Stori: Usife haraka mpenzi wangu

Stori: Usife haraka mpenzi wangu

USIFE KWANZA MPENZI WANGU......EPISODE.38


“Deo naomba unisamehe kwa nitakalokuambia, najua litakuumiza na hutanielewa kirahisi, lakini ndiyo ukweli wenyewe. Naomba unielewe kwamba sikuwa na nia mbaya, nia yangu ilikuwa nzuri kabisa, lakini lazima unisamehe Deo!”

“Ni nini? Hebu niambie basi Levina...” akasema Deo akimkazia macho Levina.
“MIMI NDIYE NILIYEKODI WATU WAKUPIGE RISASI KWENYE LIFTI!” Levina akasema akilia.
“Unasemaje?” Deo akauliza kwa sauti ya ukali sana.
SASA ENDELEA...

HAIKUWA rahisi kwa Deo kuamini kwamba Levina ndiye aliyefanya jaribio la kutaka kumuua, moyo wake ulibadilisha mapigo na hasira yake kuwa kubwa. Aliyatoa macho yake akimwangalia Levina, akiwa haamini kabisa kwamba angeweza kufanya kitendo kile.

“Levina ulitaka kuniua?” Deo akauliza kwa hasira.
“Siyo hivyo mpenzi wangu!”
“Siyo hivyo vipi na umekiri kwamba ulituma watu wanipige risasi.
“Deo kabla sijakuambia lazima nikupe masharti ili nikusamehe. Ni kweli nilifanya kosa, lakini kosa lenyewe ni katika kulinda penzi langu!”
“Ulitaka kuniua au kunilinda?”

“Kwani uliuawa?”
“Hapana.”
“Kuna kitu uliibiwa?”
“Hapana!”

“Basi ndiyo unatakiwa kufahamu kwamba nilifanya hivyo kwa ajili ya kukupata. Deo sikuwa na njia nyingine, vinginevyo wewe ungefunga ndoa na Cleopatra. Sikiliza nikuambie Deo, mimi nakupenda sana, moyo wangu una mzigo mzito wa mapenzi ambayo siwezi kufananisha na kitu chochote.”
“Sijui kama ni rahisi kukuelewa!”

“Lakini unataka kuelewa?”
“Ndiyo!”
“Ngoja nikusimulie...” Levina akasema akikaa sawa sawa kwa ajili ya kumweleza kisa kizima kilivyokuwa.

***
Alikuwa amekaa mwenyewe kwenye meza ya peke yake, macho yake yakiangaza kila upande, ni kama alikuwa anawasubiri watu wafike katika baa ile. Ilikuwa ni usiku wa saa mbili na dakika zake, Levina ametulia kwenye kona akinywa soda yake taratibu kabisa.

Akiwa anaendelea kuangaza macho yake, simu yake ikaita. Haraka akapokea akiangalia kwenye mlango mkubwa wa kuingilia pale baa.
“Yes...” akatamka Levina akisubiri sauti ya upande wa pili.
“Ni wewe uliyekaa hapo kwenye kona peke yako?”
“Ndiyo!”

“Ok! Tunakuja, nimeshakuona!” Sauti nzito ya kiume ilisikika kwenye spika za simu ya Levina.
Dakika moja baadaye, wanaume watatu walikuwa wamekaa kwenye viti kuizunguka meza aliyokuwa amekaa yeye. Walisalimiana kisha wote wakakaa kimya.

“Karibuni sana, mimi ndiye Levina niliyemuagiza Asnath awatafute, nimefurahi kukutana nanyi!” Akasema Levina.
“Hata sisi pia.”
“Kama Asnath alivyowaambia, sina haja ya kumuua huyo jamaa, hakikisheni mnampiga risasi ya bega, nataka alazwe, mambo mengine nitamaliza mwenyewe!”

“Unataka hiyo kazi ikamilike baada ya muda gani?” Mmoja wao akauliza.
“Ndani ya wiki moja kutoka sasa, unajua amebakiza siku chache sana kabla ya kufunga ndoa, ni hiyo ndiyo ambayo sitaki ifungwe!”
“Sawa, chetu?”

“Ninazo...naona niwalipe nusu kwanza, kazi ikikamilika nitawamalizia. Chukua hii...” akasema Levina akimkabidhi bahasha iliyovimba!
“Ahsante sana, hatuna muda wa kusubiri zaidi, kila kitu umeshatuelekeza kwenye simu, namba yake ya simu tunayo, anapofanyia kazi tunapajua, kazi iliyobaki ni ndogo sana, ni kumfuatilia baasi!”

