Spika Tulia Ackson azuia Mjadala wa Sakata la Bandari Bungeni, asema Bunge lilishatoa maamuzi

Spika Tulia Ackson azuia Mjadala wa Sakata la Bandari Bungeni, asema Bunge lilishatoa maamuzi

Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson amezuia mjadala wa sakata la bandari kuzungumzwa bungeni lakini akaruhusu kuwa litakapokuja kwa utaratibu mwingine wa kibunge itakuwa ruksa.

Spika Dk Tulia ametoa kauli hiyo leo Jumanne Agosti 29,2023 muda mfupi baada ya kipindi cha maswali na majibu ya wabunge ambapo amesema kuwa bunge lilishamaliza mjadala huo hivyo wabunge wanatakiwa kuendelea kuwasikiliza wananchi.

Aisee we mama jiandae tu utazitapika 2.5mUSD utake usitake It is a promise to you madam and to all who have decided to side with our oppressors!!!
 
Kwani huu ni mkataba wa kwanza kupigiwa kelele. Au sababu aliyesaini ni muislam
Mkataba upi mlishawahi kuupigia kelele kama huu wa waarabu?

Williamson mpaka leo hii wapo, mbona mpo kimya! Kisa mzungu! Wachina wameingia mkataba na viwanda vingi mbona mpo kimya! Kisa mwarabu/muislamu! Asilimia kubwa ukichunguza wanaopinga mkataba huu ni wakristo.
 
Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson amezuia mjadala wa sakata la bandari kuzungumzwa bungeni lakini akaruhusu kuwa litakapokuja kwa utaratibu mwingine wa kibunge itakuwa ruksa.

Spika Dk Tulia ametoa kauli hiyo leo Jumanne Agosti 29,2023 muda mfupi baada ya kipindi cha maswali na majibu ya wabunge ambapo amesema kuwa bunge lilishamaliza mjadala huo hivyo wabunge wanatakiwa kuendelea kuwasikiliza wananchi.



Yupo sahihi, namuunga mkono 100%, walipewa mda wa kuzungumza wa kaharibu, wakatukejeli, wakae kimya.
 
Mkataba upi mlishawahi kuupigia kelele kama huu wa waarabu?

Williamson mpaka leo hii wapo, mbona mpo kimya! Kisa mzungu! Wachina wameingia mkataba na viwanda vingi mbona mpo kimya! Kisa mwarabu/muislamu! Asilimia kubwa ukichunguza wanaopinga mkataba huu ni wakristo.
Mjinga wewe kwani mkataba wa bandari unalinganisha na wa Williamson! Kama muislamu ni mjinga kama wewe atapingwa tu!
 
Dodoma,Jumanne 29/08/2023.
Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson amezuia mjadala wa makata wa bandari kujadiliwa ikiwa tayari Bunge limeishamaliza majukumu yake ya awali, huku akisema linaweza kujadiliwa endapo litaletwa katika utaratibu mwingine wa kibunge.Spika Dk Tulia ametoa kauli hiyo leo Jumanne Agosti 29, 2023, muda mfupi baada ya kipindi cha maswali na majibu ya wabunge ambapo amesema kuwa Bunge lilishamaliza mjadala huo hivyo wabunge wanatakiwa kuendelea kuwasikiliza wananchi.

Katika mkutano wa 11 wabunge walipitisha makubaliano ya mpango wa Serikali katika kuingia makubaliano na DP World katika kuendesha bandari, ambapo kumekuwa na mjadala mrefu ukihusisha wanasiasa, wanasheria, wanaharakati, viongozi wa dini na wananchi kwa ujumla.

SOURCE.
Mwananchi online Newspapers.29/08/2023.
 
Mihimili imepigwa ganzi wanasubiri maelekezo
 
Dodoma,Jumanne 29/08/2023.
Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson amezuia mjadala wa makata wa bandari kujadiliwa ikiwa tayari Bunge limeishamaliza majukumu yake ya awali, huku akisema linaweza kujadiliwa endapo litaletwa katika utaratibu mwingine wa kibunge.Spika Dk Tulia ametoa kauli hiyo leo Jumanne Agosti 29, 2023, muda mfupi baada ya kipindi cha maswali na majibu ya wabunge ambapo amesema kuwa Bunge lilishamaliza mjadala huo hivyo wabunge wanatakiwa kuendelea kuwasikiliza wananchi.

Katika mkutano wa 11 wabunge walipitisha makubaliano ya mpango wa Serikali katika kuingia makubaliano na DP World katika kuendesha bandari, ambapo kumekuwa na mjadala mrefu ukihusisha wanasiasa, wanasheria, wanaharakati, viongozi wa dini na wananchi kwa ujumla.

SOURCE.
Mwananchi online Newspapers.29/08/2023.
Tunasubiri maelekezo!!
 
Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson amezuia mjadala wa sakata la bandari kuzungumzwa bungeni lakini akaruhusu kuwa litakapokuja kwa utaratibu mwingine wa kibunge itakuwa ruksa.

