Sep 14, 2021
- 843
- 2,525
Hawa ni viongozi wawili ambao wote ni wakuu wa mihimili 2 katika nchi, wote ni wa chama kimoja, wote walikuwepo tangu enzi za Hayati JPM, wote walikuwa ni "Makamu" kipindi cha Hayati JPM, na wote kwa sasa ndiyo wakuu wa mihimili hiyo baada ya watangulizi wao mmoja kufariki na mmoja kujiuzulu msawazia.
Baada ya JPM kufariki, Mama Samia aliposhika hatamu aliamua kubadili upepo wa aina ya uongozi wake, hakutaka kufuata mrengo aliokuwa nao JPM wa siasa za ubabe ubabe.
Lakini hali ni tofauti kwa huyu Mama Tulia, kauli yake ya jana akiwa huko Mbeya inaonesha bado ana element za u-JPM pure.
Kwenye "Mkutano wa Wadau wa Demokrasia" uliofanyika mwaka huu, Mama Samia alisema yafuatayo:
"Ni mazungumzo, siyo nguvu wala ugomvi wala matusi au kutishana, hivyo niwaombe wenzangu wenyeviti wa vyama vya siasa, tusitazame yaliyopita, tutazame mbele kwa matumaini. Tuweke nguvu zetu pamoja kujenga Tanzania mpya yenye kusameheana, yenye kuheshimiana, na kufungua kurasa mpya ya kwenda na demokrasia yetu Tanzania."
Jana Spika Tulia amekuja na hii kauli ambayo inaendana kinyume kabisa na kauli ya Rais Samia ya hapo juu:
"Isitokee kijana yeyote akaungana na mtu yeyote, anayemsema vibaya Rais wa JMT. Rais Samia ni Rais wa Nchi, lakini pia ni Mwenyekiti wa chama chetu. Asitokee mtu yeyotee, wa nje ya chama, wa ndani ya chama akawa anamsema vibaya Rais Samia halafu wewe unamtazama, shughulika naye na nyooka naye."
Maswali ya kujiuliza:
1. Nani anaongea ukweli wake wa moyoni, Rais ama Spika?
2. Je, Spika bado ana element za utawala uliyopita?
3. Je, Spika kwa kupingana hadharani na Rais anakuwa hajavunja ile "Collective Responsibility" aliyoizungumzia Rais alipomtumbua Mulamula?
4. Ni kwa nini pamoja na Rais kuruhusu vyama vifanye shughuli zake lakini bado wanazuiwa kuendesha mikutano ya kisiasa, katika mazingira haya tumuamini Spika ndiyo yuko "Real?".
Baada ya JPM kufariki, Mama Samia aliposhika hatamu aliamua kubadili upepo wa aina ya uongozi wake, hakutaka kufuata mrengo aliokuwa nao JPM wa siasa za ubabe ubabe.
Lakini hali ni tofauti kwa huyu Mama Tulia, kauli yake ya jana akiwa huko Mbeya inaonesha bado ana element za u-JPM pure.
Kwenye "Mkutano wa Wadau wa Demokrasia" uliofanyika mwaka huu, Mama Samia alisema yafuatayo:
"Ni mazungumzo, siyo nguvu wala ugomvi wala matusi au kutishana, hivyo niwaombe wenzangu wenyeviti wa vyama vya siasa, tusitazame yaliyopita, tutazame mbele kwa matumaini. Tuweke nguvu zetu pamoja kujenga Tanzania mpya yenye kusameheana, yenye kuheshimiana, na kufungua kurasa mpya ya kwenda na demokrasia yetu Tanzania."
Jana Spika Tulia amekuja na hii kauli ambayo inaendana kinyume kabisa na kauli ya Rais Samia ya hapo juu:
"Isitokee kijana yeyote akaungana na mtu yeyote, anayemsema vibaya Rais wa JMT. Rais Samia ni Rais wa Nchi, lakini pia ni Mwenyekiti wa chama chetu. Asitokee mtu yeyotee, wa nje ya chama, wa ndani ya chama akawa anamsema vibaya Rais Samia halafu wewe unamtazama, shughulika naye na nyooka naye."
Maswali ya kujiuliza:
1. Nani anaongea ukweli wake wa moyoni, Rais ama Spika?
2. Je, Spika bado ana element za utawala uliyopita?
3. Je, Spika kwa kupingana hadharani na Rais anakuwa hajavunja ile "Collective Responsibility" aliyoizungumzia Rais alipomtumbua Mulamula?
4. Ni kwa nini pamoja na Rais kuruhusu vyama vifanye shughuli zake lakini bado wanazuiwa kuendesha mikutano ya kisiasa, katika mazingira haya tumuamini Spika ndiyo yuko "Real?".