“Sawa, nawatakieni kazi njema yenye mafanikio!”
“Itakuwa hivyo, usijali!”
“Ok! Poa.”
Wale vijana wakasimama na kumuacha Levina akiwa amekaa kimya sehemu ile. Moyoni mwake alitamani sana zoezi lile likamilike, hakutaka kabisa Cleopatra afunge ndoa na Deo, mwanaume wa maisha yake.

“Tutaona sasa, mimi si katili, lakini wakati mwingine inabidi ili niweze kutetea penzi langu, naamini sasa nitafanikiwa,” akawaza Levina akisimama na kutoka katika baa hiyo.

***
Deo aligandisha macho yake usoni mwa Levina akiwa haamini kabisa anachosimuliwa, hakutegemea kama Levina angefanya tukio kubwa kiasi kile.
“Lakini levina hukuwa na njia nyingine zaidi ya hiyo?” Deo akamwuliza akiwa ameyatoa macho yake.

“Unadhani ningetumia njia gani hapo? Hata kama ni wewe ungetumia njia gani?”
“Kwanini usingenitafuta tukaongea?”
“Deo ulikuwa unatafutika wewe? Hata simu yangu ulikuwa unaiona kama kinyaa, sikuwa na njia nyingine Deo, naomba unisamehe lakini nitakusamehe kama na wewe utanisamehe na kutimiza ahadi zako zote!”

Deo akatulia kwa muda akatafakari, aliyaona makosa yake lakini pia aligundua kwamba Levina hakuwa na njia nyingine ya kufanya zaidi ya tukio alilolifanya ambalo liliweza kuwarudisha tena pamoja.

Alipata maumivu makali sana, aliteseka sana hospitalini, lakini mwisho wa siku aligundua wakulaumiwa ni yeye mwenyewe. “Nimekusamehe Levina!”
“Nimekusamehe pia Deo!”
“Sasa?” Deo akauliza akiwa anamwangalia Levina machoni.
“Nini tena mpenzi wangu?”

“Kuhusu ndoa, itawezekana kweli kuoana?”
“Nini kinachoshindikana chini ya jua?”
“Wazazi wako baby, hawanitaki kabisa hilo ndiyo tatizo.”
“Kuna kitu nilikuwa sijakuambia sweetie!”
“Kitu gani?”

“Nilishaongea na mama kila kitu...hakuna tatizo tena, mzee Massamu huwa haongei kwa mkewe Diana. Lazima kieleweke, kwa hiyo ondoa shaka mpenzi wangu. Tutapanda madhabahuni na kufunga ndoa yetu!”
“Kweli dear?” Deo akauliza akiwa ametoa macho.
“Niamini mimi mpenzi wangu!”

Deo na Levina wakasimama, kisha wakakumbatiana. Hawakuogopa macho ya watu. Walichojua wao ni kitu kimoja tu, kuwa wanapendana!
Kama Levina alivyosema, haikuwa kazi ngumu mama yake kumshawishi baba yake mzee Massamu kuhusu Deo kumuoa Levina hasa kwa kuwa tayari alikuwa na sifa walizokuwa wanazihitaji.

Deo akasafiri hadi nyumbani kwao Singida, akawaeleza wazazi wake juu ya kupata mchumba, hakuna aliyepingana naye. Taratibu zote zikafanyika, ndoa ya kifahari ikafungwa jijini Dar es Salaam.

Watu wengi sana walihudhuria, akiwemo Cleopatra ambaye tayari walishaweka mambo sawa. Mama yake Cleopatra ndiye aliyewakutanisha na kuwapatanisha. Jambo la kushangaza zaidi, Cleopatra ndiye alikuwa Mweka Hazina wa kamati ya sherehe ya Deo na Levina.

Ukawa mwisho wa machozi kwa Levina na mwanzo wa maisha ya furaha, akiwa na mwanaume aliyeota kuwa naye, mwanaume aliyemuhangaikia kwa muda; aliyekuwa tayari kufanya chochote kwa ajili yake.
Mwanaume wa maisha yake!

UNLIMITED SWAGGAZZ:.

Nawashukuru sana wasomaji wangu wapenzi kwa kufuatilia simulizi hii kuanzia mwanzo hadi mwisho, naamini haijakuacha kama ulivyokuwa, kuna kitu umejifunza.
Ila kama story itakuwa Imekukela wala Hukuifraiya

Samahan

*********MWISHO************
A very captivating story. One of its kind. I have enjoyed reading it.
 
USIFE HARAKA MPENZI WANGU

HANA haraka anapotembea, ukimtazama anaonekana kujiamini sana. Tabasamu mwanana linaupamba uso wake, lakini mavazi yake yanaonesha asivyo mtu wa dhiki! Hata kama siyo sana, lakini uwezo wa kubadilisha mboga ulikuwa mikononi mwake!

