Stakabadhi ghalani ni kupe kwa mkulima

Stakabadhi ghalani ni kupe kwa mkulima

IZENGOB

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2014
Posts
323
Reaction score
317
Mfumo huu ni umekua ni wa hovyo sijawahi kuona.Fikiria mkulima amejinyima kula vizuri,kuvaa na watoto wake lakini leo hii mkulima anakuja kumkopesha tajiri ambaye ana mali kedekede inauma sana.

Zaidi ya mwezi sasa tangu niuze mazao yangu kwa mfumo huu ambao serikali imeshindwa kuusimamia sijalipwa pesa yangu ya ufuta jambo ambalo linanipa wakati mgumu na maisha yangu kuendelea kuwa magumu kila kukicha.

Wanunuzi wa mazao haya ni matajiri wakubwa ambao wanatunyonya wakulima hali ambayo inatufanya wakulima kuendelea kuwa na maisha magumu.

Hebu fikiri
Hakuna pembejeo yoyote ya ambayo mkulima kapewa.Wala hakuna msaada wowote wa pesa wala kitaalamu ambao unatolewa kwa mkulima lakini mkulima amekuwa akikopwa mazao yake na wengine kudhulumiwa kabisa.

Kuna haja gani ya kuwa na mfumo huu katika nyakati hizi za sayansi na technolojia.Sisi wakulima tunaomba kuuza mazao hetu na pesa kupewa palepale au kuandikiwa cheki palepale.

Ni wazi kiwa wizara husika wanashindwa kuona kuwa sisi wakulima wa nchi hii tunadhurumika pakubwa.Mh Bashe Huoni kuwa wizara yako inashindwa kusimamia vyema makampuni yanayonunua mazao kutoka kwa wakulima? Sioni sababu ya kuwa na mfumo huu kandamizi na onevu kwa mkulima.
 
Mkulima ndio anayebeba mzigo..na ndiye anayeumia katika wote..chabgamoto sana..ila serikali iliangalie hili.

#MaendeleoHayanaChama
 
Pole sana. Sasa nimeelewa kwa nini uliandika ule uzi wa msaada ulime nini baada ya kupata lile burungutu la hela.

Achana na mazao ya stakabadhi, Ufuta,pareto,korosho,tumbaku.
N.k
 
Mkulima ndio anayebeba mzigo..na ndiye anayeumia katika wote..chabgamoto sana..ila serikali iliangalie hili.

#MaendeleoHayanaChama
Mimi sijawahi kuona maskini anamkopesha tajiri.Silimi tena zao la ufuta mimi.Nikilima napeleka mwenyewe kuuza Dar.wanatoa pesa baada ya masaa 4 tu.
 
Pole sana. Sasa nimeelewa kwa nini uliandika ule uzi wa msaada ulime nini baada ya kupata lile burungutu la hela.

Achana na mazao ya stakabadhi, Ufuta,pareto,korosho,tumbaku.
N.k
Ni bora nikajikita mazao ya bustani kuliko kuumia hivi
 
Mnada unasimamiwa na taasisi inaitwa KORECU
Basi hiyo ni ule mfumo wa masanduku ambao ni wa kizamani,wanachama ombeni TMX wasimamie malipo yenu,hawa ni wakala wa Serikali ambaye ndani ya masaa 48 tokea mnada ufanyike mnatakiwa muwe mmeingiziwa pesa zenu kupitia usimamizi wao
 
Mimi sijawahi kuona maskini anamkopesha tajiri.Silimi tena zao la ufuta mimi.Nikilima napeleka mwenyewe kuuza Dar.wanatoa pesa baada ya masaa 4 tu.
Nifafanulie vzr hapa?

#MaendeleoHayanaChama
 
Back
Top Bottom