Man Middo tz
Senior Member
- Sep 9, 2020
- 182
- 279
SIMULIZI: KIJANA SHUJAA….. “Ilikua ndoto yangu kuja kufanya jambo kwaajili ya Taifa”
SEHEMUYA KWANZA (01)
Man Middo
Kabla hajatimiza ndoto yake kijana shujaa alikua kapuku tu muuza dagaa katika mwalo wa Nyamkazi, Bukoba pembezoni mwa ziwa victoria. Kwa muonekano wake hata wewe unaesoma usingeamini kama angekwambia ana ndoto ya kuja kufanya jambo kubwa kwaajili ya Mama Tanzania.
Jambo ambalo litashtua nchi, jambo ambalo litafanya jina lake liwe “TRENDING” hadi mtandao wa Google.
Ilikua ni asubuhi ya Novemba 6, 2022, anga ikiwa ang’avu kabisa. Taarifa zinasema hali ya hewa ilikua shwari kabisa wakati ndege inapaa. Watu 43 ndani ya ndege, rubani, wahudumu na abiria wote wakiwa wameaga katika familia zao na kutakiwa kheri katika safari.
Katika kuperuzi peruzi mara ghafla Millard Ayo huyu hapa…… Breaking news… mganga mkuu wa mkoa wa Kagera Dr. Isesanda Kaniki amesema hadi sasa ni watu watatu wamefariki kutokana na ajali ya ndege ya Precision Air iliyotokea asubuhi ya leo Ziwa Victoria wakati ikitua.
“Tumewapokea ndugu zetu 26 wakiwa hai, wanaume 17 na wanawake 9 lakini pia tumewapokea ndugu zetu wengine watatu wakiwa wamefariki, “Ni wanaume wawili na mwanamke mmoja, uokoaji unaendelea, kwa walio hai huduma zinaendelea kutolewa hali zao ziko vizuri”
Umma ukajiuliza ni nani shujaa katika hili? Ndege ilikua na watu wa ngapi? Watu 26 wameokokaje na wengine 19 kufariki? Mara taarifa ikatoka wakati watu wakijiuliza maswali mengi
“Ndege ilikua imebeba watu 43 ambapo hadi sasa wameokolewa 26 tu na kupelekwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa kagera. Japo mkuu wa mkoa hajsema watu hao wameokolewa vipi na muda gani, Mashuhuda wanasema wameokolewa sekunde chache baada ya ajali kabla sehemu kubwa ya ndege hiyo kufunikwa na maji. Kwa upande mwingine mkuu wa mkoa amewaomba wananchi kuendelea kuwa watulivu maana mawasiliano na marubani walioko ndani ya ndege bado yanaendelea” ilifafanua taarifa ya Millard Ayo.
Wakati mashuhuda wakielezea namna wanavyodhani watu wameokokaje kumbe muokozi ni kijana shujaa na wakati huo ni miongoni mwa hao watu 26 waliotajwa kuokoka kutoka kwenye ajali ya ndege? Mimi na wewe hatukujua tuendelee kusoma Breaking news zilisemaje siku ile…
Kufika mchana taaifa ikatoka ni Yule Yule mzee wa mastori na breaking news anasema “Zoezi la uokoaji linaendelea hapa Nyamkazi, Bukoba ilikopata ajali ndege ya Precision leo asubuhi ambapo vikosi uokoaji na watu mbali mbali wameendelea kuongeza jitihada ili kuitoa Ndege hiyo ndani ya ziwa”
“Baada ya zoezi la kuivuta Ndege kwa kamba kuonekana kutofanikisha uokoaji kama ilivyotarajiwa, waya na kamba ngumu zimeongezwa kwenye eneo la tukio pamoja na magari maalum ya kunyanyulia na kuvutia vitu vizizo ili kurahisisha uvutaji huo” (Kumbe kijana shujaa alipigwa na hiyo kamba na kuzimia) ………………ITAENDELEA.
SEHEMUYA KWANZA (01)
Man Middo
Kabla hajatimiza ndoto yake kijana shujaa alikua kapuku tu muuza dagaa katika mwalo wa Nyamkazi, Bukoba pembezoni mwa ziwa victoria. Kwa muonekano wake hata wewe unaesoma usingeamini kama angekwambia ana ndoto ya kuja kufanya jambo kubwa kwaajili ya Mama Tanzania.
Jambo ambalo litashtua nchi, jambo ambalo litafanya jina lake liwe “TRENDING” hadi mtandao wa Google.
Ilikua ni asubuhi ya Novemba 6, 2022, anga ikiwa ang’avu kabisa. Taarifa zinasema hali ya hewa ilikua shwari kabisa wakati ndege inapaa. Watu 43 ndani ya ndege, rubani, wahudumu na abiria wote wakiwa wameaga katika familia zao na kutakiwa kheri katika safari.
Katika kuperuzi peruzi mara ghafla Millard Ayo huyu hapa…… Breaking news… mganga mkuu wa mkoa wa Kagera Dr. Isesanda Kaniki amesema hadi sasa ni watu watatu wamefariki kutokana na ajali ya ndege ya Precision Air iliyotokea asubuhi ya leo Ziwa Victoria wakati ikitua.
“Tumewapokea ndugu zetu 26 wakiwa hai, wanaume 17 na wanawake 9 lakini pia tumewapokea ndugu zetu wengine watatu wakiwa wamefariki, “Ni wanaume wawili na mwanamke mmoja, uokoaji unaendelea, kwa walio hai huduma zinaendelea kutolewa hali zao ziko vizuri”
Umma ukajiuliza ni nani shujaa katika hili? Ndege ilikua na watu wa ngapi? Watu 26 wameokokaje na wengine 19 kufariki? Mara taarifa ikatoka wakati watu wakijiuliza maswali mengi
“Ndege ilikua imebeba watu 43 ambapo hadi sasa wameokolewa 26 tu na kupelekwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa kagera. Japo mkuu wa mkoa hajsema watu hao wameokolewa vipi na muda gani, Mashuhuda wanasema wameokolewa sekunde chache baada ya ajali kabla sehemu kubwa ya ndege hiyo kufunikwa na maji. Kwa upande mwingine mkuu wa mkoa amewaomba wananchi kuendelea kuwa watulivu maana mawasiliano na marubani walioko ndani ya ndege bado yanaendelea” ilifafanua taarifa ya Millard Ayo.
Wakati mashuhuda wakielezea namna wanavyodhani watu wameokokaje kumbe muokozi ni kijana shujaa na wakati huo ni miongoni mwa hao watu 26 waliotajwa kuokoka kutoka kwenye ajali ya ndege? Mimi na wewe hatukujua tuendelee kusoma Breaking news zilisemaje siku ile…
Kufika mchana taaifa ikatoka ni Yule Yule mzee wa mastori na breaking news anasema “Zoezi la uokoaji linaendelea hapa Nyamkazi, Bukoba ilikopata ajali ndege ya Precision leo asubuhi ambapo vikosi uokoaji na watu mbali mbali wameendelea kuongeza jitihada ili kuitoa Ndege hiyo ndani ya ziwa”
“Baada ya zoezi la kuivuta Ndege kwa kamba kuonekana kutofanikisha uokoaji kama ilivyotarajiwa, waya na kamba ngumu zimeongezwa kwenye eneo la tukio pamoja na magari maalum ya kunyanyulia na kuvutia vitu vizizo ili kurahisisha uvutaji huo” (Kumbe kijana shujaa alipigwa na hiyo kamba na kuzimia) ………………ITAENDELEA.