Anatoka kwenye duka hili maalum kwa kuuza kadi na zawadi mbalimbali lililopo ghorofa ya saba, katika jengo moja la KPC Towers, katikati ya Jiji la Dar es Salaam. Anatembea taratibu kuifuata lifti iliyokuwa mita chache sana mbele yake.

Anatabasamu!

Ni kweli anatabasamu!

Tena basi alikuwa na kila sababu ya kutabasamu, maana zilibaki wiki tatu tu, kabla ya ndoa yake na mpenzi wake wa siku nyingi Cleopatra ifungwe.

Mkononi mwake ana bahasha ya khaki ambayo ndani yake kuna zawadi kwa ajili ya Cleopatra wake. Alijua anachotakiwa kumfanyia Cleopatra!

Siku zote alikuwa akinunua apple tu, mambo yanakuwa sawa! Huo ulikuwa ugonjwa mkubwa zaidi kwa Cleopatra.

Alipoifikia, akabonyeza kitufe fulani mlangoni, mlango ukafunguka. Akaingia na kusimama, punde mlango ukajifunga, akabonyeza kwenye herufi G akimaanisha kwamba anataka kushuka chini!

Ni kijana mtanashati sana, anayevutia kwa kila mwanamke aliyekamilika.

Anaitwa Deogratius Mgana. Mfanyakazi wa shirika moja lisilo la kiserikali jijini Dar es Salaam. Ana furaha moyoni mwake, maana anakwenda kufunga ndoa na chaguo lake.
Kwanini asitabasamu!

Hakika ana haki ya kutabasamu!

“Ni kweli lazima nitabasamu, kwanza nusu ya ndoto zangu tayari zipo kwenye mstari. Lazima nijisikie vizuri,” akawaza mwenyewe akiwa kwenye lifti.

Akabaki ametulia kimya akiwa amesimama kwenye lifti ile, ikaanza kushuka taratibu kwenda chini. Ghorofa ya sita, ghorofa ya tano, ghorofa ya nne...

alipofika ghorofa ya tatu, lifti ikasimama. Hapo akajua kuna mtu aliyekuwa akitaka kushuka chini. Mlango ulipofunguka, wakaingia wanaume watatu, wote wamevaa miwani za jua.

“Mambo bro?” Mmoja akasalimia.
“Poa,” akaitikia Deo.

Lifti ikaanza kushuka taratibu, walipofika ghorofa ya tatu, ikasimama. Mlango ulipofunguka tu, ghafla wale vijana watatu wakamsukuma hadi nje. Mara mlango ukafunga.

“Paaaaaa!” Mlio wa risasi ukasikika.
Deo akaanguka chini, akianza kuvuja damu!


* * *

Alisikia vizuri sana mlio wa simu yake, lakini aliamua kupuuzia! Si kwamba hakutaka kwenda kupokea, lakini alikuwa na kazi muhimu sana aliyokuwa akiifanya, zaidi ya kwenda kupokea simu!

Cleopatra alikuwa anapika!

Chakula kizuri ambacho mpenzi wake alikuwa anakipenda sana. Alikuwa anapika viazi vya kukausha, maarufu kama maparage, ambavyo Deo alikuwa akipenda sana.

Siku hiyo Deo alipanga kwenda nyumbani kwa akina Cleopatra, Mikocheni.

Ilikuwa zimebaki wiki tatu tu ndoa yake na Deo ifungwe. Siku ambayo alikuwa akiitamani sana na kuomba ifike haraka.

Mlio wa simu yake ukaisha ghafla. Akaendelea na mapishi yake jikoni, lakini baada ya muda mfupi sana, simu ikaita tena kwa mara nyingine...

“Nani huyo aaah!” Cleopatra akasema kwa hasira kidogo.

“Mi’ nampikia Deo wangu bwana alaaah!” Akasema tena, akifunika kile chakula jikoni na kufunga kanga vizuri.

Yap! Kama ungekuwepo, ungeamini kweli Cleopatra alikuwa mwanamke mrembo.

Pamoja na kwamba alikuwa amevaa kanga, lakini umbo lake lenye namba nane liliweza kuonekana vyema kabisa. Cleopatra alijaaliwa umbo zuri sana la kuvutia.

