Kuna food hapa?Karibu kijiweni ndugu!
Kuna stori huwa hazina mwenyewe, kila kijiwe zina mhusika tofauti... Yaani hata wewe ukiwa wa kwanza kuisimulia kwenye hicho kijiwe unajivisha uhusika mkuu.Kijiweni bhana!
iwe kwenye kahawa,drafti,kwa fundi baiskeli...kwa fundi wa kushona nguo,stori ni kiungo muhimu sana kuliko kitu chochote mahali hapo...mara Simba mara Yanga,Man U mara Chadema mara makinikia...Tshishimbi mara Niyonzima..
Ikiisha hii inakuja ile,siasa mara uchawi[simtaja mshana jr],kila mtu kijiweni ni muongeaji,asipoongea atacheka,akiondoka anaenda kuhadithia..
Kijiweni ni sehemu yenye mambo mengi sana,utasikia hata idadi ya pasi alizopiga Ajibu kwenye mechi..
Ebu ngoja niende kijiweni nitakachosikia nitakuja kuwaambia...
Kila kitu usawa huu nagongaMakande unakalaga?
Kuna stori huwa hazina mwenyewe, kila kijiwe zina mhusika tofauti... Yaani hata wewe ukiwa wa kwanza kuisimulia kwenye hicho kijiwe unajivisha uhusika mkuu.
Sasa kuna mwana akaja na stori kuwa yeye ana 'kirago' chake Segerea kwa hiyo haogopi kwenda jela, siku pila limetinga maskani na yeye akazolewa. Kufika kituoni wakamkuta kajikojolea...
Uhakika?Basi utapata bila shida yoyote..