Story za udokozi

Story za udokozi

Tuttyfruity

JF-Expert Member
Joined
Dec 3, 2017
Posts
2,414
Reaction score
6,371
Habarini wana JF

Nani hapa hajawahi kudokoa mboga jikoni? Aise! mimi nilikua mdokozi matata sana yani mama alikua anapenda kuchemsha nyama pamoja na viazi kabla ya kuunga mboga. Navizia jikoni hamna mtu nadokoa huyo nasepa.

Sasa kama wasemavyo wahenga za mwizi arubaini. Siku ya siku nikaingia jikoni kama kawaida yangu, nakumbuka nilikua na miaka 5 au 6 hivi, baada ya kuhakikisha usalama wangu nikafunua sifuria.

Kuna nyama na viazi vinachemka si nikasema leo ngoja nidokoe kiazi maana kinaonekana kikubwa kuliko nyama. Chap nikakitumbukiza mdomoni mara nikamsikia mama anakuja si nikasema nimeze tu haraka kabla sijafumwa.

Kumbe bwana ile na meza tu lahaula si kiazi cha moto yani. Mama akanikuta natoa macho akaniangalia akasema " wewe utakufa kwa kupenda kudokoa" [emoji23] toka siku hiyo sijawahi kudokoa kiazi tena , ni nyama kwenda mbele. Mpaka leo nimekua mdada. Sikubali kupika nyama labda angalau iwe nusu kilo na kuendelea maana wengine mtakunywa mchuzi tu.

Kuna siku tena mjomba alinipa sigara nikaiwashe jikoni, baada ya kuwaisha nikajisemea ngoja nitest mitambo kama imewaka basi nikavuta kidogo, kumbe bwana sigara kule sehemu ya kuvutia kuna kama ka sponge hivi kanafyonza mate , kumpelekea mjomba akavuta fundo moja akaniambia wewe kwann umevuta sigara yangu? Nikabisha[emoji23] akasema usirudie tena .

Kuna zile unapewa soda ukamfungulie mgeni alafu unapiga fundo moja ndo unaleta [emoji23].

Share story yako ya udokozi tujuane wazee wa kuonja chumvi.
 
Boyfriend wangu ananiulizaga yan wewe huwez kupika bila kudokoa [emoji23] sema mazoea hujenga tabia

Sent From Galaxy S20 Ultra

Udokozi hauishii jikoni tu, ila na we robo kilo nyama unakulaje.... maisha haya..!!
 
K
Boyfriend wangu ananiulizaga yan wewe huwez kupika bila kudokoa [emoji23] sema mazoea hujenga tabia

Sent From Galaxy S20 Ultra
Kumbe bado mnadokoana hamjaoana bado,,,kweli tabia hujenga mazoea
 
Nilipokuwa mdogo nilikuwa nadokoa sana samaki. Wale sato wakavu ambao mpaka uwavunje vipande ndo wapikwe (mojawapo ya chakula ninachomiss hapa Dsm). Siku moja nikadokoa tena ugenini, mamdogo akatuita wote watatu alipogundua upungufu wa mboga. Wale wawili kila mmoja anaongea kwa kujiamini si mimi mama, mi nimekodoa tu. Next time nikakamatwa natafuna nikaambiwa hakuna kumeza[emoji23].

Mzee mmoja jirani akatutaka watoto wote tuache kudokoa akatuonesha chumba flani cha kupangisha kibovu kuwa atakayeiba anakaa jera. Wakauliza maana ya jera akatueleza tukaogopa sana, muda wote anasema bado sikutakiwa kumeza. Alipomaliza nikaruhusiwa kumeza na tokea siku hiyo kile chumba tukawa tunakiita jera. Niliacha.
 
Ktu siach n pilau yani mm
Nkipata popote iwe jikon au
Kwenye friji lazma niweke hapo
Kijiko[emoji3][emoji3][emoji3]

stidy
 
Nakumbuka kipindi niko primary std 5 au 6, kuna ndugu yetu alikuja home.... alikua mtu wa vyombo sana so ikanunuliwa konyagi kwa ajili yake maana hakuna mwingine alikua anatumia hyo kitu pale nyumbani.
Hyo siku baada ya kunywa kiasi nikatumwa kwenda kuitunza, sasa nmefika nlipotakiwa kuiweka nikaiangalia then nikawa natamani kujua ina ladha gani, akili ya utoto ikaniambia onja😂 basi nikamimina kwenye kifuniko chake then nikabugia daah sitasahau hyo siku niliunguaaaa kuanzia kwenye koo had ilipofikia tumboni nikawa naiskilizia.
Nlitamani kulia kuomba msaada ila nlijua kitu ambacho kingenipata so nikajikaza nkaenda kujipooza na maji kuzima moto tumboni.
Since then nkawa muoga kudokoa vitu nisivyovijua.
 
Back
Top Bottom