Startup za Tanzania wajitahidi kuwa na maajabu, wanafanya mambo ya kawaida sana

Startup za Tanzania wajitahidi kuwa na maajabu, wanafanya mambo ya kawaida sana

Artifact Collector

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2019
Posts
6,617
Reaction score
10,205
Makamu wa Rais wa Marekani, Kamala Haris amekuja Tanzania, na moja ya sehemu atakazo tembelea ni Tanzania startup assocciation, binafsi yangu nilisubiria kwa hamu kuona hao watu atakao kutana nao nione idea zao

To be honest nimekua dissapoint sana kwa watu ambao wamepewa nafas ya kukutana na kamala harris, idea zao ni za kawaid sana kwenye macho ya wazungu na watu wa western, sitawataja majina ila idea zao za kawaida sana

Na sio tu Tanzania hata nchi nyingi za afrika idea za watu ni za kawaid sana lazima tuambiane ukweli ndo maana hata ukiangalia kenya ambapo wanasifiwa kwa kuraise ela ila startup zao zimejikita kwenye finance same kwa nigeria, maeneo kama pharmaceuticals, agriculture, technicians, na urban planning, ambayo ni muhimu sana kwa sababu ya ukuaji wa kasi wa population wa afrika yamesahulika

Mfano kwenye urban planning ni tatizo kubwa sana afrika, miji mingi ya afrika ni mibaya haiko organized michafu ndo maana mpaka leo tunatumia blueprint ya mipango miji ya mkoloni ni aibu kubwa sana, mfano kwa dar es salaam tumeshindwa tengeneza maeneo mazuri ya kuish zaid ya masaki ya mkoloni

Mfano ukienda France kuanzia architecture, urban planning ni tofauti kabisa na Ujerumani, au England, Scandinavia countries urban planning zao zinafanana same kwa USA na Canada, huku Afrika hatuja identity kwenye urban planning na architecture haya yanawezekana kama kukiwa na startup zinatakazokujs na innovative idea

Stakeholder wa masuala ya technologia badilikeni acheni na kuwekeza nguvu kubwa kwenye PR huko twitter huku kiuhalisia mawazo yenu ni mediocre
 
 
Mkuu startups nyingi watu hawaanzishi kwa passion au kusolve tatizo bali kujishkiza baada ya ajira kuonekana ngumu ndio maana ni ideas nyepesi tu wanatumia
 
Back
Top Bottom