Ipo nini? Na unajuaje ipo haionekani na si mawazo yako tu?
Hakuna anayeamini kwa sababu ya uthibitisho.Huwezi kuthibitisha Mungu yupo.
Kwa sababu hayupo.
Ndiyo maana unakimbilia kuwa mwanamazingaombwe ya kulazimisha mambo.
SOMA VIZURI UELEWE UMEKIMBIA MASWALI KIBAO,UNAJAZA TU THREAD BILA MISINGI YEYOTE.Mfano rahisi ni hapo hapo kwenye number line hujui number ndogo zaidi upande wa negative since negativity ni infinity na hujui number kubwa vilevile upande wa positive since positivity ni infinity,kwanini basi hujui,hujui kwasababu haina mwisho itaendelea kukuwa tu kubwa daima (no end)na itaendelea kuwa ndogo zaidi daima(no beginning) lakini hiyo hali imeshikiliwa na zero as a center ,zero defines nothing lakini hiyo zero ndo source ya both infinities both kwenye positivity na negativity.kwahiyo mahesabu yanaprove logically thinking limitation kuwa tutajua mbali zaidi kuhusu yajayo ila haiwezakani kujua mwisho ya yajayo zaidi ya kianzilishi chenyewe ambacho ni zero since ndo kimeanzisha, same applies upande wa pili tutafika mbali sana kuhusu wapi ulimwengu umeanza lakini hatutofika mwanzo maana hakuna mwanzo ,anaejua mwanzo pekee ni zero maana ndo mwanzilishi.kwa upeo wangu najua GOD EXISTS NA YUPO KWENYE EMPIRE YAKE NDANI YA ZERO,na zero ni nothing,but within nothing there is SOMETHING.
Sasa nilipokuuliza kuwa wewe nae ni mpendwa wa Mungu ulikuwa unakataa nini?Siyo mimi nimejiweka.
Kwa dhana ya Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, viumbe wake wote ni viumbe wapendwa.
Akiwepo kiumbe mmoja tu ambaye si mpendwa, hata shetani, basi huyo Mungu hana upendo wote.
Ili kitu kiwepo siyo lazima ukithibitishe. Mfano, hata wewe huwezi kuthibitisha Big Bang ilitoka wapi na kwa nini ilitokea kama ilivyotokea na si vinginevyo na huwezi kuthibitisha pia kama waasisi wa Big Bang theory kuna eneo walikosea au la maana hujui na mimi sijui. Hivyo, kuna mambo mengi hatuwezi kuyathibitisha, lakini kutoyathibisha kwetu siyo ushahidi kuwa hayapo. Whether tuthibitishe au la, kama yapo, yapo na kama hayapo, hayapo.Huwezi kuthibitisha Mungu yupo.
Kwa sababu hayupo.
Ndiyo maana unakimbilia kuwa mwanamazingaombwe ya kulazimisha mambo.
Sawa.Ili kitu kiwepo siyo lazima ukithibitishe. Mfano, hata wewe huwezi kuthibitisha Big Bang ilitoka wapi na kwa nini ilitokea kama ilivyotokea na si vinginevyo na huwezi kuthibitisha pia kama waasisi wa Big Bang theory kuna eneo walikosea au la maana hujui na mimi sijui. Hivyo, kuna mambo mengi hatuwezi kuyathibitisha, lakini kutoyathibisha kwetu siyo ushahidi kuwa hayapo. Whether tuthibitishe au la, kama yapo, yapo na kama hayapo, hayapo.
Kuamini unaweza kuamini uongo wowote ule.Hakuna anayeamini kwa sababu ya uthibitisho.
Nimemfuatilia sana kiranga kwa kina nikabaini kuwa ni mgonjwa wa akili,anaumwa "Schizophrenia Paranoid", ni ugonjwa mbaya sana,anaweza akabeba mawe na kupiga watu na kisha akakana na kudai waliomwona wathibitishe hata kama alionwa na halaiki ya watu.1. Huwezi kuthibitisha uwepo wa Mungu kwa kutumia sayansi (inayotaka empirical evidence). Ila kama unataka ninaweza kusema kwamba, kama kila kilichopo ulimwenguni kilisababishwa na Big Bang, then Big Bang ilisababishwa na Mungu ambaye ndiyo chanzo cha kila kitu.
2. Sayansi is limited to the material aspect of reality, but what is beyond the material, it is silent and it's there that we need other disciplines to explain the beyond such as natural theology or metaphysics. If we force science to prove God's existence, then what we are doing is scientism (stretching science beyond its scope of competence).
Ikiwa ulichoandika hapa ni kweli, na mimi kweli nina ugonjwa wa akili, huo pia utakuwa ni ushahidi zaidi kwamba Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote hayupo.Nimemfuatilia sana kiranga kwa kina nikabaini kuwa ni mgonjwa wa akili,anaumwa "Schizophrenia Paranoid", ni ugonjwa mbaya sana,anaweza akabeba mawe na kupiga watu na kisha akakana na kudai waliomwona wathibitishe hata kama alionwa na halaiki ya watu.
Hapa tunahangaika na kichaa kabisa
Kama kuamini si jambo muhimu kwako basi pia masuala yote yenye kuhusu imani sio muhimu pia,sasa ajabu unajadili suala la Mungu ambalo ni suala lenye kuhusu kuamini kitu ambacho sio muhimu kwako.Kuamini unaweza kuamini uongo wowote ule.
Ndiyo maana kwangu si jambo la muhimu.
Swali la muhimu ni, je, unaweza kuthibitisha?
Hujaweza kuthibitisha Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote yupo.
Kwa sababu hayupo.
Kama unabisha, thibitisha.
