Spot on Mh PM Majaliwa, Mkandarasi na TARURA wawajibishwe

Spot on Mh PM Majaliwa, Mkandarasi na TARURA wawajibishwe

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
16,419
Reaction score
26,594
20221021_083846.jpg

Miradi ya mingi ya TARURA ina matatizo ya usimamizi.

Makandarasi walio chaguliwa kwenye tenda za TARURA wengi ni wababaishaji na hivyo kukosa viwango vya kutekekeza miradi.

Waziri Mkuu Majaliwa kalionyesha hilo wazi baada ya ukaguzi wa barabara huko Ukerewe.
Mkandarasi kapewa siku kumi na mhandisi msimamizi, Waziri Mkuu kamwongezea tano kabisaa, kuwa siku kumi na tano.

Hilo safi kabisa maana sasa mpira umewaangukia TARURA, huyo mkandarasi waliyempa tenda kama ni kanjanja, hataweza kukamilisha huo mradi in 15 days.

Majuzi huko Morogoro, kuna mkandarasi aliyekuwa akijenga daraja, alifutika michanga na vipande vya mbao badaka ya zege.

Hizo ni dalili zote za kukosa usimamizi wa kitaalam toka TARURA.
 
TARURA NA TAKUKURU zilianzishwa ki makosa.
 
Ninashauri TARURA iwe chini ya uangalizi wa TANROADS ili kuiangalia utendaji kazi wake. Tunakoelekea TARURA ni janga la Taifa.

Pia upatikanaje wa watumishi wa TARURA haukuzingatia viwango na ubora wao bali ni kundi la watu walijipatia madaraka na nafasi za ulaji
 
Ninashauri TARURA iwe chini ya uangalizi wa TANROADS ili kuiangalia utendaji kazi wake. Tunakoelekea TARURA ni janga la Taifa.

Pia upatikanaje wa watumishi wa TARURA haukuzingatia viwango na ubora wao bali ni kundi la watu walijipatia madaraka na nafasi za ulaji
Tuseme ukweli tu, TARURA ina matatizo ya kimsingi katika kutekeleza miradi.

Tusisahau kuwa wahandisi wengi wa TARURA ni wale waliokuwa katika Halmashauri za Wilaya, wengi hawana uzoefu au weledi kiutendaji kwa kulinganisha na TANROADS.
 
Back
Top Bottom