Startimes Tanzania: Support thread (maswali, maoni na ushauri)

Tatizo LA mtandao wenu ni baashi ya channels zenu zina ganda kama TV 1
NIPO KONGOWE YA MKURANGA
 
Lengine hivyo kwenye station yenu hamna filam za kutosha kila siku katika channel ya tabibu mnaweka move hizohizo mpaka tumezichoka
 
Bado mnatumiaga tu startimes mpaka leo?[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] mwafaaaaaa
 
mimi king'amuzi hakionyeshi channel mbili nazo ni ITV na STAR TV hivi tatizo ni nini? hii wiki ya pili sasa
 
Habari za mdaa huu wanajamvi wenzangu,

Nimeamua kuandika uzi huu kwa wanaJF wenzangu ili kuwajuza kuwa kampuni kubwa na ya kwanza kuingia nchini kwetu ya Ving'amuzi aina ya STARTIMES ni wababaishaji,pia huduma zao zimembana mteja kwa maana nyingne vifurushi vyao ni ghali sana.

Jana STARTIMES huduma kwa wateja walinipigia simu mida ya saa nne na robo,nikaamua kupokea na kusikia sauti ya nzuri na ya ukarimu kutoka kwa muhudumu wao wakike,kisha akaniambia tunapenda kukutaarifu kwamba tuna offer kwa wateja wetu inayoendelea sasa katika ving'amuzi vyetu.Ukinunua kifurushi cha kuanzia buku sita unapata offer ya kuangalia chanels za packages nyingine kama vile smart pack ana uhuru,nikawajibu sawa lakini ni siku tatu tu zimepita tangu nilipie kifurushi cha mambo na sijaona chochote,akanijibu kwamba niliwahi kujiunga kabla ya offer yao ambayo ilianza 1st April,nikamuuliza je nikijiunga na sasa hv ntapata kuona hzo chanels zote?

Akaniambia definetly nitaziona.Basi mimi nikaamua kulipia tena na kusubiri about 45mins, bila mafanikio yoyote, nikaamua kuwapigia simu kwakutumia ile namba yao ya customer service na ikapokelea nikapewa maelezo ambayo mimi naweza kuyaita poorer, wrong and fake instractions kutokana hayukuweza kufanya kazi hata mpaka sasa kwani nilibaki kuambiwa just wait for 15 mins then utazikuta,mara mwingine weka TBC1 for 15 mins then utakuta tumekuwekea mara ya mwisho kabisa nikaulizwa ni mtoa huduma yupi aliyekupigia simu,nikamwambia akawaulize voda au TCRA kwani wao ndo wenye mamlaka na wateja wao.

Tatizo lingne la hawa majamaa ni kwamba voucher yako ikikata wanakubakizia chaneli mbili tu ambazo ni TBC1 na TV1.

PENDEKEZO;Kwa wateja wapya wenye mpango na hilo likampuni la startimes ni vyema kuchagua ving'amuzi vingine kwani startimes hawana huruma na hawajali wateja wao.
PLEASE,DON'T BE FOOLED BY THE MASKS THEY WEAR,MAKE YOUR RIGHT CHOICE USIJE UKAJUTIA PESA YAKO.
 
wanaudhi kweli, mm nilikuwa najiunga kila mara kifurushi cha elfu 18 nakuta channel hamna nikiwapigia wanasema unejiunga kifurushi cha elfu 9×2 na chaajabu baada ya mwez huduma inakata (hapo wameshanipiga buku 9) nimevumilia miez mitatu nikahamia azam
 
Nilitaka kuachana na continental niwe na startimes kama ni hivyo basi bora nibaki tu.
Maana continental nao ni janga ila bora kuliko haya ya startimes.
 


Anayetafuta ama anayetaka king'amuzi cha startimes tafadhari anitafute in-bobo! nitampatia buReeeee kabisa, nina miaka kama minne hivi sikitumii nimekifungia tu kwenye boksi.

Tido Mhando alinihamasisha na kuniaminisha kuwa baada ya muda mfupi startimes kitakuwa king'amzi bora chenye channel za ukweli. Cha ajabu Tido mwenyewe sidhani hata kama ana hicho king'amzi nyumbani kwakwe, isitoshe alishawakimbia hao startimes.

Kwa hiyo kama unakihitaji hicho king'amzi tafadhari njooooo in-bobo nikupatie chapuchap
 
Wapuuzi Sana [HASHTAG]#startimes[/HASHTAG]. Kama kunamtu anampango wa kutumia.,tafuta upande mwingine to.
Maana hawa wanaboa Sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…