Stars vs Moroco in JF

Stars vs Moroco in JF

Tulishindwa kuwafunga wale Central African Republic itakuwa Morroco Bao hizo 4 labda kushinda bao 2-1 tukubali yaishe basi. Tuombe Taifa Stars wafanye ya Niger walivyompiga Egypt kwao 3-0. Kuhusu Mwalimu mie naona tumuweke Fundi wa Vijana mzungu atolewe na fundi wa Vijana alipwe kama anavyolipwa Mzungu yule hana upendeleo wa wachezaji wapo wazuri wengi timu za mikoani na visiwani si Yanga na Simba tu na timu za Dar-es-salaam zimejaliwa kuweka wachezaji timu ya taifa.
 
tembelea hapa
OLEOLETV.COM | Watch Live Streaming TV Online Free Feed Link Broadcast Channel En Vivo Gratis Directta
GMT + 1
[TABLE="class: listing"]
[TR="bgcolor: #a2b8fa"]
[TD="class: list_date"]21:30
- 23:30
[/TD]
[TD="class: list_flag"]
dz.gif
[/TD]
[TD="class: list_champ"]CAF Africa Cup of Nations[/TD]
[TD="class: list_team"]Algeria - Central African Republic[/TD]
[TD="class: list_tv"]http://www.oleoletv.com/channelteam/a-0/4/184/a-58593.html[/TD]
[/TR]
[TR="bgcolor: #c8d7fa"]
[TD="class: list_ball"][/TD]
[TD="class: list_date"]21:30
- 23:30
[/TD]
[TD="class: list_flag"]
ma.gif
[/TD]
[TD="class: list_champ"]CAF Africa Cup of Nations[/TD]
[TD="class: list_team"]Morocco - Tanzania [/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Mechi inaanza saa nne na nusu usiku kwa saa za Afrika mashariki (22hr30). Tujipe moyo tu na kuonyesha uzalendo lakini ukweli ni kwamba hatuendi popote tunakamilisha ratiba tu!

Asante mkuu kwa ratiba maana Ngeleja kakata umeme nilikuwa nawaza sana wapi nitaangalizia kumbe mpaka saa nne!
 
Kama nchi ina wenyewe, na timu ina wenyewe na wenyewe ni magamba.
 
naomba kikosi kitakacho kamilisha ratiba usiku wa leo..
 
Kuna kituo kitarusha live mechi hii?Nina hamu kuangalia mechi hii kupima maendeleo yetu.Kiufundi Poulsen yupo safi sana kwani angalau sasa Taifa stars wanamiliki mpira.

Ah wapi! Paulsen hanalolote! Bora hata Maximo. Kilichomfanya Maximo kukosa mkataba mpya ni kiburi lakin alikuwa mzuri. Kuhusu game ya leo ,tuombe tu miujiza ya Mungu. Lakin nawatakia kila la kheri Taifa Stars. Ila kenya wanaroho mbaya sana,yaani waliibania Uganda jana na kusababisha EA kukosa timu hadi sasa. Tuombe leo Stars washinde 3 kwa 0.
 
Tehteh Raha ya hapa ndio mambo kama haya Lazima Link ya U Siasa iwepo humu Game haijaanza hatutajuwa kama tutashinda au tutashindwa ila imani yangu tutashinda ila kwa style za maoni humu tukifungwa sijui kama kutakalika na marushano ya Chi CHe MI isije kuwa tabu.
 