Sina tatizo na yeyote anayeaema anaam8ni Mungu yupo.Kama kuamini si jambo muhimu kwako basi pia masuala yote yenye kuhusu imani sio muhimu pia,sasa ajabu unajadili suala la Mungu ambalo ni suala lenye kuhusu kuamini kitu ambacho sio muhimu kwako.
Sio kuamini tu ndio unaweza kuamini uongo wowote bali hata mahakami huko watu wanatoa ushahidi wa uongo na kukubalika.
Suala la uwepo wa Mungu linajulikana ni suala la imani kwa maana watu wanaamini Mungu yupo,sasa kwani kuna mtu anayesema suala la kuwepo Mungu si imani? Maana wewe umesema hauna tatizo na wenye kuamini kwa hivyo wote unajadiliana nao humu ni wale wasiochukulia hili suala ni imani.Sina tatizo na yeyote anayeaema anaam8ni Mungu yupo.
Hiyo ana haki ya kikatiba kuamini hivyo, hata mimi nitatetea haki yake ya kuamini anavyotaka.
Nina tatizo na anayesema anajua, kweli, kwa fact, kwamba Mungu yupo.
Wewe unaamini tu au unajua kweli kabisa kwa fact Mungu yupo?
Kwa hiyo wewe huna hakika Mungu yupo, unaamini tu?Suala la uwepo wa Mungu linajulikana ni suala la imani kwa maana watu wanaamini Mungu yupo,sasa kwani kuna mtu anayesema suala la kuwepo Mungu si imani? Maana wewe umesema hauna tatizo na wenye kuamini kwa hivyo wote unajadiliana nao humu ni wale wasiochukulia hili suala ni imani.
Mimi hakika ninayo kwa maana sina mashaka ila suala la uwepo wa Mungu ni la imani na hivyo linahitaji kuamini,ndio maana nakuuliza kwani kuna mtu anayesema hili suala la uwepo wa Mungu sio imani?Kwa hiyobwewe huna hakika Mungu yupo, unaamini tu?
Huwezi kuwa na hakika, halafu hapo hapo ukawa una imani, imani ni kutokuwa na hakika, unaelewa hilo?Mimi hakika ninayo kwa maana sina mashaka ila suala la uwepo wa Mungu ni la imani na hivyo linahitaji kuamini,ndio maana nakuuliza kwani kuna mtu anayesema hili suala la uwepo wa sio imani?
Hapana anasema kama tunajua kisayansi jinsi upepo unavyotengenezwa, kiasi kwamba tunaweza tengeneza upepo artificial kwa science ya kibinadamu.Upepo hatujawahi kuuona ila tunasema upo kwa kuwa tunaona tu matendo yake kama kupuliza kupeperusha n.k
Vipi wewe unayesema MUNGU hayupo kwa kuwa tu eti hajawahi kuonekana ijapokuwa tunayaona matendo yake
Yapo maswali mengi tuHapana anasema kama tunajua kisayansi jinsi upepo unavyotengenezwa, kiasi kwamba tunaweza tengeneza upepo artificial kwa science ya kibinadamu.
Au mvua, ambayo inanyesha kiasili tukiamini ni Mungu amefanya, leo kwa science iliyopo hata wewe ukifundishwa unaweza ukaitengeneza na hakuna nguvu nyingine inayoweza kuizuia mvua yako isinyeshe.
Tsunami,tetemeko,ukame,miamba tunajua kisayansi inavyotengenezwa au jinsi ya kuibomoa.
Kama hayo yanafanyika kibinadamu na kwa kufuata science principles, kwanini tuendelee kuamini uwepo wa Mungu mwenye uweza?
It is a matter of time Wanasayansi wapo karibu zaidi na ukweli kuliko fumbo la uwepo wa Mungu, ambalo tunakatazwa kuhoji baadhi ya maswali juu yake.
Mfano Nani alimuumba Mungu
Sawa.
Lakini kuna vitu havithibitishiki kwa sababu si kweli, havipo.
Kwa mfano, mtoto aliyezaliwa na mama hawezi kuthibitisha kwamba yeye (mtoto) ni mama mzazi wa mama yake.
Sasa tutajuaje huwezi kuthibitisha Mungu yupo, ila yupo, na si kwamba huwezi kuthibitisha Mungu yupo, kwa sababu hayupo?
Hususan kwa sababu habari nzima ya Mungu kuwepo ina contradiction, kama habari ya mtoto aliyemzaa mama yake mzazi mwenyewe?
Ukiwa na mwaka mmoja tarehe 6 December SAA 8 na nusu unajua ulikuwa wapi?Yapo maswali mengi tu
Mfano
Wanasema hapo mwanzo mungu aliumba mbingu na nchi
swali,: huyo mungu alikua anaishi wapi wakati anaziumba mbingu na nchi?
Unajua kuwajibu mkuu!!Ikiwa ulichoandika hapa ni kweli, na mimi kweli nina ugonjwa wa akili, huo pia utakuwa ni ushahidi zaidi kwamba Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote hayupo.
Angekuwepo, asingeumba ulimwengu ambao viumbe wake wangeweza kuumwa ugonjwa wowote.
Habari zako za kunipa mimi ugonjwa, zinaongeza ushahidi kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.
Hazioneshi kwamba Mungu huyo yupo.
Unaelewa hilo?
Pia,
Unaelewa kwamba watu wenye utaalamu wa kuagua ugonjwa wa "Schizophrenia Paranoid" maadili yao ya kazi yanawakataza kuagua watu mitandaoni na kuwasema mitandaoni, na hivyo, wewe hata hujakaribia utaalamu unaotakiwa kujua kuagua ugonjwa huu na maadili ya kazi za watu wenye mafunzo na uwezo wa kuagua ugonjwa huu?