Stephen Wassira: Kada mkongwe wa CCM asiye na kashfa

Ni kada mkongwe kivipi maana Wassira alihama CCm na kwenda akihamahama kama vyama vinne hivi, mwishowe aliunda chake, hicho hata hakikuwa na ofisi. Nauliza hivi ukiwa CCM miaka 20, ukahamia chamakingine ukirudi CCM umri wako chamani unakuwa upi au unaunganishiwa? Nijibuni wajameni.

Pili, kuhusu kashfa hilo ni kweli. HANA KASHFA ya ufisadi hata chembe. Tumseme mengine lakini siyo ufisadi.

Tatu, kifamilia kidogo ana kadoa. Mara kesi za hapana pale na wanafamilia na hadi watoto wake wa kuzaa. Hilo linaweza kusemwa ni la binafsi, vinginevyo Wassira hana doa.
 
Wasira hana Kashfa?

Muulizeni alimfanya nini mama yake huyu jamaa:





Angejifunza kwa Mrema ambaye aligoma kurudi CCM pamoja na misukosuko yote aliyopata japo alikua anaipenda CCM.
Vijana waanze kuisoma historia ya huyu Shujaa Mrema aliyepoteza uwaziri kwa kupinga Ufisadi tofauti na hawa wanaojinadi kwmb niwapambanaji wa ufisadi huku waking'ang ania madaraka.
 
Wassira alirudishwa CCM-Mtandao na Rostam. Akapewa na hela nzuri za kwenda kugombea Ubunge na Rostam. Akafanya kazi nzuri sana ya uana-mtandao kati ya 1995-2005 kanda ya Ziwa.

Akapewa Uwaziri katika wizara mbalimbali. Ni fundi sana wa kuzitafuna kwa siri taasisi zilizo chini ya wizara anazoziongoza. Waulizeni TASAF wanavyohangaika naye sasa.

Anaandaliwa kuwa chaguo la pili endapo Lowasa atakwama.
 
Comment zako huwa zina upande mmoja tu, na Tatizo kubwa ni ushabiki wa kiitikadi ulionao.

Jaribu kutazama makala ya huyo bwana with 'Sober brain' yawezekana kuna jambo jema utaliona.

Oh wow --- NACHANGANYIKIWA... Naambiwa kuwa COMMENTs ZANGU hazieleweki -- Kwasababu Haijulikani kama niko UPANDE wa CHAMA TAWALA au UPINZANI naelemea CHADEMA... wewe unanipa KIITIKADI ni SHABIKI

Sasa Ni SHABIKI wa nani ? Kwani kweli hakuondoka CCM ? NYERERE hakumkandia ? Sasa hiyo TUITE NINI kwenye Demokrasia ya NCHI HII... KULINDANA ???
 
Yaania acha tu kaka...

Ni kwa sababu tumekosa UZALENDO.Kibaya kwetu kizuri na kizuri kwetu kibaya.Atakachosema mpinzani hata kama ni kizuri kitatafsiriwa ubaya na kitakachosemwa na CCM hata kama ni kibaya kitapewa uzuri.Inasikitisha sana.
 

Haya mambo ya mtandao ndio yanaipeleka nchi yetu pabaya. Hawa wana mtandao wanatuamulia rais kutokana na ujinga wetu.
 

Mleta mada nimesoma makala yako mwanzo hadi mwisho kwa utulivu, hakika ujumbe wako ni mzuri nilitamani uendelee kutoa story ya Ndugu Wasira.

Katika siasa kuna bahati na vipaji katika watu, kuna baadhi ya watu wanalazimisha siasa labda kwa sababu ya fedha zao au kwakuwa wao walikuwa watoto wa fulani au ukoo fulani.

Lakini tangu naanza kufuatilia siasa hizi za Tanzania nimegundua kuna watu wana mvuto sana na wamebarikiwa na Mungu kuwa na vipaji vya kuendesha siasa, Mmoja wao katika kundi hili ni Stephen Wasira.

