Startimes wameshatangaza kuonesha AFCON, Azam bado wapo kimya

Mkulima na Mfugaji

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2013
Posts
1,047
Reaction score
1,832
Kampuni ya Star Media wamiliki wa Startimes wameshatangaza kwamba wataonyesha mechi zote 52 za AFCON Cameron kuanzia January, ila washindani wao kibiashara Azam media mpaka sasa wapo kimya.

Kama hawataonesha watoe taarifa ili tusijisumbue kulipa, na tulipie Startimes kwa sisi wenye ving'amuzi viwili.

Wasije wakatufanyia kama kwenye kombe la dunia, watu tunalipia halafu wanakuja na mpango wa kuchagua mechi
 
Azam imelala yoo
 
Nimetoka kucomment sasaaivi kwenye page yao...sijui azam wanakwama wapi, hivi azam wanashindwa kupata vibali vya EPL kwel?? Kwa ukubwa walionao wangekua wanaonesha EPL si kila nyumba kungekua na Azam sasa wanatuletea Bundasliga ligi aina hata mvuto imepitwa mbali sana hata na Laliga....sijui wanakwama wapi kuweka EPL ligi namba moja duniani...haya hata hii Afcon inawapiga chenga Takataka kabisa

NB: Azam wana mchango mkubwa sanaaaa kwenye ligi ya bongo na Sekta ya michezo kwa ujumla
 
Azam hawana hela ya kurusha EPL
 
Usifikiri ni rahisi kiasi hicho. Dstv wana haki miliki kuonesha EPL kwa nchi zote za kusini mwa jangwa la Sahara.
Ingekuwa rahisi kila kampuni ya ving'amuzi wangeonesha EPL
 
Kwa wanaotumia Azam waweza kuona mechi zote kupitia UBC TV.(Uganda Broadcasting Corporation).
 
Sisi wenye DSTV hatuna shida ila kusiwepo na mvua kubwa!

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…