Tulishindwa kuwafunga wale Central African Republic itakuwa Morroco Bao hizo 4 labda kushinda bao 2-1 tukubali yaishe basi. Tuombe Taifa Stars wafanye ya Niger walivyompiga Egypt kwao 3-0. Kuhusu Mwalimu mie naona tumuweke Fundi wa Vijana mzungu atolewe na fundi wa Vijana alipwe kama anavyolipwa Mzungu yule hana upendeleo wa wachezaji wapo wazuri wengi timu za mikoani na visiwani si Yanga na Simba tu na timu za Dar-es-salaam zimejaliwa kuweka wachezaji timu ya taifa.
Unaujua mpira au unazijua fitna za bongo?Huwezi kumfananisha Poulsen na Julio(nasikia ndio anafanya form four!).Wabongo tunaongoza kudharaua elimu.Julio amefanya nini au umeisikia timu ipi ameifundisha angalau tu ikacheza mpira?Maneno yake ya 'kibongobongo' yanawachanganga wengi.Kocha unaulizwa unaionaje Nigeria,unajibu Nigeria ni sawa na uji!Again,akaulizwa unauchukuliaje mchezo na Uganda,akajibu 'Uganda walibebwa na refa.Matokeo tuliyaona wenyewe.Tuache uswahili,oh Mzungu...mweupe!Makocha wakibongo waende shule kwanza kabla ya kupewa timu ya taifa.
 
Nawatakia kila la kheri vijana wetu wanaotupeperushia bendera yetu huko. Nawaombea wawe mabalozi wema na warudi na ushindi.

Ila wakishinda tu utaona siasa zinaanza. Na yale magazeti (Uhuru, Habari leo etc.) watabadili na kuwaita JK Eleven (badala ya Taifa Stars), etc. Kila la heri Stars!
 
Kwako Lonestriker mie sikatai sijamchukia Poulsen sababu Mzungu Mie napenda fundi awe mzuri angalau Maximo akiwepo atayeweza kuweka nizamu na pia Sie Watanzania tukaweka Siasa nje kidogo tunaweza kuwa mbali kuhusu hayo maneno ya julio sikuwahi kuyasikia kama kweli kasema hivyo nakubali atakuwa kakosea ila kuhusu Julio ndio kwanza kaenda Form Four hilo pia sijui ila angalau ya yeye kakubali kwenda huko Form Four kwa umri wake ule kama ni kweli kaonesha hajazarau Elimu, Na Kuhusu Uswahili sie watanzania ni Waswahili Tatizo Neno Uswhaili tunalitumia vibaya wenzenu wanajiita English kwa kuwa Proud nasie tujifunze Kujiita sie Waswahili kwa njia ya kuwa Proud si Kwa Namna Mbaya. Kurekibishana tunapokosea si kitu kibaya.
 
Ila wakishinda tu utaona siasa zinaanza. Na yale magazeti (Uhuru, Habari leo etc.) watabadili na kuwaita JK Eleven (badala ya Taifa Stars), etc. Kila la heri Stars!

Kweli kabisa!!
 
4-4-1-1 Ndio atatumia leo Fundi Poulsen Taifa Stars: Juma Kaseja,Erasto Nyoni,Idrisa Rajab,Juma Nyoso,Agrrey Morris,Shaaban Nditi,Mohamed Rajab,Henry Joseph(C),Mbwana Samata,Abdi Kassim,Dan Mrwanda.

Bench😀ihile,Nassor cholo,John Bocco,Ramadhan Chombo,Mrisho Ngassa,Nadir Haroub,Jabir Aziz. Nimeipata Blog Flani.
 
Uzalendo huu unanitesa,najipa matumaini lakini ni sawa na kmpigia kiziwi mziki!!!!!!!!!!!!!,nakumbuka enzi zile za Marcio.

Ngoja nimuombe Muumba atende miujiza jioni ya leo japo mhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhh
 
Mungu ibariki timu yetu Taifa na uitendee japo muujiza uskiu wa leo,japo jamaa mmoja wa gamba anataka cc tuikimbie nchi hii kisa cc sio wanamagamba
 
4-4-1-1 Ndio atatumia leo Fundi Poulsen Taifa Stars: Juma Kaseja,Erasto Nyoni,Idrisa Rajab,Juma Nyoso,Agrrey Morris,Shaaban Nditi,Mohamed Rajab,Henry Joseph(C),Mbwana Samata,Abdi Kassim,Dan Mrwanda.

Bench😀ihile,Nassor cholo,John Bocco,Ramadhan Chombo,Mrisho Ngassa,Nadir Haroub,Jabir Aziz. Nimeipata Blog Flani.
Mbona Ngassa sikuhizi anaanzia bench? Kiwango kimeshuka au nini?
 
Back
Top Bottom