Wakuu sijui tuiite neema kwa timu yetu ya u17...ila yote kheri ..Kutokana na taifa la Mali kupigwa ban na Shirikisho la soka duniani FIFA kutokana na serikali ya Taifa hilo la Mali kuinglia masuala ya kamati ya mpira wa miguu...... Mali wamepigwa stop kujihusisha na mashindano yeyote yale.
Kumbuka Mali U17 ilikuwa imefudhu baada ya kuipiga Ethiopia U17 nje ndani.... Kule bamako 2-0 na kule adis Ababa 2-1...... Baada ya hapo Mali U17 akafudhu afcon U17 Gabon 2017 kwa jumla ya goli 4-1. Kundi B ndilo kundi lililokuwa limejumuisha Mali, Tanzania, Angola na Niger.... Ila kutokana na ban hiyo ya Shirikisho la soka duniani FIFA sasa ni rasmi kuwa Timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 17 ya Ethiopia ambao walitolewa katika hatua ya mwisho kwa jumla ya goli 4-1 ndio wanaochukua nafasi ya Mali U17 katika mashindano mwezi ujao kule Gabon.
Sasa kundi B. Litakuwa hivi baada ya Mali kuondoka
- Tanzania
- Angola
- Niger
- Ethiopia.
Kutoka kwa timu ya taifa ya Mali kumepunguza kwa kiasi ugumu wa kundi hilo hii ni kutokana na namna taifa hilo la Mali lilivyo na miundombinu bora kwa soka la vijana..... Naiombea mafanikio timu yetu ya taifa ya vijana ya Serengeti boys katika kushinda michezo yake yote katika kundi hili.
#Serengeti_boys washkaji zetu [HASHTAG]#wanawezaSana[/HASHTAG].