Ona anavyotembea...
Kama anaionea huruma ardhi. Ana hips pana zinazozidisha uzuri wake, ana macho mazuri yenye uwezo wa kumchanganya mwananaume yeyote yule. Labda niseme kwamba, Cleopatra alikuwa mwanamke mrembo sana.

Alivyofika sebuleni, simu ikaacha kuita. Akachukia sana, lakini akiwa anainua ili aweze kujua aliyekuwa akimpigia ili aweze kumpigia tena, akashangaa simu yake ikianza kuita tena. Kwenye kioo cha simu yake likaonekana jina ‘My Deo’!
“Jamani, kumbe ni sweetie!”

Akasema akibonyeza kifufe cha kijani ili kumsikiliza.
Ilikuwa ni namba ya Deo ikionekana kwenye kioo cha simu yake..
.
“Yes baby, najua hujasahau kuninunulia apple na napenda kukujulisha kwamba, maparage yako yanakaribia kuiva, ila sijui ungependa nikuandalie juice ya nini?

Machungwa, maparachichi, maembe au mananasi? Maana kila kitu kipo kwenye friji!” Cleopatra akasema kwa sauti iliyojaa mahaba mazito sana.

“Samahani dada, mimi siyo mwenye simu!” Sauti hii ya kiume, tulivu yenye mikwaruzo kwa mbali ilisikika kwenye simu ya Cleopatra.
“Sasa kama wewe si mwenye simu, kwanini umepiga? Kwanini unakosa ustaarabu?”

Cleopatra akamwuliza yule mtu akiwa na hasira sana.

“Samahani sana dada’ngu, lakini nadhani ni vyema ukawa mtulivu na kuuliza kilichotokea. Si kawaida mtu kupiga simu isiyo yake kwa watu ambao wamehifadhiwa kwenye simu hiyo.

Hiyo ingetosha kabisa kukufanya ugundue kwamba kuna tatizo!” Mtu huyo akasema akizidi kuonesha kwamba anahitaji utulivu wa Cleopatra.

“Ndiyo...enhee kuna nini?

Hebu niambie, maana tayari nahisi nimeanza kuchanganyikiwa!”
“Sina shaka wewe ndiye Cleopatra!”
“Ndiyo!”

“Ni nani wako?”

“Ni mchumba’ngu, kwani vipi?”

“Usijali, tuliza moyo dada yangu.

Mimi ni Dk. Palangyo wa Hospitali ya Taifa Muhimbili. Huyu ndugu mwenye simu, ameletwa hapa na wasamaria wema, baada ya kupitishwa katika Kituo cha Polisi Oysterbay!”
“Anaumwa na nini dokta?” Cleopatra akauliza akianza kulia kwa huzuni.

“Amepigwa risasi na watu wasiojulikana katika Jengo la KPC Towers.

Hata hivyo, hana hali mbaya sana, matibabu yanaendelea, lakini nimeona ni vyema kukujulisha ili uwafahamishe na ndugu wengine!”

“Asante dokta kwa taarifa, baada ya nusu saa nitakuwa hapo,” Cleopatra akajibu akizidisha kilio chake.

Akatoka mbio, hadi chumbani kwake. Hakukumbuka kwenda kuipua chakula jikoni. Akavaa haraka na kutoka hadi getini! Ghafla kumbukumbu zake zikarudi!

“Mama yangu, nimeacha chakula jikoni na jiko linawaka,” akawaza akirudi ndani mbio.

Ilikuwa ni hatari sana, maana alikuwa anapikia jiko la umeme. Mara moja akarudi ndani na kuzima jiko, akaipua kile chakula na kutoka kwa kasi sana.

“Wewe vipi mwenzetu, mbona hivyo?” Mama yake Cleopatra akamwuliza baada ya kumuona mwanaye anaonekana kuwa na haraka ambayo hakujua ni ya nini.
“Nitakupigia simu mama!”

“Unakwenda wapi?”

“Mama nitakupigia!”

“Patra, mwenzako si anakuja au haji tena?”

“Mama Deo amepigwa risasi, yupo hospitalini,” akasema Cleopatra akiwa tayari ameshaingia kwenye gari.

Akapiga honi kwa nguvu, mlinzi akafungua haraka. Cleopatra akaondoa gari kwa kasi sana. Alikuwa anakwenda Muhimbili, huku nyuma akiwa amemuacha mama yake akiwa mwenye mawazo.

Episode Ya 2 Inakuja
Hahaha
 
Back
Top Bottom