Steve Nyerere achaguliwa kuwa kiongozi wa wasanii nchi nzima kueneza amani

warumi

R I P
Joined
May 6, 2013
Posts
16,218
Reaction score
18,440
WASANII wa Bongo Movie, muziki wa dansi, taarab, maigizo na tamthilia wametangaza kuzunguka nchi nzima wakiwa na kamati ya Tanzania Kwanza Nje
ya Bunge Maalum la Katiba kwa lengo la kutangaza amani kwa vijana wa rika lote bara na visiwani.

Baadhi ya wasanaii hao ni pamoja na Steven Mengele ‘Steve Nyerere' ambaye ameteuliwa kuwa msimamizi mkuu wa uwakilishi kwa upande wa wasanii katika Tanzania kwanza nje ya Bunge maalum, Muungano huo uko chini ya Mwenyekiti Augustino Matefu. Akizungumza juzi na waandishi wa habari
jijini Dar es Salaam, Steve amesema kwamba ataungana na wasanii ambao wako katika vyama mbalimbali kama vile Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, NCCR, Mageuzi , Cuf na vyama vingine huku wote wakiwa na lengo moja tu la kuhimiza mchakato wa katiba uendelee huku wanasiasa wakizingatia kudumisha amnai na umoja wa Watanzania.

Nyerere aliongeza kwa kusema kuwa yeye hakuwa na kipingamizi pindi alipoambiwa amechaguliwa kuwa miongoni mwa wasimamizi wa mpango huo ambao umewakutanisha vijana kutoka katika itikadi mbalimbali za vyama vya siasa. "Nilipoambiwa hili jambo niliweka itikadi zangu za chama pembeni na kuuvaa Utanzania kwanza ili kuunganisha fani zetu wote kwa pamoja na kuweza kuwahimiza wananchi wadumishe amani tuliyokuwa nayo nchini" alisema Nyerere.

Aliongeza pia kwa kuwaomba viongozi wa dini masheikh na maaskofu wakiwemo mapadri wote kuungana nao wasanii hao katika kuhimizaani ya amani ya nchi. "Sisi wasanii tunapata riziki zetu kutokana na amani na utulivu uliopo nchini mwetu hivyo kila msanii na Mmtanzania aone ni jambo la fedheha kuiichezea amani ambapo siku ikipitea tutakwenda kuomba hifadhi katika nchi za jirani zilizopata uhuru na kufuata ushauri kutoka kwetu"

Aliongeza kwa kusema kwamba ana imani kubwa watanzania watawaelewa pindi watakapokuwa katika ziara hiyo kuzunguka nchi nzima huku wakiwa na
mabalozi watano kutoka kila nyanja ya sanaa ambazo ni muziki wa taarab, Hip Hop, Sanaa za maigizo, Michezo na tamthilia. Mkutano mkubwa unatarajiwa
kufanyika Kibanda Maiti Zanzibar.


Amwambia Wema aepuke umaarufu wa bila kazi


 
Asante ameongea la maana big up kwake
 
Ngoja uone Wema atakavyo ibuka na kusema hamtambui na aache kumfalia na hapo ndipo watakapo anza kuuza vichwa vya habari vya magazeti ya
Shigongo.
Nahisi kuna kitu kina tafutwa hapa japo ametoa ushauri.
 
Ngoja uone Wema atakavyo ibuka na kusema hamtambui na aache kumfalia na hapo ndipo watakapo anza kuuza vichwa vya habari vya magazeti ya
Shigongo.
Nahisi kuna kitu kina tafutwa hapa japo ametoa ushauri.

Atasema anatafuta umaarufu kupitia yeye.
 
bonge ya point hiyo. Asiishie kupokea tuzo za watu tu nae afanye kazi apate zake
 
kasema ukweli mtupu umaarufu unakuwa nao lakini haujakuletea mafanikio miaka inaenda na asifikiri siku zote atakuwa kwenye peak kama ana masikio na asikie ushauri anaopewa
 
Afu kweli umaarufu shomboo tu! Hauna mashiko umri nao unakimbia...
 
Ngoja uone Wema atakavyo ibuka na kusema hamtambui na aache kumfalia na hapo ndipo watakapo anza kuuza vichwa vya habari vya magazeti ya
Shigongo.
Nahisi kuna kitu kina tafutwa hapa japo ametoa ushauri.

Ukweli ni kwamba wasanii bongo movie asilimia kubwa hawawezi kupambana na huyu jamaa refer kwanini wanamuita baba, wataishia kuongea pembeni pembeni mitonyo mingi wanapewa na steve kutokana na kufahamiana kwake na viongoz wakuu, wafanyabiashara wakubwa hivyo huwa wanamtumia kama daraja wanapomuhitaji.

Hasa hawa dada zetu wa bongo movie steve kawapigia sana chapuo kwa mhindi wa steps na sasa lukaza ili wauze
 
Hivi Kama kuna Mtu anaejua mafanikio ya wema kupitia Sanaa aorodheshe hapa...maana sioni kitu zaidi ya kuhongwa tu...
Hiyo sijui team yake wanaona nini sijui kwa huyu Mtu .
 

Toka nimjue leo ndio nimempenda kula5
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…