Spika Dk Tulia ametoa kauli hiyo leo Jumanne Agosti 29,2023 muda mfupi baada ya kipindi cha maswali na majibu ya wabunge ambapo amesema kuwa bunge lilishamaliza mjadala huo hivyo wabunge wanatakiwa kuendelea kuwasikiliza wananchi.

Supika hiki tumeshakibaini. Hakina uzalendo kimeweka tumbo mbele. Pia akili hakina kujidai tu eti kimesoma sana. Mama mwenyewe tumbo mbele, majaji nao waoga. Kwa hiyo hakuna wa kumdhibiti mama.
 
Yale maamuzi ya kura ya ndiooooooooo huku yeye ndo akijipa kazi ya mwanasheria mkuu wa serikali, siyo?
 
Hapawezi kuwa na mjadala mwingine wa DP World kwa muda huu, kila kitu kilishamalizika. Mwezi wa kumi mwishoni mwekezaji anakabidhiwa bandari, na baada ya siku chache kupita anakuja mwekezaji mwingine tena hapo hapo TPA.

Halafu kuna uwekezaji mwingine wa bandari ya Bagamoyo. Masuala ya kiuchumi ukiyachanganya sana na siasa unapoteza muda na kuendelea kufuga umaskini.
 
Huyu mama tulishasema hafai!
Anazidi kulinda alichokula!
Ila atambue kuwa "yaliyofichika kwa binadamu kwa Mola yapo wazi"
Mola wetu huwa halali, upanga wake wa moto upo njiani kuangamiza kizazi cha dhuluma dhidi ya wananchi.
 
Anaposema bunge linatakiwa kuendelea kuwasikiliza wananchi, halafu akasema tena bunge limeshamaliza mjadala kuhusu bandari, anaamanisha bunge la sasa sio mwakilishi wa wananchi, kwasababu bunge haliwezi kuzuia kujadili kile ambacho wananchi wanataka, kwa kifupi ni kwamba, hili bunge la Spika Tulia sio mwakilishi wa wananchi.
Anachosema Tulia ni sahihi. Bunge lilijiamlia lenyewe bila kushirikisha Wananchi. Yaani Yale ni mawazo Yao binafsi na si ya wanaowawakilisha. Litakqpoletwa upya labda ndo watakuwa wanawasilisha mawazo ya Wananchi. Lakini Kwa Sasa ni kweli Wabunge wasiojitambua wameshamaliza wasubiri hukumu ya Wananchi.
 
Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson amezuia mjadala wa sakata la bandari kuzungumzwa bungeni lakini akaruhusu kuwa litakapokuja kwa utaratibu mwingine wa kibunge itakuwa ruksa.

Spika Dk Tulia ametoa kauli hiyo leo Jumanne Agosti 29,2023 muda mfupi baada ya kipindi cha maswali na majibu ya wabunge ambapo amesema kuwa bunge lilishamaliza mjadala huo hivyo wabunge wanatakiwa kuendelea kuwasikiliza wananchi.

huku ni kuwafunga midomo, miguu na mikono na kuwang'oa meno wabunge bila ganzi, na kuondoa kabisa ladha halisi ya mijadala ndani ya bunge, kwasababu hawana meno ni viboyoyo huwezi skia wala kuelewa wanachoongea. si sawa..
 
Mimi naona yupo sahihi kwakuwa bunge lilisha upigia kura na kuupisha huo mkataba tata sasa mjadala wa nini tena?
Kura yenyewe feki hata hatujui nani kapiga kura vipi.

Jambo nyeti kama hili kwa nini limepigiwa kura ya sauti na halikupigiwa kura ya mbunge mmoja baada ya mwingine tujue nani kapiga kura vipi?
 
Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson amezuia mjadala wa sakata la bandari kuzungumzwa bungeni lakini akaruhusu kuwa litakapokuja kwa utaratibu mwingine wa kibunge itakuwa ruksa.

Spika Dk Tulia ametoa kauli hiyo leo Jumanne Agosti 29,2023 muda mfupi baada ya kipindi cha maswali na majibu ya wabunge ambapo amesema kuwa bunge lilishamaliza mjadala huo hivyo wabunge wanatakiwa kuendelea kuwasikiliza wananchi.

Saa ya UKOMBOZI ikifika, Mungu huifanya mioyo ya Watawala kuwa migumu na anguko hufuata. Farao/Firauni aliwekewa kiburi moyoni kwa kuringia nguvu za majeshi, hivyo kupuuza kila kitu alichoambiwa na Nabii Mussa kuwaachia Wana wa Israel waende zao. CCM kwa hili la bandari, shupazeni tu shingo zenu anguko linakuja, saa ya UKOMBOZI imeletwa na DP World.
 
Supika hiki tumeshakibaini. Hakina uzalendo kimeweka tumbo mbele. Pia akili hakina lujidai tu eti kimesoma sana. Mama mwenyewe tumbo mbele, majaji nao waoga. Kwa hiyo hakuna wa kumdhibiti mama.
Mbona sasa hakinenepi?
 
Kwangu mimi naona hii ni kuwafunda midomo wabunge!
F4gd_f9X0AAlsIf.jpg
 
Back
Top Bottom