Mkuu hapo kwenye red kunaibua maswali mengi kuliko majibu :suspicious:. Ninachoweza kusema ni kuwa, sio kila kitu kipo kama kinavyooneka.
Hapo kwenye blue imekaa vizuri sana, na kwa sasa jamaa anaweza akajisajili GPSA (Government Procurement Services Agent) ili atambuliwe kama supplier baada ya kujaza zile bidding documents kama hiyo hapo chini
Michango yenu nimeipenda sana pia imenijenga kwa kiasi kikubwa kuendelea na biashara hii.Kifupi mimi nko kwenye hii biashara huku nikiwa nimeajiriwa muda wangu wa ziada nimekuwa nikiutumia kusimamia.Kwa kuwa mimi ni fundi sio photocopy wala printer, nimekuwa nikijifunza kwa hali na mali kupitia mitandao mbalimbali huu ufundi wa hivyo vifaa .Na kimoja kati ya vitu vinavyokwamisha watu kwenye hii biashara ni mafundi wa copy na printer.kwani stationery nyingi utakuta copy mbovu. na bila photo copy nzuri hakuna biashara. Ukimwita fundi inaweza kuchukua week na akija akitoka machine inasumbua tena.kwa hii biashara simshauri mtu asiyejituma kuifanya atachanganjikiwa.
N.B. niko mbioni natafuta frem niweze kufungua stationery ya tatu,tatizo kubwa bei ya frem.
Wajasirimali hapa mmekuwa watoa mada kwa uwazi bila kificho na kusaidiana kupeana mawazo na kuchangishana fikra mpya katika kuimarisha biashara hizi.
Kwa nyongeza tu kama eneo ni zuri, inafaa biashara mnayoongelea kuwa na malt purpose, huduma nyingi kama photo copier huwezi kuiweka kando na hata kama kuna matatizo ya kuharibika mara kwa mara. Kibiashara unatakiwa uwe na fundi wako maalumu ambaye una mkataba wa kutengeza na kuzifanyia service machine zako. Lakini hii ya kutegemea mpaka iharibike ndipo umtafute fundi hapo fundi atajifanya ni adimu na ghali zaidi. Bora uwe unatoa ndogondogo za service na inapoharibika ukimwita atakuja mara kushughulikia. Hili ni jambo la kawaida po pote duniani kwa wafanya biashara wastaarabu na waungwana.
Computer Cafe nao ni mhimu kwa vile itasogeza watu zaidi na papo siku ukikosa mauzo ya kawaida kidogo utakipata toka Cafe. Usisahau kuweka cooler ya vinywaji baridi na vitafunio kwani navyo huwafanya wateja wavutike.
Kwa vyo vyote tusitegemee kuanza biashara kubwa sana zenye mitaji mikubwa bila kuwa na uzoefu wa kuendesha kwanza hizi ndogo ili kupata uzoefu. Na pengine ukishazoea utaona afadhali kufungua zaidi matawi ya biashara ndogo ndogo kwa vile easy to manage badala ya kubwa yenye kuhitaji makubwa zaidi na kukupa stress kila leo.
Wakuu michango yenu inasubiriwa kwa hamu, feel free ku-share experience zako please.
Mkuu mimi nawashukuru kwa michango yenu maana kuna mtu wangu karibu alikuwa ameliweka mezani hilo lakini sikujua nianzie wapi. Amenunua kompyuta akawa anaomba ushauri. Naomba angalau munisaidie kujua ni vitu gani muhimu vya kuanza navyo kwa mtaji wa 2millions
2millions huwezi kufanya lolote, mwambie aongezee hela kidogo at least aanze na 5mil hata subiri sana kuanza kuingiza faida na kutanua biashara yake.
Mkuu mimi nawashukuru kwa michango yenu maana kuna mtu wangu karibu alikuwa ameliweka mezani hilo lakini sikujua nianzie wapi. Amenunua kompyuta akawa anaomba ushauri. Naomba angalau munisaidie kujua ni vitu gani muhimu vya kuanza navyo kwa mtaji wa 2millions
Used photocopy machine kwa bei poa na zipo vizuriWakuu nani anajua ufanyaji wa hii biashara je ni wapi watu hununua vitu ili waviuze kwenye stationery zao na ni vitu gani vinavyotoka zaidi.
Kwa ujumla biashara hii inafanywavipi, ndugu yangu wa karibu anataka kuanzisha biashara hii na mimi niwe partner wake lakini sina ufahamu juu ya biashara hii.
Natanguliza shukrani.
Used photocopy machine kwa bei poa na zipo vizuriMkuu sipo kwenye biashara hii kwa sasa ila nilishawahi kuifanya kwa kipindi fulani huko mikoani. Katika Business Plan zangu, huwa ninaweka exit stratergy, hivyo baada ya kupata kile nilichokitaka ktk biashara hii someone else took over. Na kwa sasa biashara imekuwa sana, lakini nikikusimulia namna ilivyoanza, unaweza usiamin (its very motivational).
Kwa uzoefu wangu, (huku Site) biashara hii unaweza ukaianza na mtaji mdogo (3m to 4m) na bado ukafanikiwa (lakin ni kama matumizi yako hayatazidi mapato yako). Wengi walianza na mitaji midogo, halafu wakawa wanawekeza ile faida inayotengenezwa kama mtaji. Kwa hiyo nikutoe wasiwasi na huo mtaji wako wa 15M. Challenge kubwa kwa hapa Dar ni RENT na mahali muafaka pa kufanyia hiyo biashara
Pia ninakushauri ufanye kitu inaitwa DEBT FINANCING, itakusaidia sana kwenye masuala ya kodi huko TRA. (Geuza huo mtaji wa 15m kama mkopo kutoka kwenye familia au rafiki). Hii itakulazimu kufanya deductions (principal + interest) kwenye mapato yako. Hivyo itakupunguza taxable income kwa kipindi cha marejesho. Kama utahitaji Tax Planning Measures zaidi (for tax saving purposes tena legally) unaweza ukaniPM
Kuhusu namna ya kulipa mshahara
Hili suala (kwa biashara hizi) kila mtu huwa analiangalia anavyoliona kulingana na ukubwa wa biashara pamoja na mapato yake kwa mwezi, bila kusahau ujuzi wa mfanyakazi husika. Personally, huwa napenda kutumia "performance indicators" kama njia ya kumlipa mfanyakazi, lakini huwa silipi chini ya Minimum wage ya serikali. Na allowance kama ya nauli na chakula (akiwa kazini) ni muhimu kama sivyo elewa kuwa atachukua mwenyewe kwa njia nyingine
N:B
Compliance ni muhimu sana, hivyo nakushauri usajili biashara yako katika mamlaka zinazohusika (itakusaidia kwenye mambo ya kibenki, utaepuka usumbufu na utajenga image nzuri kwenye jamii. Na kubwa zaidi utashiriki katika ujenzi wa Taifa lako kupitia Kodi yako.
Mamlaka zinazohusika ni BRELA, TRA na Local Government Authorities (kwa case yako ni Manispaa ya Kinondoni)
Bei gani?canon ir 2520