Story ya kurudi kwa Juma Kaseja, Aishi Manula na Rais wa Dar

Hata kama, ila ndo ana kazi sana, kutetea namba yake tena pale,

Hata mtoto mdogo, hatakubali Mechi muhimu apewe Manula Kaseja aachwe
 
Kongole! Kweli usemayo
 
He will win that battle so easy
Hata kama, ila ndo ana kazi sana, kutetea namba yake tena pale,

Hata mtoto mdogo, hatakubali Mechi muhimu apewe Manula Kaseja aachwe
 
Miaka 19 anacheza soka hakuwahi kupata kipimo aje kukipata leo kwenye mechi ya Sudan!!!

Acha kuchekesha watu. Hao magolikipa wazuri watakaompiku Kaseja wamepata vipimo lini wao?
I'm done kwaheri
 
Juma ni kipa bora wa muda wote Tz,ila timu za kariakoo ndizo zinazostaafisha wachezaji mapema sana,yaani wakikukataa tu nawewe ukakosa msimamo lazima upotee kweli
 
Na hata sisi SIMBA hatukuamini katu ile Match na UD SONGO eti kipa MANULA na sio KAKO
Yule Manula hawezi kufua dafu mbele ya Kakolanya. Ana kiwango kisichoweza kuelezeka kama ni kizuri au kibaya.

Ila Beno ni kipa mzuri muda wowote.
 
I'm done kwaheri
Sawa nenda ila tambua Kaseja hawezi kupata kipimo leo. Kuna makosa ya kipa na makosa ya safu ya ulinzi, huko KMC kuna makosa ya safu ya ulinzi na siyo makosa ya golikipa.

Manula ambaye anasemwa kuwa Tanzania 1 ana matatizo yake yeye kama yeye.
 
Sasa mkuu hapo golini tufanye yupo De Gea halafu beki ndo Baba Swalehe na Hance Mtanashati Wanyarwanda wataacha kumtungua kweli?!
 
Mkuu binadamu tumejaa unafiki sana tena sana! Wakati Manula anapewa ile 10 mil hakuna aliekuja humu ndani kusema manula kapendelewa.

Maana kila mtu anakumbuka ile mechi ya Mazembe Ugenini kazi aliyofanya kila Mtu akakiri kua Manula kwasasa ndie Tanzania 1

Leo watu wanakuja na unafiki humu kua manula nikipa mbovu. Hakuna asieujua uwezo wa Kaseja ni kipa Mzuri na bora, umewatofautisha vizuri sana.

Mkuu umemaliza kwahayo maelezo.
 
Hakika mkuu mashabiki mara nyingi hujaji mambo kwa hisia za muda mfupi tu.
 
F
Buffoon kipawa chake kilishakwisha zamani tu!
Kaseja umeishi ukimwona tangu ujanani ujana gani huo?
.
Kaseja mpaka sasa bado ni kijana sio mzee yule.
Kipimo sahihi nimeshakitaja ambacho ni Sudan na timu itakapopangwa kwenye makundi ya FIFA
Unampima kaseja dhidi ya Sudan?
Kaseja aliyeanza kudaka ligi kuu 2000?
Kaseja wa 2003 dhidi ya Zamalek?
Kaseja yupi anayehitaji kipimo?
 
Kila golikipa Ana kitu chake tofaut na inategemea na mechi siku hiyo ya mchezo hupaswi kubeza mmoja kwa kuwa mwingine amefanya vizur baadhi ya Mechi hata Dida walimsifu hivohivo leo yuko wap?
 
F

Unampima kaseja dhidi ya Sudan?
Kaseja aliyeanza kudaka ligi kuu 2000?
Kaseja wa 2003 dhidi ya Zamalek?
Kaseja yupi anayehitaji kipimo?
Kaseja wa KMC sio kaseja wa Simba
 
Na hata sisi SIMBA hatukuamini katu ile Match na UD SONGO eti kipa MANULA na sio KAKO
Kocha tu alishikwa na homa ya mabusha anaenda kumpanga Manula aliyetoka kwenye majeruhi.
 
Mmeadili gia angani tena. Si mlidaí timu imelaaniwa kisa rais w dar anaisapoti?
 
Mwezi February mwaka huu aliandika mwandishi Charles Abel.

Gazeti la Mwanaspoti.

SIDHANI kama linaweza kuwa jambo la kushangaza iwapo kipa wa KMC, Juma Kaseja atarudishwa kwenye Kikosi cha Timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ siku za usoni baada ya kuwa nje kwa zaidi ya miaka mitano.

Wengi wanamuona Kaseja kama amezeeka na huu ni wakati wa kuwapa nafasi vijana lakini zipo sababu kadhaa za msingi ambazo zinalazimisha Kaseja (34) kupewa nafasi kwa mara nyingine kwenye kikosi cha Stars. Kwanza amekuwa akifanya vizuri kwenye Ligi Kuu msimu huu na ni miongoni mwa makipa wachache waliocheza idadi kubwa ya michezo bila ya kuruhusu nyavu zao kutikiswa (clean sheet).

Kipa huyo amecheza zaidi ya mechi nane bila nyavu za KMC kutikiswa katika mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu. Ni makipa wachache wazawa ambao kitakwimu wanamzidi ama wapo sawa na Kaseja. Kimsingi mchezaji aliye kwenye fomu ndani ya nyakati husika ndio anatakiwa apewe nafasi katika Stars kwa sababu huwa sio cha majaribio. Lakini sababu nyingine inayomfanya Kaseja astahili kuwemo kwenye kikosi cha Stars ni kiwango cha chini kinachoonyeshwa na makipa ambao ndio wana mwelekeo wa kuitwa kwenye timu hiyo kulingana umri wao na uzoefu. Makipa wazawa wamekuwa wakifanya makosa ya kizembe ambayo ni nadra kuyaona kwa Kaseja hasa katika kucheza mipira ya krosi pamoja na nidhamu ndani ya uwanja.

Ndani ya kipindi cha siku nne tu zilizopita tumeshuhudia Ramadhani Kabwili, Metacha Mnata na Deogratias Kisembo wakifanya makosa mepesi ambayo yalizizawadia timu pinzani mabao mepesi.

Wakati wengine wakivurunda ndani ya uwanja, unakutana na taarifa za kipa mwingine wa Mtibwa Sugar, Benedictor Tinoco kumkanyaga kwa makusudi mchezaji wa timu pinzani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…