Pre GE2025 Steve Nyerere ampongeza Tundu Lissu kwa Uamuzi wa Kugombea Uenyekiti wa CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Msanii wa filamu na Mwenyekiti wa ‘Mama Ongea na Mwanao,’ Steven Mengele maarufu kama Steve Nyerere, amempongeza Tundu Lissu kwa kutangaza nia yake ya kugombea uenyekiti wa CHADEMA, akisisitiza kuwa ni haki yake kikatiba mradi anazingatia miko na katiba ya chama.

Kupitia ujumbe aliouandika, Steve alisema:

"Nimekusikiliza mara 100, nasema nimekuelewa. Ni haki yako kikatiba kugombea ilimradi huvunji katiba ya chama chako na miko ya chama chako. Ukijiona unatosha, basi muda wa kujipima kwa wanachama wenzako ni sasa kwa maslahi mapana ya umoja wenu."

Aliendelea kusema:

"Natamani hivi karibuni nimuone mgombea mwenza wako naye akijitokeza hadharani… Hongera Mwenyekiti."

Kwa utani, Steve akisema:

"Doo, tatizo mzigo ulikuwa unapita chumbani, sebuleni wakubwa mnakula upepo, wine, Hennessey kidogo… Lazima ubwage."


Pia, Soma:

Tundu Lissu atangaza nia ya kugombea nafasi ya uenyekiti CHADEMA

Tundu Lissu: Nimewasilisha kusudio la kugombea nafasi ya Mwenyekiti CHADEMA
 
Seriously??? Umeona huyu chawa ndio wa kumuongelea?
 
Huyo Steve mengele bado analilia majina ya watu tu??
 
Hili chawa chafu linapongeza au kujipendekeza kwa Lissu? Seeeengeee kubwa tu.
 
Kwa chama chake wagombea wao wangapi?
 
Acha kutuletea habari za vichaa, huyo Steve ni nani mpaka umpe umuhimu huo?
 
Haahaa dogo kaandika vizuri sana..m
 
Hawa uwezo wao mdogo sana CCM inapaswa iliende uongozi wa Mbowe kwa nguvu zote chama kikiwa chini ya Lissu hawatapata hata mtu wa kukaa naye kuzungumza kitu chochote
 
Sitashangaa kumsikia Katibu Mkuu au Katibu Mwenezi wa CCM anapongeza uamuzi huu wa Lissu. Pamoja na viongozi wa vyama vile vingine vya upinzani.

Amandla...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…