Siwezi kusema sana lakini hotuba zake majukwaani na harakati zimekuwa zenye mafanikio sana, ukimsikiliza huwezi kuchoka, utacheka,utafurahi na utaelewa ujumbe anaokusudia kuufikisha.

Wasira anaweza kutoa hotuba according to level of listeners, kulingana na aina ya watu anaowahutubia na ujumbe unafika.
 
Acha kutudanganya! Umesahau kashfa ya kuuchapa usingizi bungeni?
 
UPOFU MWINGINE BHANA NI MBAYA SANA... yani wassira naye ni safi? Hv Tunasahau Au Tuajisahaulisha? Si Ni Huyuhuyu Aliyefungiwa Kugombea Ubunge Na Mahakama Kwa Miaka Mitano Kutokea 1997 Mpaka 2002 Kwa Kutoa Rushwa Kwenye Uchaguzi Aliomshinda Warioba??nzishe mpango maalum wa kumchunguza kihabari ili niwaoneshe Watanzania upande mwingine wa shilingi kuhusu Mwanasiasa huyo, lakini nakiri kuwa £¿nimeshindwa kumpata£¿ Wasira katika hilo.

Huyu ndiye Wasira ambaye Mwaka jana aliwatahadharisha Vijana wasomi wa Vyuo Vikuu kutumia taaluma zao kupambanua ukweli na uwongo wa vyama vya siasa ili wasiendelee kuwa wateja wa siasa uchwara na £¿wachumia matumbo£¿


Nimeshindwa kumpata WASIRA aliyeyasema hayo katika kongamano lililofanyika mkoani Mwanza na kushirikisha vyuo mbalimbali mkoani humo kikiwemo Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine Tanzania(SAUT).
Nimeshindwa kumpata kwani kati ya watu niliobahatika kuzungumza nao au niliosoma mandishi yao, hakuna aliyenipa kashfa hata moja inayomgusa Wasira tofauti
 
Kweli Watanzania mna AKILI ZA SAMAKI na WAVIVU WA KUUTAFUTA UKWELI?! Leo mwanaume mzima na ma****nde yake anakuja JF na kuuambia umma wa wa-Tanzania kwamba Wassira ni msafi hana doa lolote! Please give us a break. Wassira huyu alishawahi kupatikana na hatia ya kutoa RUSHWA mbele ya mahakama na kufungiwa kutogombea nfasi ya uongozi wowote katika Taifa hili kwa kipindi cha miaka 5. Watanzania wachache wanaopenda kuutafuta ukweli wanaweza kupata reference ya kesi hii (Warioba V Wassira) mahakama kuu. Wassira huyu huyu alishawahi kupatikana hatia before the court of law for a violence conduct baada ya kumpiga magumi hadharani mtu. hence JK kumbatiza jina la TYSON.
 
Usimtafute sana ngoja nikusaidie mahali pa kuanzia. Mulize akueleze na kisha utuambie kuhusu ile kashfa aliyopata pale aliposhitakiwa na Mh. Jaji Joseph Sinde Warioba na kumshinda katika kesi ya uchaguzi kwa kosa la kutoa rushwa kwenye uchaguzi na hivyo kufungiwa na Mahakama Kuu kushiriki masuala ya siasa kwa muda wa miaka mitano. Je, unalijua hili au hulijui. Kama unalijua basi tueleze! Vinginevyo yeye analijua na kama ni mkweli atakueleza na wewe utatueleza.
 

Ooh! Mungu atuepushe na BALAAA HILI.
 
Ana umri gani huyu mzee maana amekuwa mtawala tangu sijazaliwa hadi sasa nina zaidi ya miaka 40. Ndo maana taifa hili haliendelei akili zile zile miaka nenda rudi
 
Ana umri gani huyu mzee maana amekuwa mtawala tangu sijazaliwa hadi sasa nina zaidi ya miaka 40. Ndo maana taifa hili haliendelei akili zile zile miaka nenda rudi

Ana miaka 68, mwenye nguvu, Afya njema, heima na Busara.


 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…